Gazeti RAI laishambulia CHADEMA

Gazeti RAI laishambulia CHADEMA

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Gazeti la RAI limeshambulia vikali chama cha CDM kwa kile lilichodai kufuja pesa ovyo kwa operesheni M4C huku chama hicho kikishindwa vibaya kwenye uchaguzi wa madiwani.
Gazeti hilo limedai matokeo hayo ya Chadema hayaridhishi kabisa wananchi ikilinganishwa na nguvu kubwa iliyotumiwa na chama hicho.
Matokeo ya udiwani yanaonyesha mgawanyo wa viti ulikuwa CCM 22 CDM 5 TLP 1 CUF 1.Hata hivyo CDM ikifanikiwa kurejesha viti vyake 2 huku ikiinyanganya CCM viti 3.

My Take:
Gazeti la RAI miezi iliyopita lilikuwa limeanza kurudu katika ramani yake kwa kutoa habari bila upendeleo lakini tangu Prince Bagenda aajiriwe kama Mhariri Mkuu amekuwa na chuki kubwa dhidi ya chama cha CDM na habari za gazeti hilo kila wiki zimekuwa zikikishambulia vikali chama hicho.Pia tangu Bagenda aajiriwe kumekuwa na makala maalum kila wiki za kushambulia viongozi wa chama hicho hasa Mkiti Freeman Mbowe n Katibu Mkuu Dr Wilbroad Slaa.Hata hivyo soko la gazeti hilo kwa sasa tangu aajiriwe Bagenda limeporomoka vibaya sana.
 
Prince Bagenda ameliangamiza kabisa RAI.Tangu aajiriwe sijawahi kununua hilo gazeti nu afadhali nisome magazeti ya udaku.
 
Mkuu fmpiganaji,
Pole sana, hilo gazeti siyo la kusoma hutopata mawazo chanya utapotea...
Bora utulie JF utapata kila kitu, maana huko baada ya kulifundia Mwanahalisi,
sijawahi soma wala nunu gazeti... na hapa JF post ya MMJ ni janga...
 
fmpiganaji, hili gazeti haliwezi hata siku moja kuiandika vizuri CDM kwa sababu ndio waliomfanya bosi wao ajiuzuru ubunge wa Igunga. Lakini pia 'Profesa' J. aliimba "ili nifanikiwe ninahitaji marafiki, ili nifanikiwe zaidi nahitaji maadui. Maadui wa CDM wamekuwa wakitoa mchango mkubwa sana (japo bila kulitambua hilo). M4C inatesa watu wengi sana, kwa kuona haraka unaweza kuona kuwa haijafanya kitu, ila kiukweli kuna kitu kikubwa sana kimefanyika, Vijana ambao bado wamenyimwa haki yao ya kupiga kura ni wangapi katika hizo kata, uandikishaji ulifanyika 2010. Siumizwi na wakala wa NYINYIEM (RAI) ila ni kuongeza umakini ktk M4C inayofuata.
 
He hivi kumbe gazeti la Rai bado lipo, mi hili gazeti liliponunulia tu na Rostam I kissed it goodbye!
 
Kwani yeye anafikiri diwani ni nani hasa?asubiri 2015 aache propaganda!
 
Huyu jamaa alikuwa na jenerali ulimwengu ,salva rweyemamu, Padri privatus karugendo ,muhingo na wengine tu enzi za gazeti la rai .

Baada ya kuuzwa wananunuzi wakafikri na waandishi akili zao pia wamezinunua ,jamaa wakaachia gazeti wakaanzisha raia mwema vichwa vyote vikahama.

Isipokuwa Prince Bagenda aliyepewa jukumu la kuandika makombora enzi za mh.Kikwete baada ya ushindi Salva Rweyemam akapewa mwandishi wa rais,Bagenda ama misimamo yake ama hulka yake akaachwa,wenzie wote wakahamia gazeti la raia mwema.

Bagenda nampenda namheshimu ila ana udhaifu wake anatumiwa ana misimamo mikali akishika kalamu akakaa chini kama uko ofisini utatafuta pa kutokea ,kumbukeni enzi za gazeti la rai kipindi cha mkapa ,ila cha muhimu shujaa mmoja akipotea huzaliwa wengine .mwanahalisi ikazaliwa.
 
fmpiganaji, hili gazeti haliwezi hata siku moja kuiandika vizuri CDM kwa sababu ndio waliomfanya bosi wao ajiuzuru ubunge wa Igunga. Lakini pia 'Profesa' J. aliimba "ili nifanikiwe ninahitaji marafiki, ili nifanikiwe zaidi nahitaji maadui. Maadui wa CDM wamekuwa wakitoa mchango mkubwa sana (japo bila kulitambua hilo). M4C inatesa watu wengi sana, kwa kuona haraka unaweza kuona kuwa haijafanya kitu, ila kiukweli kuna kitu kikubwa sana kimefanyika, Vijana ambao bado wamenyimwa haki yao ya kupiga kura ni wangapi katika hizo kata, uandikishaji ulifanyika 2010. Siumizwi na wakala wa NYINYIEM (RAI) ila ni kuongeza umakini ktk M4C inayofuata.......

