Global Publishers muwe makini

Global Publishers muwe makini

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Uandishi wenu wa kihunihuni ili muuze magazeti yenu utawagharimu siku moja. Nimeshtushwa na jinsi mlivyowahusisha baadhi ya wanafunzi wa Chuo cha Kodi na kifo cha mwanafunzi mwenzao. Katika habari hiyo, mmedai kuwa wanafunzi hao wanadaiwa kumuwekea sumu mwenzao iliyopelekea kifo chake.

Madai juu ya uhai wa mtu ni madai mazito na ya kuogofya kwani yanapelekea kosa la jinai kubwa kabisa la kuua kwa kukusudia. Mlipaswa kuhibitisha uwepo wa vipimo kwenye mwili wa marehemu na ripoti ya awali yauchunguzi wa Polisi juu ya uhusika wa wanafunzi hao kata kifo hicho. Hamkupaswa kisheria na kiuhaisia kuishia mlikoishia katika uandishi wenu. Kma ni makosa ya kiuandishi basi muwe makini wakati mwingine.
 
hili nalo muhimu, hawa jamaa wanamtupia mtu kesi kihunikihuni tuu na hii si mara ya kwanza.
 
Kuna moja ktk gazeti lao waliwahi kuandika eti "Ikulu ya JK iko mbioni kulipuliwa na alshabaab"......gazeti hilo lilinunulika kwa wingi sana, sasa baada ya kusoma ndani ndo ilikuwa ni vioja zaidi....kumbe walikuwa wanaelezea tu ni kwa namna magaidi wanaweza kutekeleza hilo huku wakiwa mbali na wakitumia majengo yaliyo jirani na nyumba hiyo namba moja nchini inayogombewa sana
 
Katika mambo ya hovyo kabisa ambayo Tanzania imeendelea kudumu nayo ni uwepo wa hii kitu inayofahamika kama Global Publishers. Takataka wanazozijaza vichwani mwa wasomaji wa hayo magazeti zitakuja kuligharimu taifa siku moja. Wasomaji wa hayo magazeti ni watoto wa shule na watu wengine ambao kwa asilimia kubwa elimu kwao imekuwa tatizo. Kurasa za magazeti yao zimejaa habari na hadithi zinazohusiana na ngono kwa asilimia kubwa. Media zina nafasi kubwa katika kulijenga taifa ila kwa taifa linalojengwa na hwa glo
 
subiri lowassa akalie kiti huo upumbavu utaisha yule ni mzee wa kazi
 
AMINA+1.jpg


global
 
I never buy tanzanian newspapers, hakuna lenye kuandika mambo ya maana, kungekua na watu wenye ufahamu wa kisheria, kesi zingekuwa nyingi mahakamani.
 
Kuna moja ktk gazeti lao waliwahi kuandika eti "Ikulu ya JK iko mbioni kulipuliwa na alshabaab"......gazeti hilo lilinunulika kwa wingi sana, sasa baada ya kusoma ndani ndo ilikuwa ni vioja zaidi....kumbe walikuwa wanaelezea tu ni kwa namna magaidi wanaweza kutekeleza hilo huku wakiwa mbali na wakitumia majengo yaliyo jirani na nyumba hiyo namba moja nchini inayogombewa sana

Katika magazeti ambayo yanatakiwa kufungiwa basi hili ni moja wapo sijui serikali na wenyewe ni wabia wa haya makitu.
 
Katika magazeti ambayo yanatakiwa kufungiwa basi hili ni moja wapo sijui serikali na wenyewe ni wabia wa haya makitu.

Mwny nayo huyu msukuma mwenzangu huwa anajigamba kuwa ana uswahiba na viongozi wakubwa wa nchi hii unadhan wataanzaje kuyafungia magazeti ya swahiba wao!!
 
Katika mambo ya hovyo kabisa ambayo Tanzania imeendelea kudumu nayo ni uwepo wa hii kitu inayofahamika kama Global Publishers. Takataka wanazozijaza vichwani mwa wasomaji wa hayo magazeti zitakuja kuligharimu taifa siku moja. Wasomaji wa hayo magazeti ni watoto wa shule na watu wengine ambao kwa asilimia kubwa elimu kwao imekuwa tatizo. Kurasa za magazeti yao zimejaa habari na hadithi zinazohusiana na ngono kwa asilimia kubwa. Media zina nafasi kubwa katika kulijenga taifa ila kwa taifa linalojengwa na hwa glo

Niliwahi kusikia mwenye haya magazeti ni mlokole.
 
Msukuma wa bamaga katajirishwa na haya ma toilet paper...
 
katika magazeti nayochukia ni ya global publisher nahisi waandishi wake wana madudu kichwani ndo maana hawaishi kuandika pumba na story za uongo kwenye magazeti yao...sijui TCRA hawayaoni?????
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom