Mjumbe wa Kamati kuu Chadema Godbless Lema leo anatarajiwa kuhutubia mkutano wa hadhara katika viwanja vya Wajenzi mjini Dodoma saa 8 mchana leo.
Kamanda Lema ambaye pia ni mbunge wa Arusha mjini anatarajiwa kuelezea mambo kadhaa kuhusiana na wizi wa Tegeta Escrow,maazimio ya bunge na utekelezaji wake.
Mjumbe huyo wa kamati Kuu anatarajiwa pia kuwashukuru wananchi kwa kuiunga mkono Ukawa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.
Akihojiwa Lema amesema anakwenda kuzungumza mambo makubwa ya nchi na kuwataka wakazi wa Dodoma wakae tayari kusikia mambo ambayo huenda hawajayasikia.
Godbless Lema alikuwa amemtaka aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini Sospeter Muhongo kujiuzulu kabla ya kikao cha bunge kinachoanza kesho vinginevyo angemtoa kwa nguvu bungeni.
Lema anatarajiwa kufuatana na Mbunge wa Nyamagana Ezekiel Wenje na wabunge wengine kadhaa wakiwemo viongozi wa Kanda wa Chadema na mkoa wa Dodoma.
Kamanda Lema ambaye pia ni mbunge wa Arusha mjini anatarajiwa kuelezea mambo kadhaa kuhusiana na wizi wa Tegeta Escrow,maazimio ya bunge na utekelezaji wake.
Mjumbe huyo wa kamati Kuu anatarajiwa pia kuwashukuru wananchi kwa kuiunga mkono Ukawa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.
Akihojiwa Lema amesema anakwenda kuzungumza mambo makubwa ya nchi na kuwataka wakazi wa Dodoma wakae tayari kusikia mambo ambayo huenda hawajayasikia.
Godbless Lema alikuwa amemtaka aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini Sospeter Muhongo kujiuzulu kabla ya kikao cha bunge kinachoanza kesho vinginevyo angemtoa kwa nguvu bungeni.
Lema anatarajiwa kufuatana na Mbunge wa Nyamagana Ezekiel Wenje na wabunge wengine kadhaa wakiwemo viongozi wa Kanda wa Chadema na mkoa wa Dodoma.