Hii ndo website walotumia
Mbona kama legit?
Sio legit, ila ni matapeli wenye akili kidogo ndio maana unaona wameweza kutengeneza hiyo website ya mchongo. Why nasema sio legit?
Sababu:
1.Uki google jina la organization yao, taarifa pekee ambazo zinatokea kuhusu wao ni za website yao (
www.ghvhi.org), pamoja na haya matangazo yao ya kazi. Hakuna taarifa nyingine yoyote kuwahusu ambayo unaiona kuhusu wao. Eg taarifa kuhusu miradi yao, etc. Hii ni tofauti na organization za aina hii za ukweli ukiingia google unakuta taarifa nyingi nyingi kuwahusu. Hawa jamaa hata hawana LinkedIn page, twitter wala Facebook.
2.Ukiingia kwenye website yao, watu ambao wamewa list kama directors na team members wao, asilimia kubwa hawapo LinkedIn, mtandao mkubwa wa professionals. Wawili ambao wamekua listed as directors wapo LinkedIn, ila ukiangalia profile zao za LinkedIn hazisemi chochote kile kuhusu kuwa viongozi wa hii organization.
3.Kwa kawaida nafasi kama hizi huwa zikitangazwa na organization kunakua na details mfano: Je mradi husika unatekelezwa mikoa ipi na wilaya zipi? Mradi husika ni wa miaka mingapi? Mradi husika umekua funded na nani? Hizo details zote hakuna kwenye hili tangazo lao. Pia, hakuna taarifa zozote kuhusu ilipo ofisi yao kwa Tanzania.
Conclusion: Hawa ni matapeli, ila wamejitahidi sana kufanya high level, hadi uwe na level fulani ya exposure kujua kuwa hawa ni matapeli.