God existed before time and He created time

Uko vizuri sana mkuu! Nakuelewa!
Naomba msaada wako kwenye hili:
1. Tukiamua au kukubaliana kutumia FACTS kujadili uwepo au kutokuwepo kwa "MUNGU", Source/Origin ya izo FACTS ni ipi?! Tuna imani gani na iyo source/origin ya izo FACTS?? Namaanisha ivi...kama FACT ni "SAYARI KULIZUNGUKA JUA" Je, source/origin ya FACT hii unaiamini kiasi gani??!

Mimi hupenda kujadili mambo kwa kitu kinaitwa "immanent critique".

Immanent critique ni nini? Kwa kifupi, ni namna ya kuchambua hoja kwa kuanza kwa kutomkatalia anayekuhoji, unaaanza kwa kusema "hebu nichukulie kwamba upande wa pili uko sawa na mimi nimekosea, nianzie hapo, halafu nitake kukubaliana na upande wa pili kwa mawazo makunjufu kabisa, lakini, nisikubali kijinga tu, niulize maswali yangu yote mpaka niridhike"

Kihesabu hapondipo unaona habari za "let x =...", yani unapofanya "let x=..." unakuwa hujakubali "x=..." ila unaanza kutafuta jibukwa mfumohuo.

Tukirudi kwenye habari yako.

Umeeleza kuhusu facts. Kuongelea "facts" tu bila framework ni umasikini wa mawazo.Facts zinahitaji framework.

Kuna mfano mmoja wa injinia aliyepewa kazi ya kujenga daraja, akasema siwezi kujenga daraja.

Kwa nini? Akasema, kwa sababu sijaweza kuipata valie of pi in decimal nikaimaliza. Kama unaelewa pi, katika decimal ni irrational number ambayo as far as we can tell hai terminate.

Injinia akagoma kujenga daraja. Akasemaanaweza kujenga daraja halafu kikavunjika, hataki lawama.

Kumbe, kiukweli, value ya pi inayohitajika kujenga daraja inatakiwa kuwa na only four significant figures, huko mbele ni mbwembwe tu.

Ukianza ku question fact, bila kutoa framework, nitakwambia sawa, fact zote ni provisional, kwa sababu kwanza hatujakamilisha framework ya muda,kuna kesho, sasa kesho tukigundua tofauti fact zetu si tutazitupa?

Ukisom Godel's Incompleteness Theorems utaona hakuna fact isiyo provisional na isiyo relative na framework

Ukisom Einstein's Relativity utaona hakuna fact isiyo provisional na isiyo relative na framework

Ukisom Wave Particle duality utaona hakuna fact isiyo provisional na isiyo relative na framework

Ukisom Hegelian Dialectics utaona hakuna fact isiyo provisional na isiyo relative na framework

Ukisom Schrodinger's Cat's experiment utaona hakuna fact isiyo provisional na isiyo relative na framework

Ukisom double split experiment utaona hakuna fact isiyo provisional na isiyo relative na framework

Sasa unapouliza facts,unauliza kwa framework gani? Kwa epistemology gani? Kwa cosmogony gani?

Halafu, nikikwambia facts haziaminiki,tusiziamini, hilo halithibitishi Mungu yupo. In fact habari hizi zinaweza kukupeleka usiamini kwamba wewe mwenyewe upo, kwa sababu wewe mwenyewe unaamini upo kwa kutumia namna fulani ya facts.

Sasa kamawewe hupo, dunia haipo, habari nzima ya kwamba Mungu yupokwa kuwa kakuumba wewe na dunia inakosa msingi.

Utaona kwamba hata ukiishambulia fact na kuisambaratisha, hilo hali prove Mungu yupo, sanasana unaongeza ushahidi kwamba Mungu hayupo.


2. Tukiamua au kukubaliana kutumia LOGIC kujadili uwepo/kutokuwepo kwa "MUNGU". Nini itakua Standard Scale ya kui-qualify hio LOGIC as meaningful??! Kwasababu wote tunajua kwamba when it comes to LOGIC, everybody becomes a LABOUR to His/Her LOGIC (LOGIC becomes a master...the same applies to one's Opinion!). Kwa kusema hivi, nilikutana na Phylosophy ya Einstein, ambayo alitumia this equation (6-3=6) to logically argue in favour of his phyllaophy.!

Mimi nimetumia logical consistency na contradictions kutenga uongo na ukweli.

Hata uki discredit logic, hilohalithibitishi Mungu yupo! Unachotakiwa kufanya ni kuthibitisha Mungu yupo.

Uki discredit logic una establish chaos kwamba hakuna yeyote anayeweza kuthibitisha lolote kwa njia yoyote popote.

Hapo hujathibitisha Mungu yupo. Kinachotakiwa ni uthibitisho kwamba Mungu yupo.

I am doing this by examples to illustrate my concerns about GIVING much EMPHASIS on other people's opinions/logic, and FACTS generated and amplified by "People" to directly affect "Lifestyle"-Religion

Unaelewa kwamba hata wewe hapa umeandika mawazo yako kwa logic ya alphabet ya watu wengine mpaka nikakuelewa?

Mimi natumia logoical consistency na contradictions,na test vitu, sikubali tu.

Mpaka sasa naona logic ya alphabet, kwa kiasi fulani, inafaa kwa matumizi ya majadiliano, kwa sababu nimeitumia kuelewa unachouliza nikakujibu.

Kamaunasema tusitumie kitu chenye logic iliyowekwa na wengine, acha kutumia simu, acha kutumia computer, acha kutumia lugha, acha kutumia alphabet, anzisha kila kitu chako.

Utaweza?

Unaweza kuthibitisha Mungu yupo kwa namna yoyote? Hata tukisema tusitumie logic kwa sababu logic haiaminiki?

Utawasiliana vipi nami hapa kuendeleza mjadala bila kutumia logic japo ya lugha na alphabet?
 
Hapa Chini ulishatoa definition ya muda. Unashindwaje kutumia knowledge yko ku-figure out hyo dhana ya muda in real-time??

Ok! Jibu lako lipo kwenye hyo defn ya pili ya muda uloitoa hapa chini. With reference to Allah's creation, hapo ndipo muda ulipoanzia. Na aliendesha kaz ya uumbaj yeye ndiye alie-determine huwo muda (hence creation). Kama ilivyo ukitaka kuutaja muda tulionao sasa (Gregorian callendar) utasema ni miaka elfu 2 Anno domino (AD) (baada ya kuzaliwa kristo, tukio hilo ndo likawa reference in naming every ensuing year!).
Kama ukitaka muda kabla ya uumbaji ulofanywa na Mungu, huo muda utaitwa "Time before Allah's Creation".
Bottom line: Kama muda ni mstari wa kufikirka ambao matukio yte hutokea juu yake, then in this particular case, what seems to matter the most ni matukio. Anaesababisha tukio ndo yupo entittled to the creation of that time!
Sawa, mkuu nimekueleweni.
 
Then you can't limit/put God in measure of time. Coz time only defines intervals between events. He was before the events. He created laws in which events occur . and one of ts measures/potentials in of power in which the events occur(time).
Ok mkuu.
 
Suala la kutokuwepo Mungu linakuja kwa sababu Mungu (mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote) angekuwepo ulimwengu huu uliojaa kuwezekana mabaya usingekuwepo.

Yani ulimwengu huu unakuwa kama umetokea kinyume na tabia za Mungu. Mungubkasimama lindo ulimwengu huu usiweze kutikea halafu umempiga tobo ukatokea.

Huyo Mungu alisinzia lindoni?
Unaruka ruka tu,umetoka kwenye Mungu kuumba huu ulimwengu ni contradiction na sasa umekuja na madai ya kwamba Mungu angekuwepo huu ulimwengu usingekuwepo.

Kipi kinakufanya uone Mungu anawajibika na huu ulimwengu?
 
Unaruka ruka tu,umetoka kwenye Mungu kuumba huu ulimwengu ni contradiction na sasa umekuja na madai ya kwamba Mungu angekuwepo huu ulimwengu usingekuwepo.

