God Father. Kitabu cha Kwanza

THE SPIRIT THINKER

JF-Expert Member
Sep 9, 2019
388
552
KITABU CHA KWANZA

Nyuma ya mafanikio yeyote kuna uhalifu.
- BALZAC




























Sura ya kwanza

Amerigo Bonasera alikuwa ameketi ndani ya jengo namba tatu la mahakama kuu ya kihalifu la New York akisubiri haki itendeke; alipiwe kisasi kwa wanaume ambao walikuwa wamemjeruhi binti yake kikakitili wakijaribu kumbaka.

Jaji, bwana mmoja mwenye mwili mkubwa, alikunja nguo yake kuipa hewa mikono huku akiwaangalia kwa umakini vijana wawili waliokuwa wamesimama mbele ya dawati lake. Uso wake ulikuwa mkavu ukionesha nuru ya madaraka aliyokuwa nayo. Lakini kulikuwa na kitu ndani ya muonekano huo ambacho Amigo Bonasera alihisi, ila hakuelewa kilikuwa ni nini.

“Mmeonesha tabia mbovu sana,” Jaji alisema kwa ukali.

Ndiyo, ndiyo, alijiwazia Bonasera. Wanyama. Wanyama.
Wale vijana waliinamishwa vichwa vyao chini kwa aibu.

“Mmeonesha tabia mbovu sana na bahati yenu hamkumbaka huyo binti. Vinginevyo ningewaweka nyuma ya nondo kwa miaka ishirini.” Jaji alitulia, macho yake yakahama kumtazama Amerigo Bonasera, halafu akayahamisha tena kutazama karatasi zilizokuwa juu ya dawati lake. Aliguna kabla ya kuongea tena.

“Lakini kwa sababu ya umri wenu, na kwakuwa hamna rekodi yeyote mbaya, kwa sababu ya familia yenu ambayo pia inaishi kwa kufuata sheria, na kwa sababu lengo la sheria sio kulipa kisasi, nitalifuta hili shauri.”

Ni kwa uzoefu wa mikasa ya hapa na pale kwa zaidi ya kipindi cha miaka kumi uliomfanya Amerigo Bonasera asioneshe chuki na hasira yake waziwazi. Binti yake mpendwa alikuwa bado yupo hospitalini huku taya zake zikiwa zimeshonwa baada ya kuvunjwa na hawa wanyama wawili; na bado sheria ilisema wataachiwa huru? Ilikuwa ni maumivu. Aliwatazama wazazi wa wale wanyama wawili wakiwakumbatia vijana wao. Familia yote ilikuwa na furaha na nyuso zao zilionesha tabasamu.

Mate machungu yalipanda hadi kooni kwa Bonasera. Akayazuia kwa meno yake yaliokuwa yameumana. Alisimama kipindi wale vijana wawili wanampita kutoka nje ya mahakama wakiwa wanajiamini, macho yao yakionesha ushindi. Aliwaacha wapite bila kusema neno lolote.

Wazazi wa wale wanyama walikuwa wanafuatia kwa nyuma, walikuwa na umri sawa na wa kwake. Walimtazama Bonasera kwa aibu, ila macho yao yalionesha wanashangilia ushindi walioupata.

Bonasera alishindwa kujizuia na kujikuta akiropoka, “Mtalia kama jinsi nilivyolia na kuomboleza – Nitahakikisha nawafanya mlie kama vijana wenu
walivyosababisha mimi nilie.”

Wakili wa utetezi alitokea kwa nyuma na kuwasukuma wateja wake waondoke. Kundi la askari lilitokea kumkinga Amerigo Bonasera. Hata hivyo haikuwa inahitajika kufanyika hivyo.

Katika miaka yake yote aliyoishi Marekani, Amerigo Bonasera aliamini kwenye sheria na ustaarabu. Na alikuwa amefanikiwa katika hilo. Lakini sasa hivi, akili yake ilikuwa imejaa chuki na hasira. Ingawa akili na mifupa ya fuvu lake ilikuwa imejawa na mawazo mabaya ya kwenda kununua bunduki na kuwaua wale vijana wawili, Bonasera alimgeukia mke wake na kumfafanulia, “Wametufanya wajinga.” Alitulia halafu akapata maamuzi ya mwisho, bila kuogopa gharama na hasara za uamuzi wake. “Ili haki itendeke ni lazima tukampigie magoti Don Corleone.”

Kwenye hoteli moja iliyopambwa kwa samani za gharama, Jonny Fontane alikuwa amelewa kwa wivu kama mume wa mwanamke yeyote. Akiwa kajilaza kwenye sofa jekundu, alikunywa pombe kali na kuikata ladha yake kwa kufakamia maji ya baridi. Ilikuwa ni saa kumi alfajiri na alikuwa na mawazo kedekede juu ya kumuua mke wake pindi atakapofika nyumbani. Hiyo ni kaama angerudi nyumbani usiku huu. Ilikuwa ni muda mbaya wa kuanza kumpigia simu mke wake wa kwanza ambaye walikuwa wameachana na kuanza kumuuliza kuhusu watoto au kuanza kuwapigia simu marafiki zake kuwaeleza anayopitia. Kuna kipindi wangefurahishwa na Jonny kuwapigia simu muda kama huo , lakini kwa sasa alikuwa ni kero kwao.

Akiwa anaendelea kuushusha mvinyo wake, alisikia mke wake akifungua mlango, lakini aliendelea kunywa hadi mke wake alipofika sebuleni na kusimama kando yake. Alikuwa ni mwanamke mzuri, mwenye uso wa malaika, macho yenye mvuto wa ajabu na mwenye mwili wenye kila mvuto kwa mwanamume yeyote. Kwenye runinga uzuri wake ulikuwa ni maradufu ya hapo. Mamilioni ya wanaume ulimwenguni walikuwa wanavutiwa na Margot Ashton. Na walikuwa tayari kulipa fedha nyingi ili tu wautazame uso wake kwenye sinema.

“Ulikuwa wapi?” Johnny Fontane aliuliza

“Nilikuwa nafanya mapenzi,” Alijibu Margot.

Alikuwa anadhani Johnny kalewa. Ila alishangaa kumuona Johnny ananyuka kwa kasi na kumkaba shingo. Lakini ile sura ya malaika na macho yenye mvuto, Johnny Fontane alisalimu hasira zake na kuwa mnyonge tena. Margot alifanya kosa jingine, alitabasamu kwa namna ya kumkebehi Johnny ambaye aliinua mkono wake kumpiga ngumi.

“Usinipige usoni, Johhny. Kuna filamu tunaanza kushuti hivi karibuni.”

Margot alikuwa anacheka. Johnny alikuwa anampiga ngumi za tumboni hadi akaanguka chini. Johnny alimrukia kwa juu. Aliendelea kumpiga ngumi kwenye mapaja na miguuni. Ilikuwa ni adhabu kali. Laiti kama angelikuwa anampiga vile usoni, basi angemharibu sura au kumtoa meno kabisa.

Hata hivyo hakuwa akimpiga kwa nguvu sana.
Asingeweza kufanya hivyo. Na Margot alilifahamu hilo.

Johnny Fontane aliinuka juu. Alikuwa anamchukia yule mwanamke pale chini, lakini uzuri wake ulikuwa ni kama kinga fulani ya maajabu. Margot pia aliinuka kutoka sakafuni. Alianza kuchezacheza huku akiimba, “Johnny usiwahi kuniumiza, Johnny usiwahi kuniumiza.” Halafu ghafla akasema, “Mjinga mkubwa, unanipiga kama mtoto mdogo. Kwanza haujui mapenzi na ukiwa kitandani unakuwa kama mtoto. Unadhani mapenzi ni kama hizo nyimbo zako ulizokuwa unaimba zamani?”

Halafu Margot akakimbilia chumbani na kujifungia.

Johnny aliketi sakafuni. Dharau aliyooneshwa ilimkera. Lakini ugumu na ujasiri uliomfanya akaishi kwenye ulimwengu wa Hollywood ulimfanya anyanyue simu ya mezani na kuomba gari kwaajili ya kumpeleka uwanja wa ndege. Kulikuwa na mtu mmoja tu ambaye angeweza kumsaidia. Angerudi zake New York. Angeenda hadi kwa mtu huyo mwenye busara na upendo. Baba yake wa kufikia Don Corleone.

Wote hawa na wengine wengi walikuwa wamepokea mwaliko kwenye harusi ya Miss Constanzia Corleone ambayo ingefanyika jumapili ya mwisho ya mwezi wa nane 1945. Baba wa bibi harusi, Don Vito Corleone, hakuwahi kuwasahau marafiki na jirani zake ingawa kwa sasa alikuwa anaishi kwenye jumba lake kubwa la kifahari. Mapokezi ya wageni wote yangefanyika ndani ya jumba hilo halafu sherehe zingeendelea siku nzima. Hakuna ubishi hili lingekuwa ni tukio la kipekee. Vita kati ya Marekani na Wajapani ilikuwa imeisha kwahivyo kusingekuwa na usumbufu wowote. Asingetokea mtu yeyote wa serikalini kuomba watoto wa kiume wa Don Corleone kwenda kusaidia taifa kupambana kwenye vita hiyo. Hata hivyo, harusi ndiyo sehemu pekee ambayo watu wangeitumia kuonesha furaha yao.

