Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, akizungumza leo Februari 26, 2026 na waandishi wa habari katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, amezungumzia meli iliyokamatwa nchini El Salvador ikiwa na tani 6.6 za cocaine na kubeba bendera ya Tanzania.
Msigwa amesema meli hiyo ilisajiliwa Zanzibar kupitia wakala, na kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imechukua hatua ya kuifutia usajili meli hiyo.
Soma > El Salvador yakamata tani 6.6 za cocaine, meli iliyobeba unga ina bendera ya Tanzania!
Ikumbukwe kuwa, Februari 19, 2026, katika eneo la La Unión nchini El Salvador, Jeshi la Majini la taifa hilo lilitangaza kukamata meli iliyokuwa imebeba tani 6.6 za dawa za kulevya aina ya cocaine. Mzigo huo ulikuwa ukisafirishwa baharini, umbali wa takriban maili 380 kusini-magharibi mwa pwani ya bahari ya Pasifiki ya nchi hiyo.
Kukamatwa kwa meli hiyo kunatajwa kuwa sehemu ya operesheni za kuimarisha mapambano dhidi ya usafirishaji haramu wa dawa za kulevya katika ukanda huo.
Msigwa amesema meli hiyo ilisajiliwa Zanzibar kupitia wakala, na kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imechukua hatua ya kuifutia usajili meli hiyo.
Soma > El Salvador yakamata tani 6.6 za cocaine, meli iliyobeba unga ina bendera ya Tanzania!
Ikumbukwe kuwa, Februari 19, 2026, katika eneo la La Unión nchini El Salvador, Jeshi la Majini la taifa hilo lilitangaza kukamata meli iliyokuwa imebeba tani 6.6 za dawa za kulevya aina ya cocaine. Mzigo huo ulikuwa ukisafirishwa baharini, umbali wa takriban maili 380 kusini-magharibi mwa pwani ya bahari ya Pasifiki ya nchi hiyo.
Kukamatwa kwa meli hiyo kunatajwa kuwa sehemu ya operesheni za kuimarisha mapambano dhidi ya usafirishaji haramu wa dawa za kulevya katika ukanda huo.