Gwajima, acha kumdhihaki Rais

My Son drink water

JF-Expert Member
Nov 30, 2016
4,932
13,283
Wewe Kama Mtumishi wa Mungu unajua formula zote za Mungu, na namna alivyo, ya kwamba Mungu si mwanadamu na hatendi kazi Kama Binadamu.

Sasa Unaweza kutoa ushahidi hapa kwamba umethibitisha vipi kwamba Magufuli ni chaguo la Mungu? Kwa sababu kumpatia mtu sifa asizostahili ni kumdhihaki.

Viongozi wengi hapa Duniani wamekuwa wakisifiwa kwamba wao ni chaguo la Mungu.
Bokassa aliyeitawala Africa ya Kati, viongozi wa Dini ktk Taifa hilo walikuwa wakimsifia kwamba ni chaguo la Mungu. Mobutu, na hata Idd Amin Dada, wote walisifiwa kwamba ni chaguo la Mungu.

Si kwamba nakataa kuwa Magufuli siyo chaguo la Mungu, bali nataka ushahidi. Kama ushahidi haupo basi hiyo ni dhihaka kwa Rais.

Napinga kwa hoja kwamba, siyo kila kiongozi ni chaguo la Mungu, Biblia inatafsiriwa Kama Kitabu cha Hadithi wakati kila kitu kipo dhahiri.
"Tiini kila mamlaka maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu”.

Mamlaka ni nini? mamlaka siyo Serikali kwa Tafsiri halisi, bali ni sheria ya haki itokayo kwa Mungu Kama amri kumi za Mungu ,amri kumi za Mungu ndo mamlaka. Luka 10:19 'mmepewa mamlaka (siyo serikali) ya kukanyaga nge na nyoka '.

Siyo kwamba mmepewa serikali ya kuganyaga nge na nyoka. Zipo Serikali nyingi hapa Duniani ambazo ni chukizo mbele za Mungu, Mungu siyo Binadamu, he doesn't contradict himself, aiweke serikali kisha serikali hiyo hiyo iliyowekwa na Mungu ipitishe sheria ya ndoa za jinsia moja, au aiweke Serikali inayotesa watu wake, wapigwe risasi kwa kuikosoa na wengine wapotezwe kwa kuikosoa, huyo siyo Mungu ,huyo ni shetani.

Kuna serikali za Mungu na serikali shetani hapa Duniani, utazijua kwa matendo yake. Shetani anaitesa Dunia akijua muda wake ni mchache kabla hajafungwa minyororo na Kutupwa kwenye ziwa na moto na wafuasi wake.
 
Muonee tu huruma. Tangu ajirekodi ile clip na baadae kusambaa mitandaoni, mikwara na upinzani wake wote dhidi ya bashite na baba yake uliishia pale.

Mwenzake Kakobe naye baada tu ya kusumbuliwa na TRA, na yeye akatulia kama maji ya mtungi. Awamu hii ukitaka uishi maisha ya amani basi unatakiwa kuunga mkono juhudi.
 
Acheni kumsingiza Mungu sema ni chaguo la tume
You may even say ''ni chaguo la shetani''. Rais anayeona wananchi wake wanakufa kwa makumi halafu anadanganya wamekufa 16 tu ni zaidi ya chaguo shetani. Huku mtaani tunazika wahnga wa korona kwa makumi kila siku halafu pamoja na raslimali yote aliyonayo hashtuki anadanganya ni 16 tu ni hatari sana. Hata huyo Mungu anayesema anamwamini na kumtaja kila siku atakuwa anapata chukizo kuu.
 
Muonee tu huruma. Tangu ajirekodi ile clip na baadae kusambaa mitandaoni, mikwara na upinzani wake wote dhidi ya bashite na baba yake uliishia pale.

Mwenzake Kakobe naye baada tu ya kusumbuliwa na TRA, na yeye akatulia kama maji ya mtungi. Awamu hii ukitaka uishi maisha ya amani basi unatakiwa kuunga mkono juhudi.

Ripoti yake ya TRA uliisoma lakini mkuu ndugu ?
Walikuta mzee wa watu yeye wala mkewe hawana akaunti yoyote ya fedha!!!