Mkuu ingwe,umenena ukweli mtupu.Bagenda haelewi hata kupiga propaganda.Watu siku hizi ni wajanja sana.Na kwa taarifa yake M4C itaendelea kwa kishindo.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
huyu jamaa alikuwa na jenerali ulimwengu ,salva rweyemamu , padri privatus karugendo ,muhingo na wengine tu enzi za gazeti la rai.

Baada ya kuuzwa wananunuzi wakafikri na waandishi akili zao pia wamezinunua ,jamaa wakaachia gazeti wakaanzisha raia mwema vichwa vyote vikahama.

Isipokuwa prince bagenda aliyepewa jukumu la kuandika makombora enzi za mh.kikwete .baada ya ushindi .salva rweyemam akapewa mwandishi wa rais ,bagenda ama misimamo yake ama hulka yake akaachwa ,wenzie wote wakahamia gazeti la raia mwema.

Bagenda nampenda namheshimu ila ana udhaifu wake anatumiwa ana misimamo mikali akishika kalamu akakaa chini kama uko ofisini utatafuta pa kutokea ,kumbukeni enzi za gazeti la rai kipindi cha mkapa ,ila cha muhimu shujaa mmoja akipotea huzaliwa wengine MwanaHalisi ikazaliwa ........

Ukinikumbusha Mwanahalisi natamani nilie kwa uchungu.Lakini Mungu yupo atajibu maombi siku si nyingi.
 
Nimelinunua gazeti la Rai, na nimelisoma lote lakini sijaona sehemu yoyote limeishambulia Chadema. Rai limeandika Chadema wamepata viti 5 vya Udiwani, CCM wamepata viti 22 vya Udiwani...sasa hapo kuna kosa gani.
 
Kwani ccm walishinda uchaguzi wa 2005 kwa kutumia shilingi ngapi?si yale mabilioni zaidi ya 139 ya epa?vipi uchaguzi wa 2010 ambao ccm ilipita kwa tabu sana walitumia shilingi ngapi?vipi arumeru mashariki?
 
Prince Bagenda ameliangamiza kabisa RAI.Tangu aajiriwe sijawahi kununua hilo gazeti nu afadhali nisome magazeti ya udaku.

Ebu niambie kosa la gazeti la Rai ni nini?
 
Bagenda ni mtu wa njaa sana!

Hata mimi si mnunuzi wa gazeti hili toka limemilikiwa na Rostam Aziz kutoka mikononi mwa Jenerali Ulimwengu & Co.
Lakini ni lazima twende mbele na turudi nyuma kidogo. Si kila kinachozungumzwa negative kuhusu CDM ni kibaya kweli. Negativity nyingine ni sehemu ya kujenga. Huwezi kuwa na taasisi Malaika isiyokosea au kuhitaji kukosolewa. Hii habari haiwezi kuwa shambulio.

Tunaweza tukabeza habari hii ya gazeti la RAI lakini principally unapoendesha project lazima uzingatie uwiano wa input na output. Kilichofanywa na gazeti la RAI ni kupima mambo hayo. Sasa kinachotakiwa kufanywa na CDM ni kukanusha kwa kuegemea mizania hiyohiyo ya INPUT na OUTPUT. Sasa suala linahojiwa na RAI ni Je Input ya CDM kwenye chaguzi hizo za udiwani inaoana na output? Hapo ndipo pa kuanzia kujadili na kupatolea ufafanuzi.

Tukianza kushambulia gazeti bila kuona mantiki ya kilichoandikwa tutakuwa tunakosea sana na huko si kukisaidia chama.
 
Nimelinunua gazeti la Rai, na nimelisoma lote lakini sijaona sehemu yoyote limeishambulia Chadema. Rai limeandika Chadema wamepata viti 5 vya Udiwani, CCM wamepata viti 22 vya Udiwani...sasa hapo kuna kosa gani.

Huwa mnamlipa Bagenda shilingi ngapi?
 
Kweli upenzi unawasumbua na utakiangamiza chama chenu huku mnakiona! Badala ya kujadili hoja mnajadili mtu. Hivi ni watu gani nyie ambao mnaamini kwamba mko perfect? There is only one perfect being.
 
Hata mimi si mnunuzi wa gazeti hili toka limemilikiwa na Rostam Aziz kutoka mikononi mwa Jenerali Ulimwengu & Co.
Lakini ni lazima twende mbele na turudi nyuma kidogo. Si kila kinachozungumzwa negative kuhusu CDM ni kibaya kweli. Negativity nyingine ni sehemu ya kujenga. Huwezi kuwa na taasisi Malaika isiyokosea au kuhitaji kukosolewa. Hii habari haiwezi kuwa shambulio.

Tunaweza tukabeza habari hii ya gazeti la RAI lakini principally unapoendesha project lazima uzingatie uwiano wa input na output. Kilichofanywa na gazeti la RAI ni kupima mambo hayo. Sasa kinachotakiwa kufanywa na CDM ni kukanusha kwa kuegemea mizania hiyohiyo ya INPUT na OUTPUT. Sasa suala linahojiwa na RAI ni Je Input ya CDM kwenye chaguzi hizo za udiwani inaona na output? Hapo ndipo pa kuanzia kujadili na kupatolea ufafanuzi.

Tukianza kushambulia gazeti bila kuona mantiki ya kilichoandikwa tutakuwa tunakosea sana na huko si kukisaidia chama.

CDM kamwe haiwezi kutoa taarifa kujibu gazeti la udaku kama Rai
 
Back
Top Bottom