Kwahivyo Jumamosi asubuhi rafiki za Don Corleone walifurika kutoka New York kuonesha heshima. Wengi walikuwa wamebeba bahasha zilizowekewa pesa kama zawadi za maharusi, hakukuwa na cheki za benki. Ndani ya bahasha kulikuwa na kikaratasi kilichoonesha jina la mtu aliyeileta zawadi kuonesha kuwa alimheshimu Godfather. Heshima ambayo ama kwa hakika ilitafutwa kwa muda mrefu.

Don Corleone alikuwa ni mtu ambaye kila mwenye shida alikuja kwake kuomba msaada, na hakuwahi kuwaangusha watu wake. Hakuwahi kutoa ahadi za uongo, au sababu za kujitetea kwamba mikono yake ilikuwa imewekewa mipaka na watu wenye nguvu zaidi duniani kuliko yeye. Ilikuwa sio lazima awe rafiki yako, au eti uwe na uwezo wa kumlipa ndiyo akusaidie! Kitu kimoja tu ndicho kilikuwa kinatakiwa. Kwamba, wewe mwenyewe, ukiri urafiki wako kwake. Halafu haijalishi hali yako ya kiuchumi, Don Corleone angelichukua tatizo lako kama tatizo lake kwa moyo mmoja. Na asingeruhusu kitu chochote kisimame njiani kuzuia utatuzi wa tatizo la mtu yeyote. Malipo yake? Urafiki, heshima ya jina la “Don”, na wakati mwingine furaha ya kuitwa “Godfather.” Au kumuonesha heshima tu. Hakuwa akilenga faida yeyote. Zawadi ndogondogo kama asali au mkate vilitosha sana. Hata hivyo, ilieleweka kuwa ni tabia njema kujiona upo kwenye deni naye na kwamba alikuwa na haki ya kukuita wakati wowote na kukuomba ulilipe deni lake kwa msaada wa huduma ndogondogo.

Sasa leo hii, kwenye harusi ya binti yake, Don Vito Corleone alikuwa amesimama kwenye mlango wa jumba lake kubwa la kifahari kuwasalimia wageni wake wote waliokuwa wanafika hapo. Wengi wakiwa ni wale anaowafahamu na kuwaamini. Maisha mazuri waliyokuwa wakiishi yote ilikuwa ni kwa sababu ya Don na hawakuona aibu kumuita Godfather mbele ya uso wake. Hata watu ambao walikuwa wanashughulikia maandalizi ya harusi walikuwa ni rafiki zake. Aliyekuwa anasimamia vinywaji alikuwa ni bwana mmoja ambaye zawadi yake kwenye harusi hii ni vinywaji vyote vitakavyotumika. Wahudumu wengine walikuwa ni marafiki za watoto wa kiume wa Don Corleone. Chakula kilichokuwa kwenye meza mbalimbali kilikuwa kimepikwa na mke wa Don akishirikiana na marafiki zake na ukumbi ulikuwa umepambwa na rafiki wa binti yake Don Corleon ambaye alikuwa anaolewa leo.

Don Corleone alikuwa ni rafiki wa kila mtu. Aliwapokea maskini na matajiri, watu wenye ushawishi na nguvu na hata wale wanyonge – na aliwaonesha upendo sawasawa. Hakumbagua yeyote. Hiyo ndiyo ilikuwa hulka yake. Na wageni walimsifia sana kwa suti aliyokuwa amevaa. Ilimkaa vizuri sana kiasi kwamba kwa mtu ambaye hakuwa anamfahamu angehisi yeye, Don Corleone, ndiye bwana harusi mwenyewe.

Mlangoni alikuwa amesimama na vijana wake wawili kati ya watatu. Mkubwa kabisa, alibatizwa kwa jina la Santino ila wengi walimwita Sonny isipokuwa Don mwenyewe. Sonny Corleone alikuwa mrefu wa futi sita, na nyewele zake zilimfanya aonekane mrefu zaidi. Uso wake ulikuwa mpana na mashavu yake yalikuwa na mashimo. Alikuwa na nguvu kama za ng’ombe dume na ilikuwa inafahamika alikuwa na maumbile makubwa kiasi kwamba mke wake alikiogopa kitanda cha ndoa kama wanaoamini katika dini wanavyoogopa moto wa jehanamu. Inasemekana alipokuwa mdogo alikuwa amepita kwenye madanguro mengi, hata wanawake ambao walikuwa makonkodi kwenye biashara ya kujiuza walipoona maumbile yake waliomba awaongezee pesa ya malipo.

Leo, hapa kwenye harusi, baadhi ya wasichana waliofika walikuwa wanampima Sonny kwa macho ya wiziwizi huku wakimtega. Lakini kwa siku ya leo walikuwa wanapoteza muda wao tu. Licha ya uwepo wa mke wake na watoto wake watatu, Sonny Corleone, alikuwa na mipango na msindikizaji wa dada yake kwenye harusi, Lucy Mancini. Lucy, akiwa anafahamu kila kitu alikuwa amekaa bustanini. Alikuwa amejaribu kumchombezachombeza Sonny kwa takribani wiki nzima iliyopita na alikuwa amefanikiwa kumshika Sonny maungoni.

Hakujali kwamba, Don Corleone, hakuwa akimuona Sonny kama mtoto wake bora. Sonny Corleone alikuwa na nguvu, alikuwa ni jasiri. Alikuwa na utu na moyo wake ulikuwa mkubwa kama yalivyokuwa maumbile yake. Lakini hakuwa na uvumilivu kama wa baba yake. Yeye alikuwa ni mwepesi wa hasira ambazo mara nyingi zilimpelekea kufanya makosa kwenye maamuzi yake. Ingawa alikuwa na msaada mkubwa kwenye biashara za baba yake, bado wengi hawakumuona kama angekuja kurithi uendeshaji wa biashara ya baba yake siku akifariki.

Kijana wa pili alikuwa ni Fredrico, wengi walimwita Fred au Fredo. Alikuwa ni aina ya mtoto ambaye wazazi wengi wa kiitalia walifunga na kumuomba Mungu awapatie mtoto kama huyo. Alikuwa mwaminifu, na alikuwa yupo tayari kufanya lolote kwaajili ya baba yake na hata akiwa na umri wa miaka thelathini bado alikuwa akiishi na wazazi wake. Alikuwa ni mfupi, hakuwa na uzuri wowote ila sura yake ilionesha alikuwa ni mmoja wa wanafamilia wa Don Corleone. Hakuwahi kumkera baba yake au kumuudhi, lakini licha ya yote hakuwa na ule muonekano au viashiria vya kiongozi, hivyo yeye pia hakutazamiwa kama atamrithi Don Corleone.

Mtoto wa tatu, Michael Corleone, hakuwa amesimama na ndugu zake au baba yake. Alikuwa amejitenga upande wa bustani kwenye kona ya mwisho kabisa. Lakini hata akiwa huko bado macho ya wageni yaliweza kumfikia.
Michael Corleone alikuwa ni mtoto wa mwisho wa Don na mtoto pekee ambaye alikataa kuishi kwa maelekezo ya baba yake. Sura yake haikutofautiana sana na ya ndugu zake. Ngozi yake ilikuwa na rangi ambayo kama ingelikuwa kwa msichana basi msichana huyo ataitwa mrembo. Ama kwa hakika Michael alikuwa ni handsome. Kuna kipindi baba yake alihofia kuhusu ushababi wa mtoto wake huyo. Hofu ambayo ilifutwa siku ambayo Michael Corleone alifikisha miaka kumi na saba.

Sasa hivi huyu mtoto alikuwa amekaa peke yake kuonesha alikuwa amejitenga na baba yake na familia yake. Pembeni yake alikuwa amekaa binti wa kimarekani ambaye kila mtu alikuwa amesikia habari zake na leo ndiyo walikuwa wanamuona kwa mara ya kwanza. Michael alikuwa ametumia heshima na kumtambulisha msichana wake huyo kwa kila mtu, ikiwemo familia yake. Na kusemwa kweli hawakuvutiwa naye. Alikuwa ni mwembamba sana, wa kawaida, uso wake ulipaswa kuwa kwa mtu mwenye jinsia ya kiume. Jina lake pia lilikuwa la ajabu masikioni mwao; Alikuwa anajiita Kay Adams. Laiti kama angewaambia kwamba jina lake ni la kawaida tu kwenye tamaduni ya Marekani wangeguna.!

Kila mtu aligundua pia Don hakuwa anamzingatia sana kijana wake huyu wa tatu. Kabla ya vita Michael alikuwa ndiye kijana pendwa wa Don Corleoe na alimchagua awe mrithi wa biashara zote za familia wakati sahihi utakapofika. Michael alikuwa na sifa za utulivu na akili kama ya baba yake, na alikuwa amezaliwa tu na uwezo wa kuwafanya watu wafanye vitu kwa amri yake. Lakini vita vya pili vya dunia vilipoanza, Michael Corleone alijitolea kupigana na jeshi la majini.
Aliipinga amri ya baba yake kwa kufanya hivyo.

Don Corleone hakuwa na lengo, au nia, ya kumwacha kijana wake mdogo akauawe kwenye uwanja wa vita kuitetea nchi ya kigeni. Madaktari walihongwa, na vikao vya siri vilifanyika. Kiwango kikubwa cha pesa kilitumika kuhakikisha haingii vitani. Lakini Michael alikuwa na miaka ishirini na moja na hakuna kitu kingeweza kufanyika kubadilisha maamuzi yake.
Alijiandikisha na kupigania ukanda wa bahari ya Pasifiki. Akawa Kapteni na kushinda medali nyingi.
Mwaka 1944 picha yake ilichapishwa kwenye gazeti la Life Magazine na maandishi ya kazi alizozifanya. Rafiki mmoja wa Don Corleone alimuonesha gazeti hilo Don, na Don aliguna kwa huzuni na kusema, “Anayafanya hayo
yote kwa watu baki tu anaisahau familia yake.”

Michael alipotolewa jeshini mwaka 1945 ili kuuguza majeraha yake, hakuwa anafahamu baba yake ndiyo alikuwa ameandaa mipango yote hadi atolewe jeshini. Alikaa nyumbani kwa wiki chache tu, halafu, bila kuzungumza na yeyote, akajiunga na chuo cha Dartmouth College kilichopo Hanover. Kwa hivyo akawa ameondoka nyumbani kwao. Muda ulikuwa umepita hadi leo aliporejea nyumbani tena kwaajili ya harusi ya dada yake na kuwatambulisha mchumba wake huyu ambaye hakuwavutia.

Michael Corleone alikuwa anamuonesha Kay Adams ucheshi kwa kumwambia hadithi za hapa na pale kuhusu wageni waliokuwa wamefika harusini hapo. Hata hivyo mawazo ya Kay Adams yalikuwa kwa kile kikundi kidogo cha watu waliojetenga kwenye meza yao
wakinywa mvinyo. Watu hao walikuwa ni Amerigo Bonasera, Nazorine, Anthony Coppola na Luca Brasi. Kwa mawazo yake, Kay Adams aligundua watu hawa hawakuwa na furaha.
Michael alitabasamu, “Hawana furaha ndiyo,” Michael alisema. “Hapo walipo wanasubiri wakutane na
baba. Lazima kuna kitu wanataka awasaidie.”

Na hilo lilionekana kwenye macho ya wanaume wale, kila mara macho yao yalikuwa kwa Don Corleone.

Don Corleone alikuwa bado amesimama akiwasalimia wageni wake wa hapa na pale, Chevrolet nyeusi iliingia na kuegeshwa upande wa pili. Wanaume wawili waliokuwa ndani ya gari hilo walichomoa vijitabu na kuanza kuandika namba za sahani za magari yaliokuwa yameegeshwa pale. Sonny alimgeukia baba
yake. “Wale jamaa, lazima ni asakri.”

Don Corleone alijibu, “Siumiliki mtaa mimi, kwahivyo wanaweza kufanya wanachojisikia.”

Uso wa Sonny ulibadilika kuwa mwekundu kwa hasira. “ Wale wajinga hawana heshima kabisa.”

Alizishuka ngazi za nyumba na kwenda hadi ile gari ilipokuwa imeegeshwa. Akauweka uso wake karibu na wa yule dereva, ambaye hakutetemeka. Baadala yake aliingiza mkono mfukoni na kutoa kadi ya utambulisho.
Sonny akapiga hatua kuondoka bila kusema kitu. Akatema mate chini yakaruka kwenye kioo na kuondoka. Alifanya hivyo kwa maksudi ili yule dereva ashuke kumfuata kwenye nyumba, lakini yule dereva hakufanya hivyo.

Alipofika aliposimama baba yake alisema, “Wale jamaa ni FBI. Nimeona wanaandika namba zote za magari yaliyopo hapa. Wajinga wakubwa.”
Don Corleone alikuwa anawafahamu ni akina nani. Hivyo marafiki zake wa karibu sana alikuwa amewashauri waje nyumbani hapo kwa kutumia magari ambayo sio ya kwao. Na ingawa hakupenda alichokifanya Sonny, lakini aliona tukio lile lilikuwa na faida.
Ingewashawishi wale jamaa kuwa ujio wao ulikuwa ni wa kushtukiza na hawakuwa wakitegemewa. Kwahivyo Don hakuwa amekasirika. Alikuwa amejifunza zamani za kale kwamba, Jamii huwa inatoa dharau ambazo ni za kupuuza, na kwamba kwenye huu ulimwengu huwa kuna nyakati ambapo mtu mnyonge zaidi, kama akiyafumbua macho yake, anao uwezo wa kumshinda mtu yeyote mwenye nguvu na ushawishi. Ni jambo hili lililomfanya Don Corleone asipoteze heshima kutoka kwa marafiki zake.
 
KITABU CHA KWANZA

Nyuma ya mafanikio yeyote kuna uhalifu.
- BALZAC




























Sura ya kwanza

Amerigo Bonasera alikuwa ameketi ndani ya jengo namba tatu la mahakama kuu ya kihalifu la New York akisubiri haki itendeke; alipiwe kisasi kwa wanaume ambao walikuwa wamemjeruhi binti yake kikakitili wakijaribu kumbaka.

Jaji, bwana mmoja mwenye mwili mkubwa, alikunja nguo yake kuipa hewa mikono huku akiwaangalia kwa umakini vijana wawili waliokuwa wamesimama mbele ya dawati lake. Uso wake ulikuwa mkavu ukionesha nuru ya madaraka aliyokuwa nayo. Lakini kulikuwa na kitu ndani ya muonekano huo ambacho Amigo Bonasera alihisi, ila hakuelewa kilikuwa ni nini.

“Mmeonesha tabia mbovu sana,” Jaji alisema kwa ukali.

Ndiyo, ndiyo, alijiwazia Bonasera. Wanyama. Wanyama.
Wale vijana waliinamishwa vichwa vyao chini kwa aibu.

“Mmeonesha tabia mbovu sana na bahati yenu hamkumbaka huyo binti. Vinginevyo ningewaweka nyuma ya nondo kwa miaka ishirini.” Jaji alitulia, macho yake yakahama kumtazama Amerigo Bonasera, halafu akayahamisha tena kutazama karatasi zilizokuwa juu ya dawati lake. Aliguna kabla ya kuongea tena.

“Lakini kwa sababu ya umri wenu, na kwakuwa hamna rekodi yeyote mbaya, kwa sababu ya familia yenu ambayo pia inaishi kwa kufuata sheria, na kwa sababu lengo la sheria sio kulipa kisasi, nitalifuta hili shauri.”

Ni kwa uzoefu wa mikasa ya hapa na pale kwa zaidi ya kipindi cha miaka kumi uliomfanya Amerigo Bonasera asioneshe chuki na hasira yake waziwazi. Binti yake mpendwa alikuwa bado yupo hospitalini huku taya zake zikiwa zimeshonwa baada ya kuvunjwa na hawa wanyama wawili; na bado sheria ilisema wataachiwa huru? Ilikuwa ni maumivu. Aliwatazama wazazi wa wale wanyama wawili wakiwakumbatia vijana wao. Familia yote ilikuwa na furaha na nyuso zao zilionesha tabasamu.

Mate machungu yalipanda hadi kooni kwa Bonasera. Akayazuia kwa meno yake yaliokuwa yameumana. Alisimama kipindi wale vijana wawili wanampita kutoka nje ya mahakama wakiwa wanajiamini, macho yao yakionesha ushindi. Aliwaacha wapite bila kusema neno lolote.

Wazazi wa wale wanyama walikuwa wanafuatia kwa nyuma, walikuwa na umri sawa na wa kwake. Walimtazama Bonasera kwa aibu, ila macho yao yalionesha wanashangilia ushindi walioupata.

Bonasera alishindwa kujizuia na kujikuta akiropoka, “Mtalia kama jinsi nilivyolia na kuomboleza – Nitahakikisha nawafanya mlie kama vijana wenu
walivyosababisha mimi nilie.”

