Katika mazingira mengi (most cases) wanadamu tumeumbwa kuitikia (respond) matukio mbali mbali kwa namna tofauti. Hata hivyo jambo hili linatofautiana kwa mwanadamu mmoja na mwingine.
Mfano ikitokea watu kadhaa wamepata taarifa za msiba. Kuna watakaochanganyikiwa na kuweza kupata au kupatwa na ajali kama watakuwa barabarani.
Au ikitokea mtu amepoteza ajira aliyokuwa akiitegemea sana kwa maisha yake kuna atakaye chukua hatua au maamuzi ambayo asingeyachukua kama asingepatwa na janga hilo.
Mara nyingi katika matukio kama haya au mengine tumekuwa tukishauriwa kutohamaki(panic) badala yake tumekuwa tukiambiwa “calm down”, “relax”, “ take it easy “ tukiaminishwa kuwa kwa kufanya hivyo tutaweza kuamua kwa busara na kuepuka ajali au matokeo hasi ya matendo yetu kutokana na kuhamaki(panic)
Swali linakuja.
Asanteni sana.
Mfano ikitokea watu kadhaa wamepata taarifa za msiba. Kuna watakaochanganyikiwa na kuweza kupata au kupatwa na ajali kama watakuwa barabarani.
Au ikitokea mtu amepoteza ajira aliyokuwa akiitegemea sana kwa maisha yake kuna atakaye chukua hatua au maamuzi ambayo asingeyachukua kama asingepatwa na janga hilo.
Mara nyingi katika matukio kama haya au mengine tumekuwa tukishauriwa kutohamaki(panic) badala yake tumekuwa tukiambiwa “calm down”, “relax”, “ take it easy “ tukiaminishwa kuwa kwa kufanya hivyo tutaweza kuamua kwa busara na kuepuka ajali au matokeo hasi ya matendo yetu kutokana na kuhamaki(panic)
Swali linakuja.
- Je, haiwezekani kuwa kwa kujaribu ku-calm down tutakuwa tunakinzana na maumbile halisi ya kiuumbaji(nature)?
- Nauliza hili nikiamini mwili wa mwanadamu ulivyoumbwa kuitikia vichocheo (stimuli) uko sahihi na hauwezi kukosea. Kwa kuthibitisha hili angalia irisi (iris) ya jicho inavyoitikia mwanga mkali au mwanga hafifu, kinywa kinapoitikia kwa kutoa mate pale unapolitazama limao au ukwaju kwa kuutamani.
- Sasa iweje mtu akihamaki(panic) tunajaribu kumtuliza?
- Je, kwa kufanya hivyo hatukosei?
Asanteni sana.