Ukimsoma semtawa ndie ambae huandika story nyingi za ZITTO,SITA,MEMBE,CHENGE.na hivi karibuni amekuwa ni kijana ambae anafanya kazi kwa kusaidia mawazo ya BOSI WETU anaitwa MAKUNGA na Pia hapa ndani sisi humuita jembe la IKULU, ukitazama mahusiano ya IKULU,ZITTO na mpango mchafu wa [COLOR="blue"]kukibomoa chama chetu vyote hivi vitakueleza nini bwana mdogo [/COLOR]semtawa anafanya
Osama is killed, Gaddafi is on pipeline!
Oh My God, kwa mara ya kwanza!!!!!????? mwandishi/msemaji anataka nielewe nini hapa jamani?
Kazi kweli kweli sijui kama mutaweza kubomoa chama kwa sasa hivi wananchi wanajua yote hayo siku nyingi ndugu mwakilishi wa magambaAcha uongo wewe! Kitila Mkumbo ni member wa hicho kikao na hakukana yote hayo. kaangalie post ya "shibuda Out"!
Ukipenda tumia na akili wewe!
SPOT-ONUkweli unauma mwandishi alicho fanya ni kuandika ukweli mtupu. Ndio maana hata gazeti lenu la Tanzania Daima halikugusia habari hizo kwa vile limewaumbua kambi ya boss wao Mbowe
Wasipotaka kuelewa ushauri huu wa bure na kufanya mabadiliko kadri inavyohitajika hicho chama tutakikuta makumbusho ya taifa.SPOT-ON
GeniusBrain, kuna waliokunywa maji ya bendera ya CDM hawaelewi ukweli hata ukiwa usoni kwao.
Tumesema tena na tena ufisadi vile vile upo CDM kwa vile chama kinaendeshwa na wafanyabiashara, mtoa mada na wengine wengi ni wavivu wa kulielewa hilo.
Wadau,
Nilipata mshtuko mkubwa niliposoma habari ya mgogoro baina ya kambi ya Zitto na Mbowe leo asubuhi.Habari ile iliandikwa kama vile ni gazeti la uhuru au Jambo leo. Wakati napitia ile habari niliamua kutoimalizia baada ya kumsoma mwandishi wa habari aliyeripoti ile habari.Huyo mwandishi ni mfuasi na shabiki mkubwa wa Zitto Zubeir Kabwe.
Mimi ni msomaji mzuri wa magazeti na ili kuthibitisha haya ninaomba wadau mrudi nyuma hadi kipindi cha wabunge kususia hotuba ya Rais bungeni,mwandishi aliandika habari kuonyesha kwamba kuna mgogoro mkubwa kati ya wabunge wa kambi ya mbowe na Zitto.Kipindi cha uchaguzi wa chama mwaka 2014 mwandishi huyu alimshabikia sana Zitto na kuonyesha kuna mgogoro mkubwa sana na chama kimegawanyika mapande mawili.
Mwandishi huyu habari zake ni za kushangaza hasa inapoonekana kuna tofauti ya mawazo kwenye vikao na hupenda yeye kuita mgogoro.
Hivi kweli kwa mfano wa suala la Shibuda kung'olewa ilipigwa kura na wajumbe 18 wakaunga mkono huku 1 akipinga,mwandishi anapata wapi ujasiri wa kusema kambi ya Mbowe imemfukuza Shibuda.?? Inaonekana mwandishi huyu ana malengo maalum na hiyo habari aliandikiwa na mjumbe aliyekuwepo kwenye kamati kuu ili kuleta chokochoko kwa wanachama.Ni wazi mtakuwa na jibu ni nani aliyempa hiyo habari ya uchochozi.
Ushauri:
Gazeti la mwananchi ni miongoni mwa magazeti yanayopendwa na kuaminiwa sana na wananchi kutokana na habari zake.Namshauri mhariri asipoteze imani hii na azihariri mara mbilimbili habari zinazoletwa na huyu mwandishi kuhusiana na chadema kwani ana kikundi anachokipigania kwa maslahi fulani......
Nawasilisha....
Tatizo mmezoea mtu mmoja anawaamulia wote kule kwenye chama chenu, hapa cdm ni kujadili, kukubali kutokubaliana kisha kufanya uamuzi wa pamoja. Democrasia si mgogoro jamani fungueni macho wala sioni mgogoro hapa!
lakini na sisi chadema tupunguze migogoro hii ni imezuka mpaka,
ukisoma vizuri chanzo ni LEMA
HABARI YENYEWE HIYO HAPO
Moto wawaka Chadema, NI VITA YA KAMBI ZA MBOWE, ZITTO
Habari kutoka ndani ya kikao hicho cha Kamati Kuu na kuthibitishwa na baadhi ya wajumbe wa kikao hicho zinasema kuwa mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema, ndiye alianzisha mvutano wa kutaka Zitto ang'olewe kutokana na kupinga wazo la kununua magari chakavu kutoka India.
Chanzo chetu cha uhakika kilidokeza kuwa mashambulizi dhidi ya Zitto yalianza pale alipounga mkono hoja ya Profesa Mwesiga Baregu na Dk Kitila Mkumbo ambao walinukuliwa wakisema kwamba, isingekuwa sahihi kwa chama hicho kinachopinga ufisadi kufanya ufisadi kwa kununua magari chakavu wakati wamekuwa wakiibana serikali isifanye hivyo.
