Egnecious
JF-Expert Member
- Jul 8, 2015
- 894
- 994
Askofu Josephat Gwajima ni mwanasiasa ambaye amekuwa kwa mara kadhaa akitoa matamko na misimamo ambayo inalenga kumtengenezea umaarufu yeye binafsi kwa maslahi yake mwenyewe.
Ikumbukwe mwaka 2019 ziliposambaa mtandaoni picha za ngono ambazo yeye mwenyewe baadae alijitokeza na kusema zimetengenezwa na maadui zake ili kumnyamazisha huku akisisitiza kuwa wamejaribu ila hawawezi kumnyamazisha alilenga kujipatia umaarufu kupitia mfululizo wa majuma kadhaa ambayo alikuwa alitoa hotuba za kujitangaza binafsi kama sehemu ya kujitetea ili ajipatie wafuasi wengi zaidi mitandaoni na kwenye jamii kwa ujumla.
Pia soma: Pre GE2025 - Askofu Gwajima: Wakuu wa Vyombo vya Usalama wasiondolewe kwenye nafasi zao kwa mapenzi ya mwanasiasa aliyewaweka
Mwaka 2020 wakati Serikali imetangaza upatikanaji wa chanjo ya CORONA, Gwajima alitumia fursa hiyo kutangaza misimamo ya kushangaza akihamasisha watu kuwa ‘HATUCHANJI’ kitu ambacho alikuwa anakifanya kwa maslahi binafsi kujipatia wafuasi kwenye mitandao ya kijamii.
Leo, baada ya kuona umaarufu na ushawishi wake umeshuka mara dufu amekuja na hii ya kuzungumzia utekaji- jambo ambalo hana uhakika nalo ili kama kawaida yake ajipatie wafuasi wengi zaidi hasa kipindi hiki kuelekea kwenye uchaguzi mkuu ili akigombea tena ubunge aweze kuonekana ni mtu wa maana.
Waswahili walisema, Debe tupu haliachi kuvuma, ni hakika kwamba Gwajima amekosa ajenda za kumfanya akae kwenye vichwa vya wapiga kura ndiyo maana ameamua kuja sasa na hoja zisizokuwa na mashiko ilimradi kuonekana anatetea jambo fulani.
Ikumbukwe hata kwenye uchaguzi wa mwaka 2020 hakushinda kwenye kura za maoni ila Chama kwa kutaka kujumuisha makundi ya watu tofauti tofauti bungeni ndipo akapata nafasi ya uteuzi kugombea ili awakilishe kundi la viongozi wa dini. Mwaka huu amepima upepo ameona hali ni mbaya jimboni hakubaliki ndiyomaana anaanza kuja na habari za kukanganya umma kama hizi za utekaji na atakuja nazo nyingi huu ni mwanzo tu, na haya yote anayafanya kwa maslahi binafsi ili kujipatia wafuasi wengi ili akigombea aweze kupata kura!
Ikumbukwe mwaka 2019 ziliposambaa mtandaoni picha za ngono ambazo yeye mwenyewe baadae alijitokeza na kusema zimetengenezwa na maadui zake ili kumnyamazisha huku akisisitiza kuwa wamejaribu ila hawawezi kumnyamazisha alilenga kujipatia umaarufu kupitia mfululizo wa majuma kadhaa ambayo alikuwa alitoa hotuba za kujitangaza binafsi kama sehemu ya kujitetea ili ajipatie wafuasi wengi zaidi mitandaoni na kwenye jamii kwa ujumla.
Pia soma: Pre GE2025 - Askofu Gwajima: Wakuu wa Vyombo vya Usalama wasiondolewe kwenye nafasi zao kwa mapenzi ya mwanasiasa aliyewaweka
Mwaka 2020 wakati Serikali imetangaza upatikanaji wa chanjo ya CORONA, Gwajima alitumia fursa hiyo kutangaza misimamo ya kushangaza akihamasisha watu kuwa ‘HATUCHANJI’ kitu ambacho alikuwa anakifanya kwa maslahi binafsi kujipatia wafuasi kwenye mitandao ya kijamii.
Leo, baada ya kuona umaarufu na ushawishi wake umeshuka mara dufu amekuja na hii ya kuzungumzia utekaji- jambo ambalo hana uhakika nalo ili kama kawaida yake ajipatie wafuasi wengi zaidi hasa kipindi hiki kuelekea kwenye uchaguzi mkuu ili akigombea tena ubunge aweze kuonekana ni mtu wa maana.
Waswahili walisema, Debe tupu haliachi kuvuma, ni hakika kwamba Gwajima amekosa ajenda za kumfanya akae kwenye vichwa vya wapiga kura ndiyo maana ameamua kuja sasa na hoja zisizokuwa na mashiko ilimradi kuonekana anatetea jambo fulani.
Ikumbukwe hata kwenye uchaguzi wa mwaka 2020 hakushinda kwenye kura za maoni ila Chama kwa kutaka kujumuisha makundi ya watu tofauti tofauti bungeni ndipo akapata nafasi ya uteuzi kugombea ili awakilishe kundi la viongozi wa dini. Mwaka huu amepima upepo ameona hali ni mbaya jimboni hakubaliki ndiyomaana anaanza kuja na habari za kukanganya umma kama hizi za utekaji na atakuja nazo nyingi huu ni mwanzo tu, na haya yote anayafanya kwa maslahi binafsi ili kujipatia wafuasi wengi ili akigombea aweze kupata kura!