Wakili wa utetezi alitokea kwa nyuma na kuwasukuma wateja wake waondoke. Kundi la askari lilitokea kumkinga Amerigo Bonasera. Hata hivyo haikuwa inahitajika kufanyika hivyo.

Katika miaka yake yote aliyoishi Marekani, Amerigo Bonasera aliamini kwenye sheria na ustaarabu. Na alikuwa amefanikiwa katika hilo. Lakini sasa hivi, akili yake ilikuwa imejaa chuki na hasira. Ingawa akili na mifupa ya fuvu lake ilikuwa imejawa na mawazo mabaya ya kwenda kununua bunduki na kuwaua wale vijana wawili, Bonasera alimgeukia mke wake na kumfafanulia, “Wametufanya wajinga.” Alitulia halafu akapata maamuzi ya mwisho, bila kuogopa gharama na hasara za uamuzi wake. “Ili haki itendeke ni lazima tukampigie magoti Don Corleone.”

Kwenye hoteli moja iliyopambwa kwa samani za gharama, Jonny Fontane alikuwa amelewa kwa wivu kama mume wa mwanamke yeyote. Akiwa kajilaza kwenye sofa jekundu, alikunywa pombe kali na kuikata ladha yake kwa kufakamia maji ya baridi. Ilikuwa ni saa kumi alfajiri na alikuwa na mawazo kedekede juu ya kumuua mke wake pindi atakapofika nyumbani. Hiyo ni kaama angerudi nyumbani usiku huu. Ilikuwa ni muda mbaya wa kuanza kumpigia simu mke wake wa kwanza ambaye walikuwa wameachana na kuanza kumuuliza kuhusu watoto au kuanza kuwapigia simu marafiki zake kuwaeleza anayopitia. Kuna kipindi wangefurahishwa na Jonny kuwapigia simu muda kama huo , lakini kwa sasa alikuwa ni kero kwao.

Akiwa anaendelea kuushusha mvinyo wake, alisikia mke wake akifungua mlango, lakini aliendelea kunywa hadi mke wake alipofika sebuleni na kusimama kando yake. Alikuwa ni mwanamke mzuri, mwenye uso wa malaika, macho yenye mvuto wa ajabu na mwenye mwili wenye kila mvuto kwa mwanamume yeyote. Kwenye runinga uzuri wake ulikuwa ni maradufu ya hapo. Mamilioni ya wanaume ulimwenguni walikuwa wanavutiwa na Margot Ashton. Na walikuwa tayari kulipa fedha nyingi ili tu wautazame uso wake kwenye sinema.

“Ulikuwa wapi?” Johnny Fontane aliuliza

“Nilikuwa nafanya mapenzi,” Alijibu Margot.

Alikuwa anadhani Johnny kalewa. Ila alishangaa kumuona Johnny ananyuka kwa kasi na kumkaba shingo. Lakini ile sura ya malaika na macho yenye mvuto, Johnny Fontane alisalimu hasira zake na kuwa mnyonge tena. Margot alifanya kosa jingine, alitabasamu kwa namna ya kumkebehi Johnny ambaye aliinua mkono wake kumpiga ngumi.

“Usinipige usoni, Johhny. Kuna filamu tunaanza kushuti hivi karibuni.”

Margot alikuwa anacheka. Johnny alikuwa anampiga ngumi za tumboni hadi akaanguka chini. Johnny alimrukia kwa juu. Aliendelea kumpiga ngumi kwenye mapaja na miguuni. Ilikuwa ni adhabu kali. Laiti kama angelikuwa anampiga vile usoni, basi angemharibu sura au kumtoa meno kabisa.

Hata hivyo hakuwa akimpiga kwa nguvu sana.
Asingeweza kufanya hivyo. Na Margot alilifahamu hilo.

Johnny Fontane aliinuka juu. Alikuwa anamchukia yule mwanamke pale chini, lakini uzuri wake ulikuwa ni kama kinga fulani ya maajabu. Margot pia aliinuka kutoka sakafuni. Alianza kuchezacheza huku akiimba, “Johnny usiwahi kuniumiza, Johnny usiwahi kuniumiza.” Halafu ghafla akasema, “Mjinga mkubwa, unanipiga kama mtoto mdogo. Kwanza haujui mapenzi na ukiwa kitandani unakuwa kama mtoto. Unadhani mapenzi ni kama hizo nyimbo zako ulizokuwa unaimba zamani?”

Halafu Margot akakimbilia chumbani na kujifungia.

Johnny aliketi sakafuni. Dharau aliyooneshwa ilimkera. Lakini ugumu na ujasiri uliomfanya akaishi kwenye ulimwengu wa Hollywood ulimfanya anyanyue simu ya mezani na kuomba gari kwaajili ya kumpeleka uwanja wa ndege. Kulikuwa na mtu mmoja tu ambaye angeweza kumsaidia. Angerudi zake New York. Angeenda hadi kwa mtu huyo mwenye busara na upendo. Baba yake wa kufikia Don Corleone.

Wote hawa na wengine wengi walikuwa wamepokea mwaliko kwenye harusi ya Miss Constanzia Corleone ambayo ingefanyika jumapili ya mwisho ya mwezi wa nane 1945. Baba wa bibi harusi, Don Vito Corleone, hakuwahi kuwasahau marafiki na jirani zake ingawa kwa sasa alikuwa anaishi kwenye jumba lake kubwa la kifahari. Mapokezi ya wageni wote yangefanyika ndani ya jumba hilo halafu sherehe zingeendelea siku nzima. Hakuna ubishi hili lingekuwa ni tukio la kipekee. Vita kati ya Marekani na Wajapani ilikuwa imeisha kwahivyo kusingekuwa na usumbufu wowote. Asingetokea mtu yeyote wa serikalini kuomba watoto wa kiume wa Don Corleone kwenda kusaidia taifa kupambana kwenye vita hiyo. Hata hivyo, harusi ndiyo sehemu pekee ambayo watu wangeitumia kuonesha furaha yao.

Kwahivyo Jumamosi asubuhi rafiki za Don Corleone walifurika kutoka New York kuonesha heshima. Wengi walikuwa wamebeba bahasha zilizowekewa pesa kama zawadi za maharusi, hakukuwa na cheki za benki. Ndani ya bahasha kulikuwa na kikaratasi kilichoonesha jina la mtu aliyeileta zawadi kuonesha kuwa alimheshimu Godfather. Heshima ambayo ama kwa hakika ilitafutwa kwa muda mrefu.

Don Corleone alikuwa ni mtu ambaye kila mwenye shida alikuja kwake kuomba msaada, na hakuwahi kuwaangusha watu wake. Hakuwahi kutoa ahadi za uongo, au sababu za kujitetea kwamba mikono yake ilikuwa imewekewa mipaka na watu wenye nguvu zaidi duniani kuliko yeye. Ilikuwa sio lazima awe rafiki yako, au eti uwe na uwezo wa kumlipa ndiyo akusaidie! Kitu kimoja tu ndicho kilikuwa kinatakiwa. Kwamba, wewe mwenyewe, ukiri urafiki wako kwake. Halafu haijalishi hali yako ya kiuchumi, Don Corleone angelichukua tatizo lako kama tatizo lake kwa moyo mmoja. Na asingeruhusu kitu chochote kisimame njiani kuzuia utatuzi wa tatizo la mtu yeyote. Malipo yake? Urafiki, heshima ya jina la “Don”, na wakati mwingine furaha ya kuitwa “Godfather.” Au kumuonesha heshima tu. Hakuwa akilenga faida yeyote. Zawadi ndogondogo kama asali au mkate vilitosha sana. Hata hivyo, ilieleweka kuwa ni tabia njema kujiona upo kwenye deni naye na kwamba alikuwa na haki ya kukuita wakati wowote na kukuomba ulilipe deni lake kwa msaada wa huduma ndogondogo.

Sasa leo hii, kwenye harusi ya binti yake, Don Vito Corleone alikuwa amesimama kwenye mlango wa jumba lake kubwa la kifahari kuwasalimia wageni wake wote waliokuwa wanafika hapo. Wengi wakiwa ni wale anaowafahamu na kuwaamini. Maisha mazuri waliyokuwa wakiishi yote ilikuwa ni kwa sababu ya Don na hawakuona aibu kumuita Godfather mbele ya uso wake. Hata watu ambao walikuwa wanashughulikia maandalizi ya harusi walikuwa ni rafiki zake. Aliyekuwa anasimamia vinywaji alikuwa ni bwana mmoja ambaye zawadi yake kwenye harusi hii ni vinywaji vyote vitakavyotumika. Wahudumu wengine walikuwa ni marafiki za watoto wa kiume wa Don Corleone. Chakula kilichokuwa kwenye meza mbalimbali kilikuwa kimepikwa na mke wa Don akishirikiana na marafiki zake na ukumbi ulikuwa umepambwa na rafiki wa binti yake Don Corleon ambaye alikuwa anaolewa leo.

