Gone too Soon inafaa utumike kwa marehemu aliye na rika gani?

Kasie

Platinum Member
Dec 29, 2013
21,247
36,300
Habari za mwisho wa mwezi mabibi na mabwana.

Kuna taarifa za msiba wa jamaa zimenifikia zikanipa tafakuri ya maisha. 🤔🤔🤔

Pindi tunapoondokewa na wapendwa wetu tunapatwa na huzuni sana. Tukitamani warudi tuendelee kuwa nao karibu hata kama tulikuwa hatuwasaidii au hawatusaidii kwenye maisha.

Wengi hutumia huu msemo pale wanapoondokewa na wapendwa wao.

Gone Too Soon.

Huu msemo yafaa/inafaa utumike kwa marehemu aliye na rika gani?

Namaanisha uishie kwa watoto hadi miaka 18 pale wanapofariki?

Uendelee hadi kwa vijana wa miaka 30 au anayefiwa na mzazi wa miaka 60 nae aseme mzazi wake ameenda mapema?

Ni yupi aliyeondokewa na mpendwa wake akasema gone at a right time? Au gone too late?

How does it sound, umefiwa na mke/mume wa miaka 70 halafu useme gone too late, we're suppose to go te years ago...😁😁😁

It's a joke right? No one says that in public but deep in people's hearts they say it and some we see through their actions.

Kimjazacho mtu, ndicho kimtokacho.

Well bado unabaki kuwa msemo wa lugha ya kimalkia sijajua kama una maana zaidi ya kulalamika mpendwa amewahi kuondoka kabla ya muda, ilifaa aendelee kuishi.

Kwa lugha mojawapo ya mkoa wetu pendwa wa Tanga, kwenye msiba huwa wanalia.

Kaita Mgima mgima. wakimaanisha kaondoka mzima mzima yaani na nguvu zake.

Kiafrika nimekuwa nikiaminishwa wazee ndo wanatakiwa wafe wazikwe na watoto wao na si wazazi kuzika watoto wao.

Inaumaaa, kuna bibi mmoja alizaa watoto 5 au 6 sikumbuki vizuri.

Hadi dakika hii tunapoongea amezika watoto wake wote na yeye amebaki mzee mwenye nguvu zake.

Ila huzuni aliyonayo moyoni mwake, anaijua yeye na Mungu wake.

Waswahili wanasema usithubutu kukutwa.

Pole kwa wote walioondokewa na wapendwa wao wiki hii na mwisho huu wa mwezi.

Alamsiki bin tafakuri za Bi Kasinde.
 
Nadhani hiyo kauli hutolewa ikimaanisha kuwa bado marehemu alikuwa anahitajika bila kujali umri wake.

Pole kwa wote walioondokewa na wapendwa wao. We all gonna die.
RAHA YA MILELE UWAPE Ee BWANA...... NA MWANGA WA MILELE UWAANGAZIE. WAPUMZIKE KWA AMANI. AMINA.
 
Nadhani hiyo kauli hutolewa ikimaanisha kuwa bado marehemu alikuwa anahitajika bila kujali umri wake.

Pole kwa wote walioondokewa na wapendwa wao. We all gonna die.
RAHA YA MILELE UWAPE Ee BWANA...... NA MWANGA WA MILELE UWAANGAZIE. WAPUMZIKE KWA AMANI. AMINA.

Okay, kwa mtizamo huo imeeleweka.
 
Nikajua kuna mtu kashachukua namba huko.

RIP yangu nilishaitoa mfukoni na kuishika mkononi tayari tayari, inabidi niirudishe mfukoni sasa.
 
Ni msemo kuonesha ya kwamba, mwendazake amefariki akiwa angali anahitajika kwa wapendwa zake na umri haukuwa umemtupa mkono kihivyo...

Hapo penye umri haukuwa umemtupa mkono.... pana utata....

Kuna babu wa miaka 82 alipofariki, wajukuu zake walikuwa wanalia babu, you've gone too soon....

Babu yao ndo alikuwa anawalea na kuwatunza. Alikuwa babu mwenye kiinua mgongo cha maana.

Yote kwa yote, hakuna anayetaka kuondokewa na mpendwa wake hata akiwa kikongwe wa miaka 200, labda awe jitu la kero na vurugu na ugomvi mara zote.
 
Nikajua kuna mtu kashachukua namba huko.

RIP yangu nilishaitoa mfukoni na kuishika mkononi tayari tayari, inabidi niirudishe mfukoni sasa.

Wee msukuma una vitukoo....😄😄😄

Yeah, kuna mtu amerudisha namba wiki hii, tena akiwa bado anahitajika na familia yake.

Imeumiza ila ni kujikaza tuu na kuendelea na maisha.

Sikuwa na lengo la kuleta msiba wake hapa, nilipata hii tafakuri wakati natafakari namna alivyorudisha namba.... ghafla mnoo.

Ulimholaa...!!??
 
Back
Top Bottom