Kipi kinakufanya uone Mungu anawajibika na huu ulimwengu?
Mungu mjuzi wa yote, muweza yote na mwenye upendo wote anaweza kufanya uovu?
 
Mungu mjuzi wa yote, muweza yote na mwenye upendo wote anaweza kufanya uovu?

Kwako wewe Uovu ni nini ?

Hili swali lingine umeuliza la uongo. Sababu Mola hana sifa ya uovu wala kudhulumu bali wala kuonea.

Ila nakukumbusha tu,unapotaka ujibiwe maswali yako na wewe uwe unajibu maswali ya wenzako.

Nasubiri majibu ya maswali yangu ....!
 
Mimi hupenda kujadili mambo kwa kitu kinaitwa "immanent critique".

Immanent critique ni nini? Kwa kifupi, ni namna ya kuchambua hoja kwa kuanza kwa kutomkatalia anayekuhoji, unaaanza kwa kusema "hebu nichukulie kwamba upande wa pili uko sawa na mimi nimekosea, nianzie hapo, halafu nitake kukubaliana na upande wa pili kwa mawazo makunjufu kabisa, lakini, nisikubali kijinga tu, niulize maswali yangu yote mpaka niridhike"

Kihesabu hapondipo unaona habari za "let x =...", yani unapofanya "let x=..." unakuwa hujakubali "x=..." ila unaanza kutafuta jibukwa mfumohuo.

Tukirudi kwenye habari yako.

Umeeleza kuhusu facts. Kuongelea "facts" tu bila framework ni umasikini wa mawazo.Facts zinahitaji framework.

Kuna mfano mmoja wa injinia aliyepewa kazi ya kujenga daraja, akasema siwezi kujenga daraja.

Kwa nini? Akasema, kwa sababu sijaweza kuipata valie of pi in decimal nikaimaliza. Kama unaelewa pi, katika decimal ni irrational number ambayo as far as we can tell hai terminate.

Injinia akagoma kujenga daraja. Akasemaanaweza kujenga daraja halafu kikavunjika, hataki lawama.

Kumbe, kiukweli, value ya pi inayohitajika kujenga daraja inatakiwa kuwa na only four significant figures, huko mbele ni mbwembwe tu.

Ukianza ku question fact, bila kutoa framework, nitakwambia sawa, fact zote ni provisional, kwa sababu kwanza hatujakamilisha framework ya muda,kuna kesho, sasa kesho tukigundua tofauti fact zetu si tutazitupa?

Ukisom Godel's Incompleteness Theorems utaona hakuna fact isiyo provisional na isiyo relative na framework

Ukisom Einstein's Relativity utaona hakuna fact isiyo provisional na isiyo relative na framework

Ukisom Wave Particle duality utaona hakuna fact isiyo provisional na isiyo relative na framework

Ukisom Hegelian Dialectics utaona hakuna fact isiyo provisional na isiyo relative na framework

Ukisom Schrodinger's Cat's experiment utaona hakuna fact isiyo provisional na isiyo relative na framework

Ukisom double split experiment utaona hakuna fact isiyo provisional na isiyo relative na framework

Sasa unapouliza facts,unauliza kwa framework gani? Kwa epistemology gani? Kwa cosmogony gani?

Halafu, nikikwambia facts haziaminiki,tusiziamini, hilo halithibitishi Mungu yupo. In fact habari hizi zinaweza kukupeleka usiamini kwamba wewe mwenyewe upo, kwa sababu wewe mwenyewe unaamini upo kwa kutumia namna fulani ya facts.

Sasa kamawewe hupo, dunia haipo, habari nzima ya kwamba Mungu yupokwa kuwa kakuumba wewe na dunia inakosa msingi.

Utaona kwamba hata ukiishambulia fact na kuisambaratisha, hilo hali prove Mungu yupo, sanasana unaongeza ushahidi kwamba Mungu hayupo.