Don Corleone alikuwa ni rafiki wa kila mtu. Aliwapokea maskini na matajiri, watu wenye ushawishi na nguvu na hata wale wanyonge – na aliwaonesha upendo sawasawa. Hakumbagua yeyote. Hiyo ndiyo ilikuwa hulka yake. Na wageni walimsifia sana kwa suti aliyokuwa amevaa. Ilimkaa vizuri sana kiasi kwamba kwa mtu ambaye hakuwa anamfahamu angehisi yeye, Don Corleone, ndiye bwana harusi mwenyewe.

Mlangoni alikuwa amesimama na vijana wake wawili kati ya watatu. Mkubwa kabisa, alibatizwa kwa jina la Santino ila wengi walimwita Sonny isipokuwa Don mwenyewe. Sonny Corleone alikuwa mrefu wa futi sita, na nyewele zake zilimfanya aonekane mrefu zaidi. Uso wake ulikuwa mpana na mashavu yake yalikuwa na mashimo. Alikuwa na nguvu kama za ng’ombe dume na ilikuwa inafahamika alikuwa na maumbile makubwa kiasi kwamba mke wake alikiogopa kitanda cha ndoa kama wanaoamini katika dini wanavyoogopa moto wa jehanamu. Inasemekana alipokuwa mdogo alikuwa amepita kwenye madanguro mengi, hata wanawake ambao walikuwa makonkodi kwenye biashara ya kujiuza walipoona maumbile yake waliomba awaongezee pesa ya malipo.

Leo, hapa kwenye harusi, baadhi ya wasichana waliofika walikuwa wanampima Sonny kwa macho ya wiziwizi huku wakimtega. Lakini kwa siku ya leo walikuwa wanapoteza muda wao tu. Licha ya uwepo wa mke wake na watoto wake watatu, Sonny Corleone, alikuwa na mipango na msindikizaji wa dada yake kwenye harusi, Lucy Mancini. Lucy, akiwa anafahamu kila kitu alikuwa amekaa bustanini. Alikuwa amejaribu kumchombezachombeza Sonny kwa takribani wiki nzima iliyopita na alikuwa amefanikiwa kumshika Sonny maungoni.

Hakujali kwamba, Don Corleone, hakuwa akimuona Sonny kama mtoto wake bora. Sonny Corleone alikuwa na nguvu, alikuwa ni jasiri. Alikuwa na utu na moyo wake ulikuwa mkubwa kama yalivyokuwa maumbile yake. Lakini hakuwa na uvumilivu kama wa baba yake. Yeye alikuwa ni mwepesi wa hasira ambazo mara nyingi zilimpelekea kufanya makosa kwenye maamuzi yake. Ingawa alikuwa na msaada mkubwa kwenye biashara za baba yake, bado wengi hawakumuona kama angekuja kurithi uendeshaji wa biashara ya baba yake siku akifariki.

Kijana wa pili alikuwa ni Fredrico, wengi walimwita Fred au Fredo. Alikuwa ni aina ya mtoto ambaye wazazi wengi wa kiitalia walifunga na kumuomba Mungu awapatie mtoto kama huyo. Alikuwa mwaminifu, na alikuwa yupo tayari kufanya lolote kwaajili ya baba yake na hata akiwa na umri wa miaka thelathini bado alikuwa akiishi na wazazi wake. Alikuwa ni mfupi, hakuwa na uzuri wowote ila sura yake ilionesha alikuwa ni mmoja wa wanafamilia wa Don Corleone. Hakuwahi kumkera baba yake au kumuudhi, lakini licha ya yote hakuwa na ule muonekano au viashiria vya kiongozi, hivyo yeye pia hakutazamiwa kama atamrithi Don Corleone.

Mtoto wa tatu, Michael Corleone, hakuwa amesimama na ndugu zake au baba yake. Alikuwa amejitenga upande wa bustani kwenye kona ya mwisho kabisa. Lakini hata akiwa huko bado macho ya wageni yaliweza kumfikia.
Michael Corleone alikuwa ni mtoto wa mwisho wa Don na mtoto pekee ambaye alikataa kuishi kwa maelekezo ya baba yake. Sura yake haikutofautiana sana na ya ndugu zake. Ngozi yake ilikuwa na rangi ambayo kama ingelikuwa kwa msichana basi msichana huyo ataitwa mrembo. Ama kwa hakika Michael alikuwa ni handsome. Kuna kipindi baba yake alihofia kuhusu ushababi wa mtoto wake huyo. Hofu ambayo ilifutwa siku ambayo Michael Corleone alifikisha miaka kumi na saba.

Sasa hivi huyu mtoto alikuwa amekaa peke yake kuonesha alikuwa amejitenga na baba yake na familia yake. Pembeni yake alikuwa amekaa binti wa kimarekani ambaye kila mtu alikuwa amesikia habari zake na leo ndiyo walikuwa wanamuona kwa mara ya kwanza. Michael alikuwa ametumia heshima na kumtambulisha msichana wake huyo kwa kila mtu, ikiwemo familia yake. Na kusemwa kweli hawakuvutiwa naye. Alikuwa ni mwembamba sana, wa kawaida, uso wake ulipaswa kuwa kwa mtu mwenye jinsia ya kiume. Jina lake pia lilikuwa la ajabu masikioni mwao; Alikuwa anajiita Kay Adams. Laiti kama angewaambia kwamba jina lake ni la kawaida tu kwenye tamaduni ya Marekani wangeguna.!

Kila mtu aligundua pia Don hakuwa anamzingatia sana kijana wake huyu wa tatu. Kabla ya vita Michael alikuwa ndiye kijana pendwa wa Don Corleoe na alimchagua awe mrithi wa biashara zote za familia wakati sahihi utakapofika. Michael alikuwa na sifa za utulivu na akili kama ya baba yake, na alikuwa amezaliwa tu na uwezo wa kuwafanya watu wafanye vitu kwa amri yake. Lakini vita vya pili vya dunia vilipoanza, Michael Corleone alijitolea kupigana na jeshi la majini.
Aliipinga amri ya baba yake kwa kufanya hivyo.

Don Corleone hakuwa na lengo, au nia, ya kumwacha kijana wake mdogo akauawe kwenye uwanja wa vita kuitetea nchi ya kigeni. Madaktari walihongwa, na vikao vya siri vilifanyika. Kiwango kikubwa cha pesa kilitumika kuhakikisha haingii vitani. Lakini Michael alikuwa na miaka ishirini na moja na hakuna kitu kingeweza kufanyika kubadilisha maamuzi yake.
Alijiandikisha na kupigania ukanda wa bahari ya Pasifiki. Akawa Kapteni na kushinda medali nyingi.
Mwaka 1944 picha yake ilichapishwa kwenye gazeti la Life Magazine na maandishi ya kazi alizozifanya. Rafiki mmoja wa Don Corleone alimuonesha gazeti hilo Don, na Don aliguna kwa huzuni na kusema, “Anayafanya hayo
yote kwa watu baki tu anaisahau familia yake.”

Michael alipotolewa jeshini mwaka 1945 ili kuuguza majeraha yake, hakuwa anafahamu baba yake ndiyo alikuwa ameandaa mipango yote hadi atolewe jeshini. Alikaa nyumbani kwa wiki chache tu, halafu, bila kuzungumza na yeyote, akajiunga na chuo cha Dartmouth College kilichopo Hanover. Kwa hivyo akawa ameondoka nyumbani kwao. Muda ulikuwa umepita hadi leo aliporejea nyumbani tena kwaajili ya harusi ya dada yake na kuwatambulisha mchumba wake huyu ambaye hakuwavutia.

Michael Corleone alikuwa anamuonesha Kay Adams ucheshi kwa kumwambia hadithi za hapa na pale kuhusu wageni waliokuwa wamefika harusini hapo. Hata hivyo mawazo ya Kay Adams yalikuwa kwa kile kikundi kidogo cha watu waliojetenga kwenye meza yao
wakinywa mvinyo. Watu hao walikuwa ni Amerigo Bonasera, Nazorine, Anthony Coppola na Luca Brasi. Kwa mawazo yake, Kay Adams aligundua watu hawa hawakuwa na furaha.
Michael alitabasamu, “Hawana furaha ndiyo,” Michael alisema. “Hapo walipo wanasubiri wakutane na
baba. Lazima kuna kitu wanataka awasaidie.”

Na hilo lilionekana kwenye macho ya wanaume wale, kila mara macho yao yalikuwa kwa Don Corleone.

Don Corleone alikuwa bado amesimama akiwasalimia wageni wake wa hapa na pale, Chevrolet nyeusi iliingia na kuegeshwa upande wa pili. Wanaume wawili waliokuwa ndani ya gari hilo walichomoa vijitabu na kuanza kuandika namba za sahani za magari yaliokuwa yameegeshwa pale. Sonny alimgeukia baba
yake. “Wale jamaa, lazima ni asakri.”

