My Son drink water
JF-Expert Member
- Nov 30, 2016
- 4,932
- 13,283
Wewe Kama Mtumishi wa Mungu unajua formula zote za Mungu, na namna alivyo, ya kwamba Mungu si mwanadamu na hatendi kazi Kama Binadamu.
Sasa Unaweza kutoa ushahidi hapa kwamba umethibitisha vipi kwamba Magufuli ni chaguo la Mungu? Kwa sababu kumpatia mtu sifa asizostahili ni kumdhihaki.
Viongozi wengi hapa Duniani wamekuwa wakisifiwa kwamba wao ni chaguo la Mungu.
Bokassa aliyeitawala Africa ya Kati, viongozi wa Dini ktk Taifa hilo walikuwa wakimsifia kwamba ni chaguo la Mungu. Mobutu, na hata Idd Amin Dada, wote walisifiwa kwamba ni chaguo la Mungu.
Si kwamba nakataa kuwa Magufuli siyo chaguo la Mungu, bali nataka ushahidi. Kama ushahidi haupo basi hiyo ni dhihaka kwa Rais.
Napinga kwa hoja kwamba, siyo kila kiongozi ni chaguo la Mungu, Biblia inatafsiriwa Kama Kitabu cha Hadithi wakati kila kitu kipo dhahiri.
"Tiini kila mamlaka maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu”.
Mamlaka ni nini? mamlaka siyo Serikali kwa Tafsiri halisi, bali ni sheria ya haki itokayo kwa Mungu Kama amri kumi za Mungu ,amri kumi za Mungu ndo mamlaka. Luka 10:19 'mmepewa mamlaka (siyo serikali) ya kukanyaga nge na nyoka '.
Siyo kwamba mmepewa serikali ya kuganyaga nge na nyoka. Zipo Serikali nyingi hapa Duniani ambazo ni chukizo mbele za Mungu, Mungu siyo Binadamu, he doesn't contradict himself, aiweke serikali kisha serikali hiyo hiyo iliyowekwa na Mungu ipitishe sheria ya ndoa za jinsia moja, au aiweke Serikali inayotesa watu wake, wapigwe risasi kwa kuikosoa na wengine wapotezwe kwa kuikosoa, huyo siyo Mungu ,huyo ni shetani.
Kuna serikali za Mungu na serikali shetani hapa Duniani, utazijua kwa matendo yake. Shetani anaitesa Dunia akijua muda wake ni mchache kabla hajafungwa minyororo na Kutupwa kwenye ziwa na moto na wafuasi wake.
Sasa Unaweza kutoa ushahidi hapa kwamba umethibitisha vipi kwamba Magufuli ni chaguo la Mungu? Kwa sababu kumpatia mtu sifa asizostahili ni kumdhihaki.
Viongozi wengi hapa Duniani wamekuwa wakisifiwa kwamba wao ni chaguo la Mungu.
Bokassa aliyeitawala Africa ya Kati, viongozi wa Dini ktk Taifa hilo walikuwa wakimsifia kwamba ni chaguo la Mungu. Mobutu, na hata Idd Amin Dada, wote walisifiwa kwamba ni chaguo la Mungu.
Si kwamba nakataa kuwa Magufuli siyo chaguo la Mungu, bali nataka ushahidi. Kama ushahidi haupo basi hiyo ni dhihaka kwa Rais.
Napinga kwa hoja kwamba, siyo kila kiongozi ni chaguo la Mungu, Biblia inatafsiriwa Kama Kitabu cha Hadithi wakati kila kitu kipo dhahiri.
"Tiini kila mamlaka maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu”.
Mamlaka ni nini? mamlaka siyo Serikali kwa Tafsiri halisi, bali ni sheria ya haki itokayo kwa Mungu Kama amri kumi za Mungu ,amri kumi za Mungu ndo mamlaka. Luka 10:19 'mmepewa mamlaka (siyo serikali) ya kukanyaga nge na nyoka '.
Siyo kwamba mmepewa serikali ya kuganyaga nge na nyoka. Zipo Serikali nyingi hapa Duniani ambazo ni chukizo mbele za Mungu, Mungu siyo Binadamu, he doesn't contradict himself, aiweke serikali kisha serikali hiyo hiyo iliyowekwa na Mungu ipitishe sheria ya ndoa za jinsia moja, au aiweke Serikali inayotesa watu wake, wapigwe risasi kwa kuikosoa na wengine wapotezwe kwa kuikosoa, huyo siyo Mungu ,huyo ni shetani.
Kuna serikali za Mungu na serikali shetani hapa Duniani, utazijua kwa matendo yake. Shetani anaitesa Dunia akijua muda wake ni mchache kabla hajafungwa minyororo na Kutupwa kwenye ziwa na moto na wafuasi wake.