Ghorofa hatarishi bado liko wima

Ghorofa hatarishi bado liko wima

Crucifix

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2011
Posts
1,655
Reaction score
593
Nimepita eneo karibu na ghorofa lililoporomoka na kuona lile jingine ambalo mwenyewe aliamriwa kulibomoa bado limesimama dede! Je, amri ya kulibomoa haikuwa sahihi, au kuna zuio mahakamani au ndio akili zimeshahamia kwenye matusi ya wabunge na hakuna anayekumbuka hatari iliyo karibuni?
 
Amri ya papo kwa papo ya Political Engineer Prof. Mama Tibaijuka
 
Amri ya papo kwa papo ya Political Engineer Prof. Mama Tibaijuka

Wanasikilizia kwanza upepo unavumaje, mkuu wa kaya si bado amelala! Wakifanikiwa kulipaka rangi tu, huwezi amini halitabomolewa tena!
 
Infwact, god will never forgive us to break down such beautiful and expensive building. Actually, ni dhambi aisee!! So, we've decided to let it collapse by itself like the fellow storey. What's important for you is 2 run whenever u pass near it coz' still not known the time it's gonna make the decision. However, our experts team is working on it. Most importantly,Never miss news alert 2b updated on the exact time when the dude is gonna get down by itself, OK?
 
Wamepewa siku 30 kufanya hivyo. Tamko lilitolewa tarehe 5 au 6 mwezi wa nne ama sikosei. Waziri alikuwa na hata ya kusema,
“Ninaagiza jengo hilo kuwa libomolewe ndani ya siku 30 kwa gharama za mmiliki na akikaidi atalipishwa faini ya asilimia mbili ya gharama ya kuendeleza pasipokuwa na kibali kwa kila siku hadi atakapotekeleza agizo hilo,” alisema Profesa Tibaijuka na kuongeza;

“Makazi haya yanatakiwa kujengwa majengo yasiyozidi ghorofa 10, lakini katika hili ghorofa ambalo linatakiwa kubomolewa kwanza kiutaalamu halikuzingatia vigezo kutokana na kujengwa kwenye kiwanja chenye mita 150 ambacho ni kidogo.”
 
Nimepita eneo karibu na
ghorofa lililoporomoka na kuona lile jingine ambalo mwenyewe aliamriwa
kulibomoa bado limesimama dede! Je, amri ya kulibomoa haikuwa sahihi, au
kuna zuio mahakamani au ndio akili zimeshahamia kwenye matusi ya
wabunge na hakuna anayekumbuka hatari iliyo karibuni?

Mpaka liue tena ndio akili zitakaa sawa.
 
Nimepita eneo karibu na ghorofa lililoporomoka na kuona lile jingine ambalo mwenyewe aliamriwa kulibomoa bado limesimama dede! Je, amri ya kulibomoa haikuwa sahihi, au kuna zuio mahakamani au ndio akili zimeshahamia kwenye matusi ya wabunge na hakuna anayekumbuka hatari iliyo karibuni?
kwani siku 30 zimeshfika mkuu? au unahesabu usiku na mchana?
 
kwani siku 30 zimeshfika mkuu? au unahesabu usiku na mchana?

Hakuna hata dalili kuwa wanajiandaa kulibomoa ingawa sijui siku ya 30 itafika lini......
 
Back
Top Bottom