Don Corleone alijibu, “Siumiliki mtaa mimi, kwahivyo wanaweza kufanya wanachojisikia.”

Uso wa Sonny ulibadilika kuwa mwekundu kwa hasira. “ Wale wajinga hawana heshima kabisa.”

Alizishuka ngazi za nyumba na kwenda hadi ile gari ilipokuwa imeegeshwa. Akauweka uso wake karibu na wa yule dereva, ambaye hakutetemeka. Baadala yake aliingiza mkono mfukoni na kutoa kadi ya utambulisho.
Sonny akapiga hatua kuondoka bila kusema kitu. Akatema mate chini yakaruka kwenye kioo na kuondoka. Alifanya hivyo kwa maksudi ili yule dereva ashuke kumfuata kwenye nyumba, lakini yule dereva hakufanya hivyo.

Alipofika aliposimama baba yake alisema, “Wale jamaa ni FBI. Nimeona wanaandika namba zote za magari yaliyopo hapa. Wajinga wakubwa.”
Don Corleone alikuwa anawafahamu ni akina nani. Hivyo marafiki zake wa karibu sana alikuwa amewashauri waje nyumbani hapo kwa kutumia magari ambayo sio ya kwao. Na ingawa hakupenda alichokifanya Sonny, lakini aliona tukio lile lilikuwa na faida.
Ingewashawishi wale jamaa kuwa ujio wao ulikuwa ni wa kushtukiza na hawakuwa wakitegemewa. Kwahivyo Don hakuwa amekasirika. Alikuwa amejifunza zamani za kale kwamba, Jamii huwa inatoa dharau ambazo ni za kupuuza, na kwamba kwenye huu ulimwengu huwa kuna nyakati ambapo mtu mnyonge zaidi, kama akiyafumbua macho yake, anao uwezo wa kumshinda mtu yeyote mwenye nguvu na ushawishi. Ni jambo hili lililomfanya Don Corleone asipoteze heshima kutoka kwa marafiki zake.
🔥🔥🔥🔥
 
Sonny akapiga hatua kuondoka bila kusema kitu. Akatema mate chini yakaruka kwenye kioo na kuondoka. Alifanya hivyo kwa maksudi ili yule dereva ashuke kumfuata kwenye nyumba, lakini yule dereva hakufanya hivyo.

Alipofika aliposimama baba yake alisema, “Wale jamaa ni FBI. Nimeona wanaandika namba zote za magari yaliyopo hapa. Wajinga wakubwa.”
Don Corleone alikuwa anawafahamu ni akina nani. Hivyo marafiki zake wa karibu sana alikuwa amewashauri waje nyumbani hapo kwa kutumia magari ambayo sio ya kwao. Na ingawa hakupenda alichokifanya Sonny, lakini aliona tukio lile lilikuwa na faida.
Ingewashawishi wale jamaa kuwa ujio wao ulikuwa ni wa kushtukiza na hawakuwa wakitegemewa. Kwahivyo Don hakuwa amekasirika. Alikuwa amejifunza zamani za kale kwamba, Jamii huwa inatoa dharau ambazo ni za kupuuza, na kwamba kwenye huu ulimwengu huwa kuna nyakati ambapo mtu mnyonge zaidi, kama akiyafumbua macho yake, anao uwezo wa kumshinda mtu yeyote mwenye nguvu na ushawishi. Ni jambo hili lililomfanya Don Corleone asipoteze heshima kutoka kwa marafiki zake.

Bendi ya muziki ilianza kuburudisha watu. Wageni wote waliokuwa wamealikwa walikuwa wamefika. Don Corleone aliwapotezea waliokuwa wamevamia sherehe na kuwaongoza vijana wake wawili kuelekea kwenye sherehe.
Kulikuwa na mamia ya wageni, baadhi wakicheza muziki laini wa bendi, wengine walikuwa wamekaa kwenye meza zao zilizopambwa vyakula vya kuvutia na glasi zenye vinywaji. Bibi harusi, Connie Corleone, alikuwa amekaa mbele ya ukumbi kwenye meza iliyopambwa akiwa na bwana harusi, msindikizaji wa bibi harusi na wapambe wengine wawili. Ilikuwa ni aina ya harusi ya familia ya Italia. Haikuwa ni chaguo la bwana harusi, lakini Connie alikubali harusi yake ifanyike hivi kwa sababu alitaka kumfurahisha baba yake alipogundua baba yake hakuwa ameridhika na uchaguzi wake wa mume wa kumuoa.
Bwana harusi, Carlo Rizzi, alikuwa ni chotara. Baba yake alikuwa ni mtu wa Italia na mama yake alikuwa ni Mmarekani. Wazazi wake walikuwa wanaishi Nevada ila Carlo alitoroka huko kwa sababu za makosa madogomadogo ya kisheria. Alipofika New York akakutana na Sonny Corleone na ndiyo ikasababisha uhusiano na dada yake. Don Corleone, bila shaka, aliwatuma marafiki zake aliowaamini kwenda Nevada kuchunguza kuhusu maisha ya Carlo. Walirudi na majibu kuwa Carlo alikuwa amevunja sheria ya kumili silaha bila kibali. Lilikuwa ni kosa dogo ambalo linawezwa likafutwa kwenye rekodi za polisi. Walirudi pia na taarifa za kutosha kuhusu michezo ya kamari inavyofaidisha upande wa Nevada na Don Corleone aliwekeza huko. Ilikuwa ni tabia yake kuhakikisha anapata faida katika kila anachokifanya.
Connie Corleone mwenyewe hakuwa mzuri wa kuvutia, alikuwa ni mwembamba kuliko kawaida. Lakini leo, akiwa ndani ya shera lake ukijumlisha na bikra yake alionekana mrembo kuliko kawaida. Chini ya meza, alikuwa ameuweka mkono wake juu ya mapaja ya bwana harusi wake. Akaegemea kidogo na kumbusu mashavuni bwana wake huyo.
Alimuona kama mwanamume mwenye mvuto sana. Carlo Rizzi alikuwa ameishi maisha yake ya hali ya chini akifanya kazi ngumu. Mwili wake ulikuwa umejazia kama wa wabeba nondo. Aliyatazama macho ya Conny Corleone na kujaza kinywaji kwenye glasi ya Conny Corleone. Carlo Rizzi alionesha heshima ya hali ya juu. Lakini muda wote jicho lake lilikuwa kwenye pochi aliyokuwa ameshikilia Connie ambayo kwa sasa ilikuwa imejaa bahasha zenye pesa kibao. Ilikuwa na shilingi ngapi? Dola elfu kumi? Elfu ishirini? Carlo Rizzi alitabasamu. Huo ulikuwa ni mwanzo tu. Hata hivyo, alikuwa ameoa kwenye familia ya kifahari. Lazima wangehakikisha wanamtunza na kumjali.

Kwenye umati wa watu waliofika shereheni, kuna kijana mwingine pia alikuwa anautolea macho ya tama ule mkoba. Kutokana na uzoefu wa muda mrefu, Paulie Gatto alikuwa amemshtukia huyo kijana na akawa anajiuliza huyo kijana atawezaje kuuchukua ule mkoba. Hata hivyo, alijua wazo la kijana huyo lilikuwa ni kama ndoto za mchana za mtoto mdogo awazavyo kupindua gari lililobeba pipi. Pauli Gatto alihamisha macho yake kumtazama bosi wake, mnene, umri wa kati – Peter Clemenza aliyekuwa anacheza na wasichana wadogowadogo ukumbini. Clemenza alikuwa mrefu na mwenye mwili mkubwa, lakini alikuwa anaonesha ufundi wake wa kucheza jukwaani. Wageni wote waliofika harusini hapo walikuwa wanamshangilia yeye. Clemenza alipochoka na kurejea kuketi kitini, Paulie Gatto alimletea glasi ya wine nyeusi na kumfuta jasho.
Clemenza alikuwa anathema kwa nguvu kama mbwa aliyekimbia mwendo mrefu huku akinywa kwa kasi kinywaji alicholetewa; Lakini baadala ya kumshukuru Paulie Clemenza alisema kwa ukali, “Usianze kuniambia kuhusu nilivyocheza, fanya kazi yako, zungukia eneo lote uhakikishe kila kitu kipo sawa.”

Paulie aliondoka bila kujibu kitu chochote.

Bendi ya muziki nayo ilichukua mapumziko. Kijana mmoja aitwaye Nino Valenti alichukua mandolin na kuanza kuipiga huku akiimba wimbo mmoja wa mahaba kwa lugha ya Italia. Uso wa Nino Valenti ulikuwa ni uso wa kuvutia ingawa ulikuwa umeharibiwa kwa tabia yake ya unywaji pombe na hata alipokuwa anaimba alikuwa tayari kalewa. Aliyazungusha macho yake ukumbini huku ulimi wake ukiendelea kuchuja mashairi ya wimbo aliokuwa anaimba. Wanawake waliimba naye pamoja na wanaume walikuwa wanamalizia kila neon la mwisho aliloimba.

Don Corleone, yeye mwenyewe hakuwa akifanya hivyo, hata hivyo mke wake alikuwa anashangilia kama wageni wengine wote. Don Corleone aliondoka taratibu na kimyakimya na kuingia kwenye ofisi yake ya nyumbani hapo. Kwa kuona hivi, Sonny Corleone alitembea hadi ilipo meza ya bibi harusi na kukaa pembeni kidogo ya Lucy Mancini, msindikizaji wa bibi harusi. Walikuwa wapo salama. Mke wa Sonny alikuwa yupo jikoni akifanya maandalizi ya mwisho ya keki ya sherehe nzima. Sonny alinong‟ona maneno kadhaa kwa sauti ya chini kwenye masikio ya Lucy na Lucy akainuka na kuondoka. Sonny alisubiri kwa dakika kadhaa nay eye akasimama kumfuata kwa nyuma, huku akisimama kuongea na mgeni huyu na yule huku akiendelea kumfuata Lucy kwa nyuma ili watu wasishtukie.
Macho yote yalikuwa yanawatazama wao. Msindikizaji wa bibi harusi mwenyewe akiwa ameathiriwa na umarekani kwa miaka mitatu aliyokaa chuoni alikuwa na „sifa‟ tayari. Muda wote wa maandalizi ya harusi alikuwa amemchombeza sana Sonny Corleone kwa namna ya utani ambayo yeye alihisi ni sawa kwa wasindikizaji wa maharusi kutaniana. Sasa akiwa amelishikilia gauni lake Lucy Mancini aliingia ndani ya nyumba, tabasamu usoni lililoonesha hatia, alitembea hadi kuelekea zilipokuwa bafu. Alikaa huko kwa muda kidogo. Alipotoka, Sonny Corleone alikuwa amesimama ghorofa ya juu akimuelekeza kwa ishara amfuate.

Nyuma ya dirisha la ofisi ya Don Corleone lililokuwa limefungwa , Thomas Hagen alikuwa anachungulia kila kilichokuwa kinaendelea kwenye sherehe hiyo. Ndani ya chumba kulikuwa kumejaa vitabu vya sheria. Hagen alikuwa ni wakili wa Don na mshauri wa mwisho, na kwahivyo alikuwa anashikilia nafasi muhimu sana kwenye biashara ya familia. Yeye akishirikiana na Don walikuwa wamefumbua vitendawili vigumu ndani ya chumba hikihiki, na kwahivyo Don atakapoingia huku, Hagen alikuwa anajua, kuwe na harusi au hakuna harusi, kulikuwa na kazi kidogo leo. Na Don alikuwa anakuja kumuona muda sio mrefu. Halafu akamuona Sonny akimnong‟oneza kitu Lucy na akaona komedi yao walioifanya wakiongozana kwenda ndani. Hagen aliguna, akajiuliza kama amtaarifu Don au aache, na aliamua kuacha. Alirudi hadi lilipo dawati lake akachukua kikaratasi na kuanza kupitia orodha ya majina ya watu waliokuwa wanatakiwa kuonana na Don Corleone. Na Don Corleone alipoingia humo ndani, Hagen alimpatia ile orodha. Don Corleone alitikisa kichwa. “Bonasera awe wa mwisho kabisa.”

Hagen alifungua mlango na kutoka nje bustanini kwenye meza ya wale wageni waliokuwa wamejitenga. Akamwita jamaa mmoja aliyejulikana kama Nazorine.
Don Corleone alimsalimia Nazorine alipoingia ndani. Walikuwa wamecheza pamoja udogoni huko Italia na wakawa wakubwa urafiki wao bila kufa.

Don Corleone alimpatia Nazorine sigara na kumshika bega. Hiyo ilikuwa ni ishara ya urafiki wa Don. Alikuwa anafahamu, kutokana na uzoefu wa muda mrefu, ilikuwa inahitaji ujasiri kiasi gani kwa
mwanamume kumwomba mwanamume mwenzake msaada.

Nazorine alielezea kisa cha binti yake na Enzo. Enzo alikamatwa kama mtumwa wa vita na jeshi la Marekani, akaletwa Marekani, na kuitumikia nchi ya Marekani. Lakini kwa kipindi hiki aliangukia kwenye penzi la binti wa Nazorine na vita ilikuwa imeisha muda wowote Enzo angetakiwa kurudishwa kwao Italia. Na ni Don Corleone tu ambaye angeweza kusaidia penzi la hawa vijana wawili. Yeye ndiye alikuwa tumaini lao la mwisho.

Don Corleone alianza kumtembeza Nazorine kutoka kona moja ya chumba hadi kona nyingine, huku akitikisa kichwa cheke kukubali na kumpa ujasiri Nazorine. Na alipomaliza kueleze, Don Corleone alitabasamu na kusema, “Rafiki yangu kipenzi, weka wasiwasi wako pembeni.” Akaendelea kuelezea kila hatua inayotakiwa kuchukuliwa. Kwamba ni lazima Congressmen apendekeze sheria itakayomruhusu Enzo awe mwananchi halali. Na ni lazima pendekezo hilo likubaliwe. Don Corleone alisema pia jambo hili lingegharimu kiasi kikubwa cha pesa, labda dola elfu mbili za kimarekani. Na kwamba, yeye Don Corleone alikuwa tayari kukubali na kulipa hicho kiasi cha pesa, je rafiki yake huyo alikuwa anaona ni sawa?

Nazorine alitikisa kichwa kukubali. Hakuwa anategemea kufanyiwa msaada mkubwa kama huo bila kulipa jambo lolote. Hilo lilikuwa linaeleweka. Pendekezo kama hilo huwa halitoki kwa bei ndogo! Don Corleone alimsindikiza rafiki yake hadi mlangoni huku akimhakikishia kuwa watu watatumwa kuja ofisini kwake kuandaa kila kinachohitajika. Nazorine alimkumbatia Don Corleone kabla ya kutoka nje.

Don Corleoe akamgeukia Hagen, “ Jaribu
Congressman Luteco. Fischer haongeki.”

Mwanamume mwingine aliyeletwa alikuwa na ombi dogo tu. Jina lake lilikuwa ni Anthony Coppola na alikuwa ni jamaa aliyewahi kufanya kazi za shirika la reli na Don Corleone huko Italia miaka hiyo. Coppola alikuwa anahitaji Dola mia tano ili aanzishe biashara ya mgahawa; Mtaji wa kutosha kuendesha biashara hiyo. Kwa sababu ambazo hazikuwekwa wazi, pesa isingehamishwa kwa njia ya benki. Ila Don aliingiza mkono wake mfukoni na kutoa bunda la pesa. Lilikuwa ni bunda nene kidogo, ila halikuwa linafika pesa iliyoombwa. Don Corleone alimgeukia Hagen na kusema, “Nitakulipa Jumatatu nikienda benki. Naomba nikopeshe dola mia moja.”

Yule mwanamume alianza kusema dola mia nne zingetosha, lakini Don Corleone alimshika bega, huku akisema kwa sauti ya upole, “Hii harusi imenichukulia kiasi kikubwa cha pesa na kuniacha nikiwa kwenye hali mbaya kidogo.”

Akaipokea ile pesa kutoka kwa Hagen na kumpatia Antony Coppola. Hagen alimtazama kwa jicho la furaha. Don alifundisha mara kwa mara kwamba, kama mtu ana moyo wa upendo, basin a aoneshe upendo muda wote. Ilikuwa ni jambo la furaha kwa Anthony Coppola kuona mwanamume kama Don Corleone yupo tayari kukopa kwaajili yake. Sio kwamba Coppola hakuwa anafahamu Don Corleone alikuwa ni milionea, lakini kuna mamilionea wangapi wapo tayari kuwekwa kwenye utata kidogo na marafiki masikini?

Copolla alipotoka, Don aliinua kichwa chake kama anayemuuliza Hagen. Hagen alisema, “Huyu hayupo kwenye orodha, ila Luca Brasi anataka aongee na wewe. Anaelewa hapaswi kuja kukuona sasa hivi ila anataka kukupa pongezi binafsi.”

Kwa mara ya kwanza Don alionekana kukereka. Jibu lilikuwa la kushtusha kidogo. “Kwani ni lazima nimuone?” Aliuliza.

Hagen akainua mabega juu, “Wewe unamfahamu kuliko mimi ninavyomfahamu. Aliniambia anashukuru sana umemualika kwenye harusi. Hakuwa anategemea hilo. Nadhani anataka tu kukupa shukrani.”

Don Corleone alitikisa kichwa kukubali kwamba Luca Brasi aruhusiwe kuja kumuona.

