DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
"Nilikataa kukatwa mguu, lakini madaktari waliniambia nimechelewa kupata matibabu." Huo ni ushuhuda wa kusikitisha wa George Chipeta (24), fundi wa umeme wa magari mkazi wa Banana, mkoani Dar es Salaam aliyetoa maelezo mbele ya Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Oktoba 29, 2025.
George, ambaye sasa analazimika kuishi bila mguu wake wa kulia, ameiambia Tume jana, Januari 19, 2026, kuwa alipigwa risasi na askari polisi mchana wa tarehe 29 Oktoba akiwa katika shughuli zake za kutafuta vipuri (spare parts) maeneo ya Vingunguti.
Siku ya tukio, George alikuwa ametoka ofisini kwake Banana kuelekea Tabata kununua booster ya gari. Wakati akirudi kwa kutumia pikipiki yake kupitia njia ya Vingunguti, alikutana na kundi la watu wapatao 50 hadi 70 wakikimbizana na gari la polisi (Defender). Amesema alipatwa na hofu akageuza pikipiki ili aondoke. Wakati anageuza, ndipo akapigwa risasi ya paja kutokea nyuma iliyokata mishipa ya damu.
George, ambaye sasa analazimika kuishi bila mguu wake wa kulia, ameiambia Tume jana, Januari 19, 2026, kuwa alipigwa risasi na askari polisi mchana wa tarehe 29 Oktoba akiwa katika shughuli zake za kutafuta vipuri (spare parts) maeneo ya Vingunguti.
Siku ya tukio, George alikuwa ametoka ofisini kwake Banana kuelekea Tabata kununua booster ya gari. Wakati akirudi kwa kutumia pikipiki yake kupitia njia ya Vingunguti, alikutana na kundi la watu wapatao 50 hadi 70 wakikimbizana na gari la polisi (Defender). Amesema alipatwa na hofu akageuza pikipiki ili aondoke. Wakati anageuza, ndipo akapigwa risasi ya paja kutokea nyuma iliyokata mishipa ya damu.