Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,897
- 6,933
Kijana aliyefanya maangamizi haya huyu hapa, ni mdogo sana.
Tatizo la Marekani umilikaji wa silaha za moto ni kama vijana wa vijijini wanavyoshindana kuwa na manati ya kuulia ndege. Maduka ya silaha yako kila sehemu kama maduka ya nguo vile na sehemu za uswahilini. Hakuna cha pingamizi la pekee la umilikaji silaha Marekani isipokuwa kama mtu amethibitishwa na daktari kuwa na matatizo ya kiakili. Mara kadhaa nilipokuwa naongea na polisi walinishauri niende nikanunue silaha ya kujilinda, lakini dhamiri yangu ilikataa kwani sihitaji kitu hicho na pengine huweza kunifanya nisiishi kwa amani na nikawa windo la wanaotafuta silaha za maangamizi ambao wana bad credit kupata kwa halali.
Movie nazo huchangia, maana watoto wanaangalia hizo na kufanyia mazoezi, na wawapo katika magenge yao ya kuvuta weed, ikikolea majadiliano huwa ni maangamizi. Wanaangalia movie za kijasusi na hapo hujifunza namna ya kufanya, na hapo uzoefu wa matumizi ya unga huwaharibu akili zao na siku unga ukikolea na kitu kidogo kikimwuzi basi mbinu alizoona kwenye movie za akina Swazilneger zitatumika na kuishia kujimaliza mwenyewe, hapo yanabaki maombolezo na kesi imefungwa kwa vile mwuaji amejihukumu kwa kujiruhusu kutangulia mbele ya Mwenye haki.
Taifa la marekani katika utafiti uliofanywa kama miaka 7 iliyopita ni kwamba robo ya wamarekani ni waathirika wa madawa ya kulevyo. Sijawahi kuziona dawa za kulevya kwa macho yangu Tanzania, lakini nilipotia mguu tu Marekani, hoteli niliyofikia nikashtuliwa na mmoja ambaye aliungana nami kwenye elevator ambaye aliniuliza kama nahitaji, nikamjibu nini? Akanionyesha kipakiti fulani kina unga mweupe, nikamwuliza nini? Kaniambia ni Cocaine. Kwa vile nilishafikia flower nilikokuwa naenda basi niliishia kuachana na maongezi yale kwani kwangu ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa. Kesho yake nikaamua kunza kutafuta nyumba baada ya kumweleza kisa hicho dean of studies. Akanishauri hama mara moja hapo si mahala panapokufaa na ni hatari. Nashukuru after a week nikapata nyumba sehemu iliyotulia hadi nilipoondoka kurudi zangu bongo.
Madawa ya kulevya Marekani huunzwa mitaani kama machinga bongo wafanyavyo kutembeza karanga vile. Bangi hata nashangaa wanaipata wapi. Kazini walifukuzwa vijana kadhaa kwa matumizi ya bangi wakiwa kazini.
Marekani siku hizi sharti la kwanza katika ajira ni kwenda hospitalini kwa wataalamu kupimwa uhakiki kama una matumizi ya madawa ya kulevya, vinginevyo ukipatikana hakuna ajira. Uzuri wa Marekani daktari anachukua vipimo na wenye kufanya uchunguzi ni kampuni nyingine ya maabara ambao hawamjui ni nani kwani wanapata maelfu ya order. Uchunguzi licha ya kupelekwa kwa mwajiri bila hungia kwenye record ya mhusika serikalini.