Salaam wanabodi;
Nilichojifunza hadi sasa ni kwamba siasa za Tanzania hazina misingi ya kiitikadi bali zinaendeshwa kwa HASIRA na VISASI vya “wanasiasa wakubwa” ambao wanajaribu kuonesha nguvu zao (wafuasi wao) dhidi ya “mfumo” fulani uliowatenga au waliojitenga nao. Kwa maneno mengine, vyama vya siasa, hasa vya upinzani vinatumika kama majukwaa na wanasiasa wanaojitenga au kutengwa kuonesha nguvu zao au ushawishi walionao dhidi ya hiyo mifumo.
Kwa bahati nzuri au mbaya, wanasiasa wakubwa wote wanasifa zinazofanana. Moja ya sifa zao ni kwamba walishawahi kushika nafasi za juu za uongozi serikalini au kwenye vyama hasa CCM. Hivyo basi kutokana na nafasi za uongozi walizopitia, walipata nafasi nzuri ya kujenga ushawishi na kujitengenezea wafuasi. Sifa ya pili ni kwamba wanasiasa hao, kutokana na hulka zao za kupaparikia urais walikuwa wanatumia mbinu chafu (ukabila, udini, undugu au ukanda) dhidi ya washindani wao wa ndani ambazo hazikubaliki kwa misingi ya vyama vyao hadi wakaishia kujitenga au kutengwa na vyama vyao halisi. Sifa yao nyingine muhimu wanasiasa wakubwa ni kwamba wamekuwa na ndoto ya kushika nafasi ya urais katika nchi hii na hii ndio maana halisi ya kujijengea kwao wafuasi.
Wanasiasa hao hawakati tamaa. Bali wanapokosa fursa ya kugombea urais kupitia majukwaa yao ya asili (vyama) hutafuta majukwaa mengine ili watimize ndoto zao. Wanasiasa hao wakubwa wanapojiunga na vyama vingine, wale wafuasi wao wanakuwa hawana namna bali ili wasibaki wapweke huamua kumfuata “mtu wao” na huu ndo msingi wa kauli mbiu “ULIPO TUPO”. Kwa bahati mbaya sana vyama vya siasa vimebaki kutegemea nguvu za wanasiasa wakubwa wanaohamahama na kwahiyo wenyeji wa vyama hivyo wako tayari KUBADILI GIA ANGANI, KUTOA KADI No. 1 au kusema “KARIBU NYUMBANI” kwa wanasiasa wakubwa wanaohamia.
Matokeo yake kwavile wanaingiza makundi makubwa ya wafuasi wao “ugenini” wanasiasa hao nao hawako tayari kuwa chini ya wenyeji waliowakuta, bali wanajiona kuwa ni wanachama wenye hisa kubwa na hivyo wanataka wabaki kuwa “top and influential” dhidi ya wenyeji wao. Kubadili gia angani, kutoa kadi # 1 na kauli mbiu ya “ulipo tupo” na ile ya “karibu nyumabani” maana yake ni wenyeji kukubali kuacha itikadi na misingi ya vyama vyao na kuwa tayari kuwatukuza na kuendeshwa na utashi wa wageni wao ambao msingi wake ni HASIRA na VISASI dhidi ya mifumo walioihama. Kwakuwa mbali na jina, utambulisho muhimu wa chama cha siasa ni itikadi ambayo ndo msingi wa sera za chama husika, chama kinapobadili gia angani ili kiendane na “hisia” za wageni hupoteza utambulisho wake ambao ndo msingi wa umaarufu wake.
Kwahiyo siku hizi viongozi wa siasa wenye utashi wa kuendeleza kwa kujenga itikadi za vyama vyao kwa wanchi ni wachache sana. Viongozi tulionao ni “opportunistic” kwa maana uwezo wao ni kutumia fursa za kuwapokea wanasiasa wenye hasira na waliojitenga dhidi ya vyama vyao vya asili. Zaidi, tunachokiona ni kutamalaki kwa USALITI (kujivua uwanachama) miongoni mwa makada wa vyama. Hii maana yake ni kwamba wanachama wako “too loose” kwa maana hawajajengeka KIITIKADI bali KIUFUASI wa wanasiasa wakubwa.
Kwa bahati mbaya sana wanasiasa hawajui kwamba mtindo huu wa siasa unadhihirisha rangi zao za asili kwamba hawako pale kutetea wananchi na kuwaletea mabadiliko bali kutafuta maslahi yao binafsi. Bali siasa hizi zinasababisha wanasiasa wanaohamahama kupwaya na kupoteza mvuto kwa sababu wanawangeusha wananchi kutokana na misimamo yao inayobadilika kila msimu. Matokeo yake wananchi (wenye akili) wanahisi hakuna mwanasiasa “mwenye jipya” na ndio maana idadi ya wapiga kura katika chaguzi zinaendelea kushuka.
Hata hivyo ni matumaini yangu kwamba mtindo huu wa siasa utafutika baada ya kizazi cha "wanasiasaa wakubwa" waliojijengea wafuasi kwisha.
Nilichojifunza hadi sasa ni kwamba siasa za Tanzania hazina misingi ya kiitikadi bali zinaendeshwa kwa HASIRA na VISASI vya “wanasiasa wakubwa” ambao wanajaribu kuonesha nguvu zao (wafuasi wao) dhidi ya “mfumo” fulani uliowatenga au waliojitenga nao. Kwa maneno mengine, vyama vya siasa, hasa vya upinzani vinatumika kama majukwaa na wanasiasa wanaojitenga au kutengwa kuonesha nguvu zao au ushawishi walionao dhidi ya hiyo mifumo.
Kwa bahati nzuri au mbaya, wanasiasa wakubwa wote wanasifa zinazofanana. Moja ya sifa zao ni kwamba walishawahi kushika nafasi za juu za uongozi serikalini au kwenye vyama hasa CCM. Hivyo basi kutokana na nafasi za uongozi walizopitia, walipata nafasi nzuri ya kujenga ushawishi na kujitengenezea wafuasi. Sifa ya pili ni kwamba wanasiasa hao, kutokana na hulka zao za kupaparikia urais walikuwa wanatumia mbinu chafu (ukabila, udini, undugu au ukanda) dhidi ya washindani wao wa ndani ambazo hazikubaliki kwa misingi ya vyama vyao hadi wakaishia kujitenga au kutengwa na vyama vyao halisi. Sifa yao nyingine muhimu wanasiasa wakubwa ni kwamba wamekuwa na ndoto ya kushika nafasi ya urais katika nchi hii na hii ndio maana halisi ya kujijengea kwao wafuasi.
Wanasiasa hao hawakati tamaa. Bali wanapokosa fursa ya kugombea urais kupitia majukwaa yao ya asili (vyama) hutafuta majukwaa mengine ili watimize ndoto zao. Wanasiasa hao wakubwa wanapojiunga na vyama vingine, wale wafuasi wao wanakuwa hawana namna bali ili wasibaki wapweke huamua kumfuata “mtu wao” na huu ndo msingi wa kauli mbiu “ULIPO TUPO”. Kwa bahati mbaya sana vyama vya siasa vimebaki kutegemea nguvu za wanasiasa wakubwa wanaohamahama na kwahiyo wenyeji wa vyama hivyo wako tayari KUBADILI GIA ANGANI, KUTOA KADI No. 1 au kusema “KARIBU NYUMBANI” kwa wanasiasa wakubwa wanaohamia.
Matokeo yake kwavile wanaingiza makundi makubwa ya wafuasi wao “ugenini” wanasiasa hao nao hawako tayari kuwa chini ya wenyeji waliowakuta, bali wanajiona kuwa ni wanachama wenye hisa kubwa na hivyo wanataka wabaki kuwa “top and influential” dhidi ya wenyeji wao. Kubadili gia angani, kutoa kadi # 1 na kauli mbiu ya “ulipo tupo” na ile ya “karibu nyumabani” maana yake ni wenyeji kukubali kuacha itikadi na misingi ya vyama vyao na kuwa tayari kuwatukuza na kuendeshwa na utashi wa wageni wao ambao msingi wake ni HASIRA na VISASI dhidi ya mifumo walioihama. Kwakuwa mbali na jina, utambulisho muhimu wa chama cha siasa ni itikadi ambayo ndo msingi wa sera za chama husika, chama kinapobadili gia angani ili kiendane na “hisia” za wageni hupoteza utambulisho wake ambao ndo msingi wa umaarufu wake.
Kwahiyo siku hizi viongozi wa siasa wenye utashi wa kuendeleza kwa kujenga itikadi za vyama vyao kwa wanchi ni wachache sana. Viongozi tulionao ni “opportunistic” kwa maana uwezo wao ni kutumia fursa za kuwapokea wanasiasa wenye hasira na waliojitenga dhidi ya vyama vyao vya asili. Zaidi, tunachokiona ni kutamalaki kwa USALITI (kujivua uwanachama) miongoni mwa makada wa vyama. Hii maana yake ni kwamba wanachama wako “too loose” kwa maana hawajajengeka KIITIKADI bali KIUFUASI wa wanasiasa wakubwa.
Kwa bahati mbaya sana wanasiasa hawajui kwamba mtindo huu wa siasa unadhihirisha rangi zao za asili kwamba hawako pale kutetea wananchi na kuwaletea mabadiliko bali kutafuta maslahi yao binafsi. Bali siasa hizi zinasababisha wanasiasa wanaohamahama kupwaya na kupoteza mvuto kwa sababu wanawangeusha wananchi kutokana na misimamo yao inayobadilika kila msimu. Matokeo yake wananchi (wenye akili) wanahisi hakuna mwanasiasa “mwenye jipya” na ndio maana idadi ya wapiga kura katika chaguzi zinaendelea kushuka.
Hata hivyo ni matumaini yangu kwamba mtindo huu wa siasa utafutika baada ya kizazi cha "wanasiasaa wakubwa" waliojijengea wafuasi kwisha.