Baada ya Zitto kuunga mkono hoja hiyo, vyanzo hivyo nifafanua kuwa ndipo vurugu zilipoanza kwani Lema alianza kumrushia vijembe akisema kwamba Zitto ni tatizo na kwamba amekuwa akimtetea Shibuda.
Habari zinasema baadhi ya wajumbe walisema hoja ya Lema haikuwa na nguvu ya kumshutumu Zitto kwani Shibuda ni mbunge halali wa Chadema.
Duru zaidi za kisiasa kutoka ndani ya kikao hicho zinasema wakati mvutano huo ukiendelea, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa alikuwa kimya huku kwa mara ya kwanza Mbunge wa Ubungo, John Mnyika akiwa mmoja wa wajumbe waliomtetea Zitto.
"Wakati Lema akisema hivyo, Dk Slaa wakati wote alikuwa kimya na hakusema chochote. Mnyika alisimama na kumtetea Zitto kwa mara ya kwanza, na katika utetezi pia alikuwepo Grace Kiwelu," kiliweka bayana chanzo hicho.
Katika majibizano hayo inadaiwa ulifika wakati Zitto alisimama na kumwambia mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, kwamba mpango mkakati wake huo wa kujenga mtandao utakuja kumgharimu katika siku za usoni."Zitto alimwambia Mbowe mpango wake huo wa kujenga mtandao ungekuja kumletea matatizo hapo baadaye, "kilisema chanzo hicho kikimnukuu Zitto ndani ya kikao.
MY TAKE: kama hukusoma habari yote umekuja na hii hoja kutoka wapi? soma habari nzima ili uwe na uchambuzi wa kutosha, haya mambo ya watu siku hizi kujifanya mimi sitaki kusoma hiki kisha unajifanya kuelemisha watu kwa hoja uliyokataa kuisoma sio akili kabisa, si ni ili gazeti kila siku tunalisifia na lina aminika na watanzania wote, hata kwenye uchaguzi lilitusaidia sana chadema kwa kuandika habari huru na ukweli, tung'oe mzizi wa fitina kuna kitu ndani ya chama hakiko sawa na kukubali marekebisho nao ni ukomavu.
huu sio wakati wa kulazimisha vyombo vya habari kuegemea upande wetu wakati kuna madudu yanafanyika.
kama huyo lema hatopewa elimu ya jinsi ya kuongea na watu basi kuna mengi yatatokea, yeye anadhani ni shujaa wa taifa ili na hiyo ni uruka mbaya, lazima wote tusimame pamoja
inaonekana kuna mpango maalumu umewekwa kuidhoofisha CDM lkn kwa nguvu ya umma naamini hawataweza hawa wazandiki hivyo basi muda ndio utakaowaumbua:bange::bange::bange:
swali, je aliyoandika ni ya uongoo?.. Kama ni ya Uongo mwaga ukweli hapa, Ila ukiishia tuu kumlaumu mwandishi wa habari eti kisa 'Zitto' katajwa humo unakua kama mkurupukaji tuu!..
Wadau,
Nilipata mshtuko mkubwa niliposoma habari ya mgogoro baina ya kambi ya Zitto na Mbowe leo asubuhi.Habari ile iliandikwa kama vile ni gazeti la uhuru au Jambo leo. Wakati napitia ile habari niliamua kutoimalizia baada ya kumsoma mwandishi wa habari aliyeripoti ile habari.Huyo mwandishi ni mfuasi na shabiki mkubwa wa Zitto Zubeir Kabwe.
Mimi ni msomaji mzuri wa magazeti na ili kuthibitisha haya ninaomba wadau mrudi nyuma hadi kipindi cha wabunge kususia hotuba ya Rais bungeni,mwandishi aliandika habari kuonyesha kwamba kuna mgogoro mkubwa kati ya wabunge wa kambi ya mbowe na Zitto.Kipindi cha uchaguzi wa chama mwaka 2014 mwandishi huyu alimshabikia sana Zitto na kuonyesha kuna mgogoro mkubwa sana na chama kimegawanyika mapande mawili.
Mwandishi huyu habari zake ni za kushangaza hasa inapoonekana kuna tofauti ya mawazo kwenye vikao na hupenda yeye kuita mgogoro.
Hivi kweli kwa mfano wa suala la Shibuda kung'olewa ilipigwa kura na wajumbe 18 wakaunga mkono huku 1 akipinga,mwandishi anapata wapi ujasiri wa kusema kambi ya Mbowe imemfukuza Shibuda.?? Inaonekana mwandishi huyu ana malengo maalum na hiyo habari aliandikiwa na mjumbe aliyekuwepo kwenye kamati kuu ili kuleta chokochoko kwa wanachama.Ni wazi mtakuwa na jibu ni nani aliyempa hiyo habari ya uchochozi.
Ushauri:
Gazeti la mwananchi ni miongoni mwa magazeti yanayopendwa na kuaminiwa sana na wananchi kutokana na habari zake.Namshauri mhariri asipoteze imani hii na azihariri mara mbilimbili habari zinazoletwa na huyu mwandishi kuhusiana na chadema kwani ana kikundi anachokipigania kwa maslahi fulani......
Nawasilisha....