Tatizo letu wabongo tunapenda dezo, yaani mpaka haki zetu tunataka watu watusemee Kakobe ni Askofu, So akiongea kuhusu siasa sawa asipoongea pia ni sawa, huwezi kumlazimisha kama tusivyokulazimisha wewe mkuu
 
Wewe Kama Mtumishi wa Mungu unajua formula zote za Mungu, na namna alivyo, ya kwamba Mungu si mwanadamu na hatendi kazi Kama Binadamu.

Sasa Unaweza kutoa ushahidi hapa kwamba umethibitisha vipi kwamba Magufuli ni chaguo la Mungu? Kwa sababu kumpatia mtu sifa asizostahili ni kumdhihaki.

Viongozi wengi hapa Duniani wamekuwa wakisifiwa kwamba wao ni chaguo la Mungu.
Bokassa aliyeitawala Africa ya Kati, viongozi wa Dini ktk Taifa hilo walikuwa wakimsifia kwamba ni chaguo la Mungu. Mobutu, na hata Idd Amin Dada, wote walisifiwa kwamba ni chaguo la Mungu.

Si kwamba nakataa kuwa Magufuli siyo chaguo la Mungu, bali nataka ushahidi. Kama ushahidi haupo basi hiyo ni dhihaka kwa Rais.

Napinga kwa hoja kwamba, siyo kila kiongozi ni chaguo la Mungu, Biblia inatafsiriwa Kama Kitabu cha Hadithi wakati kila kitu kipo dhahiri.
"Tiini kila mamlaka maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu”.

Mamlaka ni nini? mamlaka siyo Serikali kwa Tafsiri halisi, bali ni sheria ya haki itokayo kwa Mungu Kama amri kumi za Mungu ,amri kumi za Mungu ndo mamlaka. Luka 10:19 'mmepewa mamlaka (siyo serikali) ya kukanyaga nge na nyoka '.

Siyo kwamba mmepewa serikali ya kuganyaga nge na nyoka. Zipo Serikali nyingi hapa Duniani ambazo ni chukizo mbele za Mungu, Mungu siyo Binadamu, he doesn't contradict himself, aiweke serikali kisha serikali hiyo hiyo iliyowekwa na Mungu ipitishe sheria ya ndoa za jinsia moja, au aiweke Serikali inayotesa watu wake, wapigwe risasi kwa kuikosoa na wengine wapotezwe kwa kuikosoa, huyo siyo Mungu ,huyo ni shetani.

Kuna serikali za Mungu na serikali shetani hapa Duniani, utazijua kwa matendo yake. Shetani anaitesa Dunia akijua muda wake ni mchache kabla hajafungwa minyororo na Kutupwa kwenye ziwa na moto na wafuasi wake.

Naunga Mkono Hoja yako mkuu!! Kusema mtu ni chaguo la Mungu ni kitu ambacho kwakweli kina ukakasi!!

KUHUSU BIBLIA HAPO
Labda niseme tu kuhusu ufafanuzi wa huo mstari
Sidhani kama kuna serikali hata moja duniani ambayo inafanya mambo matakatifu muda wote, ingawa zinaezekana zikawepo machaguo ya Mungu.
Kwa mfano katika maandiko Yuko mfalme Mpagani kabisa aliyeitwa Nebukadreza, ukisoma kitabu cha Daniel, huyu mfalme Muabudu sanamu.. kuna wakati Mungu alimtumia kwa ajili ya kuwapiga fimbo wanaisrael baada ya kumkosea Mungu, na kwa huo wakati Mungu alimuitwa Nebukadreza mtumishi wangu.
Kwahiyo mtu anaeza akawa ni mbaya, muovu lakini akawa chaguo la Mungu kulingana na kusudi ambalo Mungu anataka lifanyike wakati huo.

Kwahiyo Kuitwa Chaguo la Mungu, sidhani kama ni sifa nzuri moja kwa moja kwa mtu yeyote
Kwako Mkuu
 
Wewe Kama Mtumishi wa Mungu unajua formula zote za Mungu, na namna alivyo, ya kwamba Mungu si mwanadamu na hatendi kazi Kama Binadamu.

Sasa Unaweza kutoa ushahidi hapa kwamba umethibitisha vipi kwamba Magufuli ni chaguo la Mungu? Kwa sababu kumpatia mtu sifa asizostahili ni kumdhihaki.

Viongozi wengi hapa Duniani wamekuwa wakisifiwa kwamba wao ni chaguo la Mungu.
Bokassa aliyeitawala Africa ya Kati, viongozi wa Dini ktk Taifa hilo walikuwa wakimsifia kwamba ni chaguo la Mungu. Mobutu, na hata Idd Amin Dada, wote walisifiwa kwamba ni chaguo la Mungu.

Si kwamba nakataa kuwa Magufuli siyo chaguo la Mungu, bali nataka ushahidi. Kama ushahidi haupo basi hiyo ni dhihaka kwa Rais.

Napinga kwa hoja kwamba, siyo kila kiongozi ni chaguo la Mungu, Biblia inatafsiriwa Kama Kitabu cha Hadithi wakati kila kitu kipo dhahiri.
"Tiini kila mamlaka maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu”.

Mamlaka ni nini? mamlaka siyo Serikali kwa Tafsiri halisi, bali ni sheria ya haki itokayo kwa Mungu Kama amri kumi za Mungu ,amri kumi za Mungu ndo mamlaka. Luka 10:19 'mmepewa mamlaka (siyo serikali) ya kukanyaga nge na nyoka '.

Siyo kwamba mmepewa serikali ya kuganyaga nge na nyoka. Zipo Serikali nyingi hapa Duniani ambazo ni chukizo mbele za Mungu, Mungu siyo Binadamu, he doesn't contradict himself, aiweke serikali kisha serikali hiyo hiyo iliyowekwa na Mungu ipitishe sheria ya ndoa za jinsia moja, au aiweke Serikali inayotesa watu wake, wapigwe risasi kwa kuikosoa na wengine wapotezwe kwa kuikosoa, huyo siyo Mungu ,huyo ni shetani.

Kuna serikali za Mungu na serikali shetani hapa Duniani, utazijua kwa matendo yake. Shetani anaitesa Dunia akijua muda wake ni mchache kabla hajafungwa minyororo na Kutupwa kwenye ziwa na moto na wafuasi wake.
Huyo mtaalamu wa kifo cha mende ni BUMUNDA.
 
Gwajima hajakosea

Rais Magufuli ni chaguo la Mungu

Rais Magufuli ni Rais bora kwa sasa Africa and duniani
Mkuu umesoma kweli au umetafasiri kikao cha kikao cha viongozi wa dini na Makonda?
Hata hivyo tunaomba source mleta post
 
Ripoti yake ya TRA uliisoma lakini mkuu ndugu ?
Walikuta mzee wa watu yeye wala mkewe hawana akaunti yoyote ya fedha!!!

Tatizo letu wabongo tunapenda dezo, yaani mpaka haki zetu tunataka watu watusemee Kakobe ni Askofu, So akiongea kuhusu siasa sawa asipoongea pia ni sawa, huwezi kumlazimisha kama tusivyokulazimisha wewe mkuu

Unatambua lakini kabla na hata baada ya uchaguzi mkuu wa 2015 Askofu Kakobe alikuwa ni mkereketwa wa Chadema kama alivyokuwa mwenzake Gwajima?

Ila tangu aandamwe na serikali kwenye suala la kodi na suala la uraia wake (natambua hakuwa na hatia) aliamua kukubali matokeo kwa kuunga mkono juhudi za awamu ya tano ili kuondokana na misukosuko mbalimbali bila shaka! Mimi sihitaji kusemewa/kutetewa na hao viongozi wa dini maana ninaweza kujisemea/kujitetea mwenyewe.
 
Hakuna mungu anayekuchagua halafu anakuondolea akili kichwani na kukuachia mashonde.

Mungu wa hivyo hayupo.
Mungu alimchagua Ezekiel,sikumbuki vizuri,lakini Ezekiel aliambiwa ale mashonde,,,pia Ezekiel dish lilikuwa limeyumba kidogo
 
Back
Top Bottom