PreGE2025 GEITA: UVCCM yasema CCM haijaruhusu fujo na harakati kwenye majimbo

PreGE2025 GEITA: UVCCM yasema CCM haijaruhusu fujo na harakati kwenye majimbo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Wont be the same

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
1,564
Reaction score
2,483
Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Geita kimetoa wito kwa wanachama wake kuzingatia utulivu na kuheshimu taratibu zilizowekwa wakati wa kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

Akizungumza na wanachama wa CCM katika Kata ya Uyovu Wiaya ya Bukombe, Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Geita Manjale Magambo, amesema chama kimetangaza mchakato wa kuchukua fomu ifikapo Aprili mosi ya mwaka huu, lakini hakijaruhusu kuanza kwa fujo na harakati zisizo rasmi katika kata na majimbo.

“Tunaheshimu na kutambua uwepo wa madiwani na wabunge waliopo kwa sasa, ambao bado hawajamaliza muda wao. Hivyo ni muhimu kufuata utaratibu bila kusababisha migawanyiko ndani ya chama,” amesema Magambo.
 
Back
Top Bottom