Ni kweli...mada iliopo mezani ni "Uwepo wa Mungu"
Sasa naomba tukubaliane kitu kimoja just a few inches before we go kwenye mada kuu: UWEPO WA MUNGU HUDHIHIRIKA KWA WALIO NA IMANI JUU YA UWEPO WAKE. JE, WEWE UNA IMANI?? (IMANI/FAITH NI TOTAL SUBMISSION).
Naomba usinielewe vibaya, I am not too religious...ninachojaribu kufanya hapa ni ku-set a ground for our discussion! Kwasababu, imagine...my God is infinity, how can an infinity God be figured out by My "3.2 pound mind"??! The same mind which can be inconsistent due to emotions, environment, physical state and what's not! (this is unfair!)...

Kama ulikua unadhani kua nashambulia "facts" ili niue mjadala. You are wrong! Mi nilitaka wewe uchague "Angle" of discussion...facts, logic au religious belief (which I am sure u arent a fan of this!). Au laah, kama unaona Facts zilizopo zinatosha pasipokua na hofu kuthibitisha kuwepo/kutokuwepo kw Mungu. Basi naomba unithibitishie "IMANI" yako katika chanzo hcho cha Facts utakazozitumia ku support concepts zko! Maana ni dhahir kwmba kwa kiasi kikubwa umewekeza imani yko kwenye hivyo vyanzo!



Mimi nimetumia logical consistency na contradictions kutenga uongo na ukweli.

Hata uki discredit logic, hilohalithibitishi Mungu yupo! Unachotakiwa kufanya ni kuthibitisha Mungu yupo.

Uki discredit logic una establish chaos kwamba hakuna yeyote anayeweza kuthibitisha lolote kwa njia yoyote popote.

Hapo hujathibitisha Mungu yupo. Kinachotakiwa ni uthibitisho kwamba Mungu yupo.

Ndugu yangu, uko nondo sana! Tofauti kati yetu ni kwmba wewe umesahau kuwekeza muda kukijua cha ndani kwako...uka invest kwenye kujua ulicholetewa na "brain-washers". Unachambua maandiko yao, kwa kutumia knowledge waliokupa wao!
Babu zetu hawakua wanaandika sana, lakini nina uhakika babu zetu walikua na ukwel ghafi (Crude Truth) juu ya Mungu waliokua wanamwabudu. Ukiujua ukwel huu, utakusaidia kutafuta imani uliotakiwa kua nayo. Siyo hyo ya kuambukizwa.

Rudi kwenye suala la kutumia Logic. Kwanini unajaribu ku win points kwa kutumia general knowledge ya "logic" badala ya ku establish logic ambayo itatetea au ku materialize msimamo wko juu ya uwepo wa Mungu??!
Sijaona haja ya kuingiza logic ya alphabet kwny mada sensitive kama hii.

When it comes to logic, phylosophy, opinions, everything must have a meaning! Kwahyo kama utategemea Mungu with HIS DEVINE LAWS afanye mambo yake kama HUMAN BEINGS do, then you are wrong. In fact, how men decide logically, mustnt match Allah's decision when He does in His Godly Manner.


Unaelewa kwamba hata wewe hapa umeandika mawazo yako kwa logic ya alphabet ya watu wengine mpaka nikakuelewa?

Mimi natumia logoical consistency na contradictions,na test vitu, sikubali tu.

Mpaka sasa naona logic ya alphabet, kwa kiasi fulani, inafaa kwa matumizi ya majadiliano, kwa sababu nimeitumia kuelewa unachouliza nikakujibu.

Kamaunasema tusitumie kitu chenye logic iliyowekwa na wengine, acha kutumia simu, acha kutumia computer, acha kutumia lugha, acha kutumia alphabet, anzisha kila kitu chako.

Utaweza?

Unaweza kuthibitisha Mungu yupo kwa namna yoyote? Hata tukisema tusitumie logic kwa sababu logic haiaminiki?

Utawasiliana vipi nami hapa kuendeleza mjadala bila kutumia logic japo ya lugha na alphabet?

MUNGU HUJIDHIHIRISHA KWA WALE WENYE IMANI NA UWEPO WAKE. WEWE UPO NJE YA UTARATIBU, UTADHIHIRISHIWAJE UWEPO WAKE.

Kwamfano: UKIAMBIWA KUA NGAMIA AKITAKA KUCHINJWA ANAPIGWA KISOMO MPAKA ANAELEKEA KIBRA MWENYEWE ILI ACHINJWE (Hii inakupa tafsiri gani wewe kama si mtu wa imani??!)
 
MUNGU HUJIDHIHIRISHA KWA WALE WENYE IMANI NA UWEPO WAKE. WEWE UPO NJE YA UTARATIBU, UTADHIHIRISHIWAJE UWEPO WAKE.

Kwamfano: UKIAMBIWA KUA NGAMIA AKITAKA KUCHINJWA ANAPIGWA KISOMO MPAKA ANAELEKEA KIBRA MWENYEWE ILI ACHINJWE (Hii inakupa tafsiri gani wewe kama si mtu wa imani??!)
Hujathibitisha. Unahubiri.
 
Udhibitisho wa namna gani unautaka?? Zaidi ya kazi za mikono yake zinazoji manifest??
Sitaki udhibitisho.

Nataka uthibitisho.

Unaelewa tofauti? Unajua Kiswahili?

Uthibitisho ulio logically consistent na usio na contradiction.

Mungu ana mikono? Ina vidole vingapi?
 
Unaikubali quran kama chanzo chako cha kumuelezea mungu

Je unaweza kuniambia quran kaindika nani?

UANDISHI WA QUR'AN TUKUFU:

Kujibu swami lako kwanza ifahamike kuwa Qur'an ni uteremsho kutoka kwa Mola wa walimwengu wote kuja kwa Mtume wa mwisho ambaye Ni Muhammada Mustafa.
Uteremsho huo ulidumu kwa kipindi cha miaka 23 ya utume wake. Kutoka kwa Mola Kuja kwa Muhammad. Mletaji wa ufunuo (wahyi) huo ni Malaika Mtukufu - Jibril (as) au malaika Gabriel.

Ushahidi:
Tutarejea kwenye Quran yenyewe.
1. Al-Ahqaf :2, "Uteremsho wa kitabu umetoka kwa Mwentezi Mungu, mwenye nguvu, mwenye hikima".
2. Fussilat: 2, "Uteremsho huu umetoka kwa mwingi wa rehema, mwenye kurehemu".
3. As-Sajda: 2, " Huu ni uteremsho wa Kitabu kisichokuwa na shaka yoyote kinachotoka kwa Mola wa walimwengu wote".
4. Pia unaweza kurejea Az-Zumar: 2, Az-Zukhruf:4, Al-Baqara (2:97).

ILIHIFADHIWA VIPI?
Wakati wote ufunuo ukiteremshwa, haikuwa ikiandikwa kwenye sahifa au karatasi bali kwenye Ngozi , mawe, mifupa na kwenye vitambaa. Muhimu zaidi ni kuwa Qur'an ilihifadhiwa kwenye nyoyo za wanafunzi wa Mtume a.k.a Masahaba. Vile haikushuka kama kitabu kimoja au sura moja, mpangilio wake uliratibiwa na Mwenyezi Mungu kwa maelekezo ya Malaika Jibril. Mfano aya zikishuka basi Mtume anaagiza kuwa aya hizi ni katika sura Fulani. hivyo!.
Ilipokuwa utume umekamailika na Mtume tena hayupo, successor wake ambaye ni Abubakar as-Siddiq Allah awe radhi naye alishauriwa kuikusanya Qur'an katika mpangilio wa kitabu kimoja.

Zayd bin Thabit ndiye aliyepewa jukumu la kuikusanya.

Wakati wa utawala wa Uthman bin Affan, Allah awe radhi naye, aliamrisha wandishi waandike Qur'an kwa kunukulu kutoka kwa ile copy iliyokusanywa na Zayd bin Thabit ili isambazwe Africa, Asia na Ulaya.

MAJINA YA WAANDISHI WA QUR'AN TUKUFU.
1. Zayd bin Thabit
2. Abdullah bin Zubeir
3. Said bin Al - `As
4. Abdul-Rahman bin Harith bin Hisham
Mola awarehemu wote - Aamin!

