Wadau,
Nilipata mshtuko mkubwa niliposoma habari ya mgogoro baina ya kambi ya Zitto na Mbowe leo asubuhi.Habari ile iliandikwa kama vile ni gazeti la uhuru au Jambo leo. Wakati napitia ile habari niliamua kutoimalizia baada ya kumsoma mwandishi wa habari aliyeripoti ile habari.Huyo mwandishi ni mfuasi na shabiki mkubwa wa Zitto Zubeir Kabwe.
Mimi ni msomaji mzuri wa magazeti na ili kuthibitisha haya ninaomba wadau mrudi nyuma hadi kipindi cha wabunge kususia hotuba ya Rais bungeni,mwandishi aliandika habari kuonyesha kwamba kuna mgogoro mkubwa kati ya wabunge wa kambi ya mbowe na Zitto.Kipindi cha uchaguzi wa chama mwaka 2014 mwandishi huyu alimshabikia sana Zitto na kuonyesha kuna mgogoro mkubwa sana na chama kimegawanyika mapande mawili.
Mwandishi huyu habari zake ni za kushangaza hasa inapoonekana kuna tofauti ya mawazo kwenye vikao na hupenda yeye kuita mgogoro.
Hivi kweli kwa mfano wa suala la Shibuda kung'olewa ilipigwa kura na wajumbe 18 wakaunga mkono huku 1 akipinga,mwandishi anapata wapi ujasiri wa kusema kambi ya Mbowe imemfukuza Shibuda.?? Inaonekana mwandishi huyu ana malengo maalum na hiyo habari aliandikiwa na mjumbe aliyekuwepo kwenye kamati kuu ili kuleta chokochoko kwa wanachama.Ni wazi mtakuwa na jibu ni nani aliyempa hiyo habari ya uchochozi.
Ushauri:
Gazeti la mwananchi ni miongoni mwa magazeti yanayopendwa na kuaminiwa sana na wananchi kutokana na habari zake.Namshauri mhariri asipoteze imani hii na azihariri mara mbilimbili habari zinazoletwa na huyu mwandishi kuhusiana na chadema kwani ana kikundi anachokipigania kwa maslahi fulani......
Nawasilisha....
Nilipata mshtuko mkubwa niliposoma habari ya mgogoro baina ya kambi ya Zitto na Mbowe leo asubuhi.Habari ile iliandikwa kama vile ni gazeti la uhuru au Jambo leo. Wakati napitia ile habari niliamua kutoimalizia baada ya kumsoma mwandishi wa habari aliyeripoti ile habari.Huyo mwandishi ni mfuasi na shabiki mkubwa wa Zitto Zubeir Kabwe.
Mimi ni msomaji mzuri wa magazeti na ili kuthibitisha haya ninaomba wadau mrudi nyuma hadi kipindi cha wabunge kususia hotuba ya Rais bungeni,mwandishi aliandika habari kuonyesha kwamba kuna mgogoro mkubwa kati ya wabunge wa kambi ya mbowe na Zitto.Kipindi cha uchaguzi wa chama mwaka 2014 mwandishi huyu alimshabikia sana Zitto na kuonyesha kuna mgogoro mkubwa sana na chama kimegawanyika mapande mawili.
Mwandishi huyu habari zake ni za kushangaza hasa inapoonekana kuna tofauti ya mawazo kwenye vikao na hupenda yeye kuita mgogoro.
Hivi kweli kwa mfano wa suala la Shibuda kung'olewa ilipigwa kura na wajumbe 18 wakaunga mkono huku 1 akipinga,mwandishi anapata wapi ujasiri wa kusema kambi ya Mbowe imemfukuza Shibuda.?? Inaonekana mwandishi huyu ana malengo maalum na hiyo habari aliandikiwa na mjumbe aliyekuwepo kwenye kamati kuu ili kuleta chokochoko kwa wanachama.Ni wazi mtakuwa na jibu ni nani aliyempa hiyo habari ya uchochozi.
Ushauri:
Gazeti la mwananchi ni miongoni mwa magazeti yanayopendwa na kuaminiwa sana na wananchi kutokana na habari zake.Namshauri mhariri asipoteze imani hii na azihariri mara mbilimbili habari zinazoletwa na huyu mwandishi kuhusiana na chadema kwani ana kikundi anachokipigania kwa maslahi fulani......
Nawasilisha....