Halooooow ngoja nimuite
chige atuambie
Mkuu
Shark, thanx kwa kunikaribisha kwenye mjadala! Hii video nimejaribu kuifungua mara mbili, lakini window inakuwa blocked.
Hata hivyo, nikiangalia maoni ya watu naona wame-base kwenye story line! Na kwa sisi, ukisia story line tunamaanisha video iandane na maudhui ya wimbo kama unavyotafsiri movie script into images! Hata kama video nyingi zinakuwa na story line lakini sio LAZIMA... na hata ukiangalia video za mbele, no one care about story line! Music video is all about visual creative art! Sasa kama lyrics zinasema kwa mfano "baby unaniumiza, nakukimbiza najikwaa... nainuka nazidi kukukimbilia...!" halafu tena na wewe unatuletea video inatuonesha mtu anamkimbiza demu, anajikwaa, anainuka anaanza tena kumkimbiza...!" eti unataka kutafsiri maudhui ya wimbo... where's visual creative art hapo?
Anyway, nisiseme sana manake sijaiangalia lakini ngoja nigusie hoja ya
kadoda11. Audio ya ule wimbo nishaisikia lakini sioni kama inazungumzia house part ya kawaida ya Uswahilini; sana sana naona ni party iliyovamiwa na Waswazi! Chukulia verse ya kwanza kwa mfano, Dogo Aslee anazungumzia alivyo-struggle kufika kwenye party... manake ilibidi atembee kwa mguu! Mto wa Kiswazi hawezi kulalamika kutembea kutoka Temeke hadi Tandika au Buguruni hadi Kigogo... hii party watu waliifungia safari!!!! Kufika kwenye party, anakuta Wamasai na marungu... haya mambo ya Wamasai na marungu ni huko huko kwenu watoto wa kishua manake wanawalinda... huku kwetu wanakuwa na dawa za asili! Kuna mchizi kuingia kwenye party analazimika kuruka ukuta...! Huku kwetu na mambo ya ukuta wapi na wapi? Huku kwetu ukipata matofali, unaangalia kama kuna kinafasi kimebaki, kama kipo unaongeza kabanda hata kama ni kadogo unajua utapata mtu wa kuongeza hela ya mboga, na kama kanafasi hakuna kabisa, unayangiza sokoni! Party imejaa madaktari kibao... huku kwetu kabla hujaenda chuo unaulizwa "huo udaktari unasomea miaka mingapi" In short, tunaukwepa manake hatuwezi kukaa tena miaka 6 masomoni wakati ndugu wanatuangalia tuwasaidie; kwahiyo ukiona party ina madaktari wengi namna hiyo basi ni ya kwa akina
kadoda11 na mpwa
warumi... sijui kafia wapi huyu na yeye!
Sasa description ya huo wimbo hata kama party yenyewe itakuwa ni ya uswazi kama anavyosema Mkuu Kadoda, basi ni Uswazi kwenye familia bora! Si unajua watoto wa kishua pamoja na mbwembwe zao zote, baba zao wakistaafu wanakuwa hawana ubavu wa kujenga Masaki au Mbezi Beach na badala yake wanakuja huku huku mitaani kwetu... wanawahamisha wazazi wetu na kutuletea utamaduni wao wa kizungu!!!!