Naamini nimejibu swali lako zuri na nimetimiza wajibu kwa Mola wangu, nami nataraji kamili kutoka kwake.
 
Yes nilitegemea maelezo yake yange-base kwenye uwepo wa Mungu before time and within it and when (maybe) the time was created

Alipokua akitengeneza muda (time) yeye alikua kwenye time zone ipi ?

Maswali ni mengi kuhusu muda kulingana na kichwa cha Uzi
Itakua poa kama ataweka sasa
Habarini wa GT.
Kumekuwa na mgongano wa mawazo kuhusu uwepo na ithibati ya Mungu.Naomba niseme ya kuwa mgongano huu haujaanza leo wala jana bali ni karne kwa karne zimeshapita. Nitaanza kwa kusimulia visa kadhaa kabla ya kujenga hoja.
Mwanafalsafa Plutarch(myunani) aliyekufa mwaka 120b.c na mwandishi wa habari za wayunani na warumi katika kitabu chake kinachoitwa "Parallel lives of illustrious Greek and Romans"aliandika ya kuwa Kuna miji isiyo na kuta, wala vitabu isiyo na mfalme, wala nyumba wala hazina wala mahala pa kuchezea michezo; Lakini hakuna mji usiokuwa na hekalu la Mungu(mungu fulani) hakuna mji huo na hutapata kuuona.

Mwana sayansi wa elimu ya viumbe Athanasius Kirchner(1601-1680) alikuwa na rafiki yake ambaye alikuwa anapinga uwepo wa Mungu. Kuna siku huyu rafiki alimtembelea Kirchner, Alikuta Kirchner ameshika tufe lenye sura ya dunia, kutokana na ustadi uliotumika kulifanya tufe hilo Jamaa akamuliza Kirchner"Nani aliyeufanya mfano wa dunia hivi? Kirchner akajibu Hakuna mtu, umejifanya wenyewe.Jamaa akasema acha kunichekesha aliyeufanya mfano huu lazima awe mstadi mkubwa, Jinsi gani Kirchner akahoji? Hutaki kukubali ya kuwa mfano huu dhaifu wa tufe la dunia umejifanya wenyewe lakini unakazana kuwa dunia hii kubwa (universe) umejifanya wenyewe.
Kuna watu wa aina bado wapo.

WHAT'S INVISIBLE THAT CREATES WHAT'S VISIBLE.

Kama kitu hakithibitishiki kwa milango ya fahamu (pua,ulimi, macho, ngozi,masikio) haifanyi kitu hicho kisiwepo.Kuna ya vitu hauwezi kuthibitisha kupitia milango ya fahamu lakini vipo katika mazingira yetu.Ili kuthibitisha uwepo wa mambo/vitu hivyo tuna angalia athari yake (Low of course and effect)Hapa nitaweka baadhi vitu/mambo hayo ili kuelewa vizuri low hii.
These facts are not all of one kind, some are material and some are non material. We shall mention here a few of them.
Electricity, Gravitation, Magnetism, Invisible radiation, Intelligence, Love, Hate, Determination. and so on.......
Hivi ni baadhi ya vitu/mambo hatuwezi kuthibitisha kwa milango yetu ya fahamu lakini vipo, Tunamini vipo kwasababu ya athari zake.
Kwa hiyo; hoja ya kuwa Mungu hayupo kwa kuwa hatuwezi kumthibitisha kwa milango yetu ya fahamu inakufa/haina uhai kwa scenario hii.
Mungu hujibainisha kwa viumbe wake kupitia alama/sign mbalimbali rejea paragraph za juu hapo(matukio hayo mawili).

Karibuni
Mleta mada umenivuruga kidogo. Mimi naamini kuwa Mungu yupo, lakini unaposema alikuwepo kabla ya muda na yeye ndiye aliyetengeneza muda, ni vipi tukio la yeye kuwepo litokee nje ya muda. Hebu nifafanulie hapo.
 
I'm doubting , "God created out of nothing " what is nothingness ? Where did He stay during the time of creation ? If no answer , then there must be one who created God !
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom