Mkwawe
JF-Expert Member
- Jun 10, 2016
- 3,210
- 5,680
Wakati mmoja nilikuwa na-scroll reels za Facebook ikatokea clip moja ikionesha watawa wa kikatoliki wakiimba Kwa ala za kuvutia sana (angelic voices). Hiyo clip ilikuwa ikimuonesha msanii wa kimarekani Kai Cenat akishangaa jinsi zile sauti zilivyokuwa zinavutia hata Mimi zikanishangaza sana, kupitia comments nikajua kumbe ule mtindo unaitwa Gregorian chant unaotumiwa na kanisa Katoliki katika Sala za tafakuri na maombi ya kina.
Nilipakua nyingi sana na chant ya kwanza kabisa ilikuwa inaitwa "Anima Christi" ya Marco Frisina ilikuwa fupi na niliipenda ilabidi nipakue extended yenye muda saa zima, Kila nilipokuwa nasikiliza nilikuwa najisikia utofauti wa Hali ya juu nikawa kama napokea kitu kipya ndani yangu. Na nyakati zote nikiwa najihisi kutotulia kiakili huwa nakaa katika utulivu Kwa angalau masaa mawili nikisikiliza Gregorian chant na wakati mwingi ninaambatanisha na kusali Rozari
Kwa atakayependa kutafakari na Gregorian chants atakuja kuleta mrejesho humu
Nilipakua nyingi sana na chant ya kwanza kabisa ilikuwa inaitwa "Anima Christi" ya Marco Frisina ilikuwa fupi na niliipenda ilabidi nipakue extended yenye muda saa zima, Kila nilipokuwa nasikiliza nilikuwa najisikia utofauti wa Hali ya juu nikawa kama napokea kitu kipya ndani yangu. Na nyakati zote nikiwa najihisi kutotulia kiakili huwa nakaa katika utulivu Kwa angalau masaa mawili nikisikiliza Gregorian chant na wakati mwingi ninaambatanisha na kusali Rozari
Kwa atakayependa kutafakari na Gregorian chants atakuja kuleta mrejesho humu