Huko kwenye bustani, Kay Adams alishangazwa na kovu lililokuwa juu ya uso wa Luca Brasi. Alihoji maswali matatu kumhusu Luca. Michael alikuwa amefanya maksudi kumleta Kay kwenye harusi ili aumeze ukweli kuhusu baba yake, Don Corleone. Lakini Kay hakuwa anamuelewa. Hivyo Michael aliamua kumwambia ukweli nusu tena sio kwa njia ya moja kwa moja. Alieleza kwambwa Luca Brasi alikuwa ni moja kati ya wanaume wanaoogopwa sana kwenye ulimwengu wa kiza wa New York. Kipaji chake kikubwa, ilikuwa inasemekana, alikuwa na uwezo wa kutekeleza mauaji yeye binafsi, bila wasaidizi, jambo ambalo lilimfanya iwe ngumu kugundulika na sheria. Michael alitabasamu halafua akaongeza, “Sijui kama yote wanayosema kuhusu huyu
bwana kama ni kweli au la.”

Kwa mara ya kwanza Kay alianza kuelewa. Aliuliza kwa uoga kidogo, “Usiniambie huyo bwana anafanya kazi na baba.”

Michael alijibu, “Takribani miaka kumina tano iliyopita kuna watu walitaka kumtaifisha baba kwenye biashara yake ya kuingiza mafuta. Walienda mbali hadi kujaribu kumuua. Luca Brasi ndiyo aliwatafuta mmoja baada ya mmoja. Habari ni kwamba aliua wanaume sita ndani ya wiki mbali na ile vita yote ikaisha.” Halafu Michael akatabasamu kama vile kila alichoongea kilikuwa ni utani wa kawaida tu.

“Unamaanisha baba yako alipigwa risasi na majambazi?”

“Miaka kumi na tano iliyopita,” Michael alisema.
“Kuanzia hapo kila kitu kimeenda sawa.”

“Unajaribu kunitisha,” Kay alisema. “Au hautaki kunioa. Unajifanya mjanja?”

Michael alitabasamu, “Ninataka tu utakapoamua kuoelewa na mimi uwe umetafakari vyema.”

“Unasema kweli kwamba huyo bwana ameua wanaume sita?”

“Hivyo ndivyo vyombo vya habari vilivyoandika.” Mike alisema. “Hakuna aliyewahi kuthibitisha hilo. Lakini kuna stori nyingine kuhusu huyu jamaa ambayo huwa haisemwi na mtu yeyote. Ni mbaya sana kiasi kwamba mtu yeyote huwa haiongelei hata baba yangu. Kuna jamaa anaitwa Tom Hagen anaifahamu na kuna siku nilimuuliza nikitaka kujua stori ya huyo jamaa hadi niwe na miaka mingapi. Unajua aliniambia nini? Hadi nifikishe miaka mia moja.” Michael akapiga funda la kinywaji chake.

Ama kwa hakika Luca Brasi alikuwa ni aina ya mtu mwenye uwezo wa kumuogopesha hata shetani mwenyewe. Alikuwa mfupi, mwenye fuvu zito na uwepo wake ulifanya kengele za hatari za eneo husika zilie. Uso wake ulikuwa na chapa ya barakoa ya hasira. Macho yake yalikuwa yanafanana nay ale ya maiti. Midomo yake tu ndiyo ilikuwa na mvuto wa uhai.

Sifa ya ukatili wa Brasi ilikuwa ni ya kutisha na alimtii Don Corleone kwa kiwango cha juu sana. Yeye alikuwa ni moja ya nguzo muhimu sana kwenye mfumo wa Don Corleone wa kazi. Aina ya mtu kama yeye ilikuwa ni adimu sana.

Luca Brasi hakuogopa polisi, hakuogopa jamii, hakumuogopa Mungu, hakuogopa kuzimu, hakuogopa au kuwapenda binadamu wenzake. Lakini ni kama alikuwa amechagua kumuogopa na kumpenda Don Corleone. Alipoingia ndani ya ofisi ya Don Corleone alionesha heshima. Akatoa maua yake na kumpatia Don Corleone kama zawadi na kumpatia bahasha iliyokuwa na fedha kama zawadi kwaajili ya maharusi.

Na hicho ndicho kitu alichokuwa anataka kukifanya Hagen aliona mabadiliko kwa Don Corleone. Don alimpokea Brasi kama mfalme ampokeavyo kijakazi aliyefanya kazi kubwa. Kwa kila ishara, kwa kila neon, Don Corleone alionesha wazi kwamba alimthamini sana Luca Brasi. Hakuonesha mshtuko eti ile zawadi ililetwa kwake moja kwa moja. Alikuwa anaelewa.

Hela iliyokuwa kwenye ile bahasha lazima ingelikuwa ni kiasi kikubwa kuliko kiasi kilichotolewa na mtu yeyote. Brasi alikuwa ametumia muda mrefu kuamua aweke kiasi gani, akilinganisha na kila mgeni atakayekuja ataleta kiasi gani. Alitaka kuonekana kama ana heshima zaidi kuliko wote na ndiyo maana aliipeleka bahasha moja kwa moja hadi kwa Don Corleone. Hagen aliona uso wa Brasi ukibadilika kutoka wa kutisha hadi uso wenye furaha. Brasi aliushika mkono wa Don Corleone na kutoka nje ya ofisi bila kuzungumza chochote, Hagen alimshikia Luca Brasi mlango na kutabasamu wakati Luca akitoka nje.

Mlango ulipofungwa, Don Corleone alipumua. Brasi alikuwa ndiye mwanamume pekee anayemtisha. Brasi alikuwa kama ana guvu fulani ya asili, sio ya kuamuriwa ila kujipangia mambo. Hivyo ilitakiwa sana kummudu kwa ustaarabu kama bomu linalokaribia kulipuka. Don aliguna. Alikuwa anajua kuna muda hata bomu linaweza kulipuliwa na lisisababishe madhara. Akainua kichwa
chake kumtazama Hagen. “Bonasera ndiye aliyebakia?”

Hagen alitikisa kichwa kukubali. Don Corleona alitafakari kidogo, na kusema, “Kabla haujamleta ndani, Mwambie Santino aje humu ofifini. Kuna kitu nataka ajifunze.”

Hagen alienda bustanini kumtafuta Sonny Corleone. Alimwambia Bonasera awe mvumilivu na akaelekea walipokuwa wamekaa Michael na mchumba wake. “Mmenionea Sonny?” Aliuliza. Michael alitikisa kichwa .

Mungu wangu, Hagen alijiwazia, Kama Sonny bado alikuwa anamfanyia kazi yule msindikizaji wa bibi harusi basi muda wowote kuna tatizo lingetokea. Mke wake, familia ya huyo binti; Ingelikuwa majanga. Kwa haraka akauendea mlango ambako alimuona Sonny akiingilia alipokuwa akimfuata Lucy kwa nyuma karibu nusu saa iliyopita.

Kay Adams alipomuona Hagen ameondoka akamuuliza Michael, “Huyo ni nani? Uliniambia ni kaka yako mwanzoni lakini mbona jina lake na lako halifanani halafu haonekani kama ana asili ya Italia.”

“Tom ameishi na sisi tangu akiwa na miaka kumi na mbili,” Michael alijibu na kuongeza, “Wazazi wake walifariki na alikuwa anazunguka mitaani kama chokoraa na ugonjwa wa macho. Sonny akamleta nyumbani usiku mmoja na akaishi na sisi. Hakuwa na
sehemu ya kwenda. Alikaa na sisi hadi alipooa.”

Kay Adams alishangaa, “Huo ni upendo wa hali ya juu,” Alisema. “Baba yako ana moyo mzuri sana. Kuchukua na kumrithi mtoto tu hivo na kumlea wakati
tayari ana familia kubwa ya watoto wake wa damu.”

Michael hakuona kama kuna haja ya kumwambia Kay Adams kwamba watu wa Italia waliona familia ya watoto wanne kama familia ndogo sana. Aliishia kusema,
“Tom hakurithiwa. Aliishi na sisi tu, basi.”

“Oh!” Kay alishangaa. “Mbona hakumrithi sasa?”

Michael alicheka, “Kwa sababu baba yangu alisema itakuwa ni kuwakosea heshima wazazi wa Tom kwa
kumbadilishia jina.”

Walimuona Hagen akimwingiza Sonny kupitia milango iliyokuwa inaingia ndani ya ofisi ya Don Corleone halafu Hagen akampa ishara Bonasera aje.

“Mbona wanamsumbua baba yako, kwenye siku muhimu kwa binti yake kama ya leo.” Kay aliuliza.

Michael alicheka tena. “Kwa sababu wanajua kwa tamaduni zetu watu wa Italia hakuna mwanamume anaweza kukataa ombi lolote siku ya harusi ya binti
yake. Kwahivyo wanautumia huo mwanya.”

Lucy Mancini
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom