Gesi Mtwara: Bibi wa Msimbati, nimeamini maneno yako

Gesi Mtwara: Bibi wa Msimbati, nimeamini maneno yako

Bujibuji Simba Nyamaume

Platinum Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
78,151
Reaction score
166,094
Bibi wa Msimbati alishasema gesi haitoki, CCM na Serikali yake wakaenda kupiga na kuua wananchi wa Mtwara wasio na hatia. Juzi kwa mbwembwe na madaha tumeambiwa mitambo ya kuzalisha Umeme wa gas umewashwa na mgao itakuwa ni jambo lililobaki Kwenye Vitabu Vya historia.

Wakati Simba Chawene alijinasibu kwa madaha mbele ya umma kuwa tatizo la umeme litakua historia, leo gazeti la Mwananchi limeandika Eng. Mramba wa TANESCO anasema mgao wa umeme haukwepeki kwani uzalishaj wa umeme umeshuka toka 561 megawatts mpaka 105 megawatts kutokana na ukame ulioikumba nchi...

Swali la kujiuliza; Gas iliwashwa au ilikua changa la macho?

Maneno ya Bibi wa Msimbati ndio ukweli mtupu, Gesi HAITOKI!
 
Msipoteze muda kujadili Porojo za CCM dawa yakitu chochote kinachokukera nikukitupa so Bado siku chache kufikia tar 25/10/2015 Ondoa matapeli wa uongozi
 
CCM wanapoongopa, wanadhani muda unasimama!

Wadhungu hawakukosea waliposema, time will tell.
 
Tatizo kubwa la viongozi wetu si watu wenye maono....ingekua ni busara ujinadi kwa mbwembwe nyingi ikiwa mmeshatest hiyo mitambo na kuona inafanya kazi ndio mtambe...sasa hata kazi ilikua haijaanza mshatuaminisha mgao hakuna!!haya sasa kazi imebuma mna la kutuambia?? Yaani akili za kitanzania ni Mungu tu ndio anajua.
 
apo mna nipa wakati mgumu kuamini hayo mambo ya upande wa pili kama ni kwel basi inabidi waziri usika inabidi akamuombe radhi bibi
 
Bujibuji

This is from a friend who works in the Oil and Gas sector in the Arab world:

Brother, kuchimba kisima cha Oil or Gas inahesabiwa in days min 15 days max 90 days inategemea na formation ya ardhi kule chini. Na kazi inakwenda sambamba na mabomba (Flowlines) zinazopeleka product to the Gathering Facilities for processing to be ready for delivery katika Main Pipeline inayopeleka Downstream for distribution to the end user, hata hivyo still huko mwisho kuna more facilities that are required like booster pumping stations for Oil and Pressure Reducing Terminals for gas.

Nafaham kwetu Tanzania visima vya gas zaidi ya 30 vishachimbwa tayari. Lakini gas haiwezi kuunganishwa kwa flowlines mpaka kufika katika Upstream Gathering Facilities and Processing Plants kam hizo hazijawa tayari kupokea gas.

These very huge multiphase multistage facilities feed by wells from number of gathering satelite field stationsna kama hizonazo hazijawa tayari no way Kinyerezi or Ubungo can recieve LNG gas for powering the Turbine engjnes.

So kwa case ya Mtwara na Kilwa haiwekani kama zimeshajengwa na ziko tayari. Na abadan huwezi kuunganisha kisima direct to the main line. Gas laizima iwe refregerated and pressure under control to become liquid ndio isafirishwe to any where for use in Tanzania. I guess TPDC and Tanesco hawasemi ukweli.

Nataraji umefaham. Namasteji
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom