Godoro la mtumba-19-
ILIPOISHIA IJUMAA WIKIENDA:
Mjomba hakujibu kitu, aliendelea kujiinamia. Ilikuwa aibu kubwa. Kifupi lilikuwa fumanizi la kufa mtu.
Mama alitulia kwa muda mrefu bila kusema chochote wala hata kukohoa kidogo. Kilichokuwa kikisikika ndani ya chumba ni kelele za watu nje tena wale waliokuwa wanaitana kwa mbali.
Nilijutia moyoni kitendo kimoja, ni kwa nini hatukufunga mlango kwa funguo wakati nimeingia chumbani kwa mjomba, pengine hilo lingeniokoa kama jana yake kwamba nilitoka nje kufungua maji.
RUKA NAYO SASA…
Mama alitembea hadi kwenye mlango, akasimama na kuuuegemea huku akituangalia kwa zamu. Uso wake uliongea mengi lakini kubwa kuliko yote ulionesha kwamba baada ya siku hiyo yeye na mjomba Msafiri hawatakuwa na uhusiano tena japokuwa wahenga walisema udugu ni taka la goti hivyo hauwezi kufutika.
Mimi nilizama kwenye mawazo makali. Nilianza kuwaza tangu siku ya kwanza mjomba aanze kunionesha dalili za kunitaka kimapenzi ilikuwa hivi…
"Anko tunaweza kuongea kidogo?"
"Sawa.""Wapi sasa?"
"Njoo huku." "Anko."
"Abee mjomba…"
"Unajua umekua sana."
"Kweli anko?"
"Kweli kabisa, yaani siku hizi unapendeza anko si kama zamani. Ukivaa nguo zako za kisasa hizi ndiyo kabisa, daa! Ankoooo."
"Zuwena," mama alinishtua kutoka kwenye mawazo.
"Abee…"
"Umekubali kufikia hatua hii mwanangu?"
Kabla sijamjibu mama mawazo yalinirejea kwenye lile swali nililomuuliza mjomba kuhusu godoro la kitanda chake…
"Hivi ni kwa nini niliuliza kuhusu godoro kama ni la mtumba au la dukani! Na kwa nini mjomba alinijibu vile? Eti la dukani mjomba, we si unaona lebo hii?"
"Mama ni shetani tu si kusudi langu."
Mama aliniangalia kwa jicho bay asana, akamgeukia mjomba…
"Msafiri."
"Naam dada."
"Mimi si dada yako tena na hata Zuwena si mpwa wako tena, mimi ni mama mkwe wako na Zuwena ni mkeo kuanzia leo."
"Dada usiseme hivyo."
"Lazima niseme, nisiposema nitakuwa mama wa ajabu sana, mtoto anachezewa naangalia hivihivi…
"Nikiwa nyumbani Tanga niliwahi kuota ndoto si chini ya mara saba kwamba nyinyi hapa nyumbani mna uhusiano wa kimapenzi. Usiku mmoja baada ya kuota nilimwambia Mungu kwamba kama ndoto ile ni ya kweli anioteshe tena mara tatu ili zifike kumi, akafanya hivyo.
"Niliamua kufunga safari kuja Dar ili kuthibitisha mwenyewe. Kwa hiyo kama mnadhani nilikuwa nawafuatilia si kwa sababu ya hisia, bali nina ushahidi…
"Jana usiku niliota ndoto mmelala kwenye kitanda kimoja hotelini lakini asubuhi wewe Msafiri ukanipigia simu ukisema eti mjomba wako alikamatwa na polisi akalala kituoni kwa sababu ya wizi wa pesa za abiria kwenye daladala, ina maana abiria wote kwenye hilo daladala walilala polisi?"
"Ndiyo dada."
"Siyo kweli bwana. Kama mtu amepoteza hela kwenye daladala si wakifika kituoni wanasachiwa? Kama hakuna abiria atakayepatikana na hiizo pesa ina maana huyo aliyeibuwa tukio lake halikufanyika ndani ya daladala," mama alisema kwa sauti iliyojaa utulivu wa hali ya juu.
Baada ya hapo kitendo alichokifanya mama kilinishtua sana, alifuungua mlango akatoka. Chumbani tukabaki mimi na mjomba tukiangaliana kwa macho yenye maswali mengi lakini pia kwa hofu na wasiwasi.
"So?" aliniuliza mjomba.
"Sijui."
"Hebu toka kamwangalie."
Nilisimama, nikatoka chumbani kwenda kumwangalia mama, sikumuona. Chumbani hakuwepo, wala begi lake halikuwepo, nilirudi chumbani kwa mjomba mbio…
"Baby baby, hayupo."
"Hayupo?"
"Hayupo baby, kweli tena."
"Atakuwa amekwenda wapi?"
"Sijui, hata begi lake halipo."
Tulitoka na mjomba hadi nej ambapo tulikuta begi liko wazi kuashiria kwamba alitoka.
Tulitoka hadi nje ya geti, tukasimama kuangalia kulia na kushoto, hatukumwona mama wala jirani yetu. Ghafla kwenye nyumba moja alitokea mwanamke anaitwa mama Maulidi…
"Vipi jirani?" alituuliza maana alituona tunaangazaangaza…
"Kuna mgeni wetu sijui katoka," alisema mjomba.
"Katoka, kapita kwenye uchochoro wangu tena alikuwa anatembea kwa haraka amebeba begi jeusi."
Utata uliishia hapo, ni mama. Bila shaka aliamua kurudi nyumbani Tanga.
Mama Maulidi aliposema ‘katoka, kapita kwenye uchochoro wangu tena alikuwa anatembea kwa haraka amebeba begi jeusi' mimi na mjomba tuliangaliana…
"Kwani vipi?" mama Maulidi alituuliza.
"Hata, tupo sawa jirani," alijibu mjomba.
Tulirudi ndani na kufikia sebuleni, kila mmoja alikaa kwenye kochi lake tena kwa ukimya. Naamini mawazo yangu mimi hayakuwa mawazo ya mjomba, kila mtu aliwaza lake.
Mara mjomba alivunja ukimya…
"Sikia baby, acha mimi nikimbie Ubungo, nikimkuta namrudisha tuje tujadili hili suala, tukiliacha atalieneza kwa ndugu mbalimbali itakuwa aibu yetu…
"Baby bwana…"
"Baby bwana nini tena, nisiende?"
"Usiende ndiyo. We huoni kama ile ahadi yako ya kunioa ndiyo imetimia?" nilimwambia mjomba, nikamwona anacheka kwa mara ya kwanza huku akisimama…
"Halafu wewe bwana, unajua ulinichekesha sana saa zile?"
"Nlifanyaje?"
"Ulipata wapi wazo la kuniuliza kama godoro la kitanda changu ni la mtumba ama la!"
Na mimi nilicheka, tena nilicheka sana kama vile hakuna kilichotokea katikati yetu…
"Unajua baby hata mimi mwenyewe nilijishangaa sana. Ila ni swali ambali nilitaka kukuuliza kwa siku nyingi sana kwamba mbona nikilala kwenye godoro lako nakuwa kama nimelala kwenye majani mabichi laini ya pembeni ya bahari, nahisi ni godoro la mtumba."
"Siyo la mtuumba lile ila lipo viwango," alisema mjomba huku akiondoka na funguo za gari…
"Usiondoke baby mpaka nirudi," aliniambia.
Niliongozana na mjomba mpaka kwenye geti, nikalifungua, akatoka na gari, nikafunga geti na kurudi ndani. Nilikwenda chumbani kwa mjomba, nikapanda kitandani kulala, lakini nikawaza kitu kwamba nimpigie simu mama nimuulize aliko. Lakini kabla ya kitendo hicho nikawaza kwamba anaweza akanijibu jambo baya sana, itakuwaje?
"Anaweza kuniambia Zuwena kuanzia leo wewe si mtoto wangu, tafuta mama yako mwingine. Je, sii itakuwa sawa na kuniachia laana?" nilijiuliza mwenyewe moyoni, lakini nikasema hata kama, lazima nimpigie tu nione kitakachotokea.
Nilibonyeza namba nikamtwangia simu mama, iliitaka kama mara nne halafu akapokea yeye mwenyewe, nikasema…
"Halo mama…"
Je, ni nini kiliendelea hapo? Usikose kwenye jumatano ijayo....