Gazeti la Mwanahalisi linatafuta cha kusema pindi baraza la Mawaziri litakapotangazwa

TataMadiba

JF-Expert Member
Feb 7, 2014
9,866
5,742
LEO 07/12/205 gazeti la Mwanahalisi kwenye ukurasa wa mbele limeandika kichwa cha habari kinachosema "MAWAZIRI WAVUJA" huku kukiwa na picha ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli na picha watu wanane, wakiwa Wabunge na wengine wasiyo Wabunge kuwa ni miongoni mwa Mawaziri wateule katika baraza la Mawaziri atakaloliunda rais.
Mwanahalisi hawana jipya hapa. wanatafuta tu sifa na jambo la kusema pindi tu Rais atakapotangaza bazara la mawaziri.
Pamoja na mambo ambayo wataandika baada ya baraza kutangazwa yatakuwa ni:
1. Rais amepangua baraza na kuja na majina mapya baada ya yale ya awali kuvuja na kuandikwa na gazeti hili(MWANAHALISI). Huu utakuwa ni upuuzi mtupu, yaani rais ajichimbie takribani mwezi mmoja kwa lengo la kujiridhisha na aina ya watu anaowataka halafu, kwa sababu tu MWANAHALISI limewaandika awaache?
2. MWANAHALISI lilishaandika majina haya kuwa ni miongoni mwa baraza la Mawaziri. hii ni endapo baraza atakalolitangaza rais, majina hayo yatakuwemo. MWANAHALISI wanafanyakazi kwa kubahatishabahatisha tu, kutafuta sifa sifa tu kuwa ni wachunguzi.

LAKINI lengo hasa la MWANAHALISI kufanya hivi na kutaja mjina hayo 8 ni nini? Baraza la Magufuli lina Wizara 8 tu? mbona hawajataja baraza zima? hapa MWANAHALISI hawana jipya, malengo hapa ni mawili tu:
1. wana mambo yao binafsi na hayo majina manane(8) na kwa namna moja au nyingine kutaka kuonesha kuwa wanafaa kuwa kwenye baraza la Magufuli au hawafai.
2. wanataka tu kuionesha Serikali ya MAGUFULI ambaye anakenda na kasi ya ajabu katika utendaji wake kuwa ama iko makini au haiko makini. kwa kifupi ni kutaka tu kuikosoa kupitia ujumbe wake kwa wananchi.

TAFAKURI: MWANAHALISI wanapaswa kujitafakari kwa kina hususani katika kuwahabarisha wananchi. Hii serikali ya awamu ya Tano watanzania wana imani kubwa sana nayo na wako tayari kuiunga mkono kwa kila jambo linalolenga kuwaletea watanzani maendeleo. Propaganda za kijinga kama ambazo wanaanza kuzianzisha zimeshapitwa na wakati. Siyo muda tena wa kuwaaminisha watu mambo ambayo hayana tija kwa taifa.
MWANAHALISI wamuache RAIS AANDAYE BARAZA LAKE LA MAWAZIRI, Rais Magufuli siyo wa MAGAZETI wanajisumbua bure.

attachment.php
 

Attachments

  • IMG-20151207-WA0001.jpg
    IMG-20151207-WA0001.jpg
    32.9 KB · Views: 7,189
Yani wote walioandikwa na Mwanahalisi hawafai kuwa mawaziri kabisa... Eti Membe, Mwigulu, January, Migiro.... Hao wote ni mizigo tupu
 
Kubenea mhuni na tapeli hafai kwa lolote kazi yake ni kucheze akili za watu apuuzwe.
 
mwanahalisi hata ukinipa la bure sitaki, unafki wao wa kuniaminisha Lowassa ni fisadi na tamthilia zao za akina Jason Bourne zilinifanya niamini ni gazeti makini, ila niliyoyashuhudia baadaye halinifai even kwa kulikalia kwenye vumbi.
 
Hili gazeti toka lilipo kula matapishi yake nimekuwa nikilipuuza sana,kwangu mimi hili gazeti halina jipya.
 
Umeandika kana kwamba wote tumelisoma hilo gazeti la MwanaHalisi. Andika ueleweke Mkuu kwa kutaja hata hayo majina na kadhalika. Bure kabisa!
 
Wakati joto la kusubiri rais John Magufuli atangaze majina ya baraza lake la mawaziri likizidi kupanda, gazeti la Mwanahalisi limetoa baadhi ya majina yanayodaiwa kuvuja kutoka kwenye orodha hiyo.


Mmoja kati ya majina ambayo yamevuta usikivu wa wengi ni jina la aliyekuwa waziri wa mambo ya nje, Bernard Membe ambaye alikuwa mmoja kati ya wagombea wa CCM waliokuwa wanatajwa kuwa chaguo la rais mstaafu, Jakaya Kikwete.


Kwa mujibu wa gazeti la Mwana Halisi, majina mengine yanayotajwa ni pamoja na
January Makamba,
Dk. Asha Rose Migiro,
Ridhiwani Kikwete,
Peter Serukamba na
Mwigulu Nchemba.

Jina jingine lililotajwa kwenye orodha hiyo ni jina la aliyekuwa Makamo Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agostino (SAUT), Dk. Charles Kitima.

Dk. Kitima anadaiwa kuwa mmoja kati ya watu waliomuamini sana Dk. Magufuli wakati akiwa Waziri wa Ujenzi na hata kumualika kuwa mgeni rasmi kwenye mahafari ya chuo hicho.


NB: Majina haya ni kwa mujibu wa gazeti la Mwanahalisi ambalo limedai kuyapata baada ya kuvuja. Rais Bado hajatangaza baraza lake la mawaziri


Hata hivyo,Rais Magufuli anatarajiwa kutangaza baraza lake la mawaziri muda wowote kuanzia sasa.

Kwa mujibu wa katiba, rais anapaswa kutangaza baraza lake kabla ya kuanza kwa vikao vya bunge vya mwezi Januari.

source Mpekuzi blog
 
Mleta uzi hujajieleza vya kutosha, in short unang'ata hapa unaacha, put the record straight
 
Hahahahahhahahaaaa.....tulisema sisi hakuna jipyaaaaaaa...hahahahahhaaa...

Huyo mangoes yeye ni mambo ya nje nini?ahhahaha ccm buanaaa
 
Wakati joto la kusubiri rais John Magufuli atangaze majina ya baraza lake la mawaziri likizidi kupanda, gazeti la Mwanahalisi limetoa baadhi ya majina yanayodaiwa kuvuja kutoka kwenye orodha hiyo.


Mmoja kati ya majina ambayo yamevuta usikivu wa wengi ni jina la aliyekuwa waziri wa mambo ya nje, Bernard Membe ambaye alikuwa mmoja kati ya wagombea wa CCM waliokuwa wanatajwa kuwa chaguo la rais mstaafu, Jakaya Kikwete.


Kwa mujibu wa gazeti la Mwana Halisi, majina mengine yanayotajwa ni pamoja na
January Makamba,
Dk. Asha Rose Migiro,
Ridhiwani Kikwete,
Peter Serukamba na
Mwigulu Nchemba.

Jina jingine lililotajwa kwenye orodha hiyo ni jina la aliyekuwa Makamo Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agostino (SAUT), Dk. Charles Kitima.

Dk. Kitima anadaiwa kuwa mmoja kati ya watu waliomuamini sana Dk. Magufuli wakati akiwa Waziri wa Ujenzi na hata kumualika kuwa mgeni rasmi kwenye mahafari ya chuo hicho.


NB: Majina haya ni kwa mujibu wa gazeti la Mwanahalisi ambalo limedai kuyapata baada ya kuvuja. Rais Bado hajatangaza baraza lake la mawaziri


Hata hivyo,Rais Magufuli anatarajiwa kutangaza baraza lake la mawaziri muda wowote kuanzia sasa.

Kwa mujibu wa katiba, rais anapaswa kutangaza baraza lake kabla ya kuanza kwa vikao vya bunge vya mwezi Januari.

source Mpekuzi blog
Majigambo ya mtoto wa rahisi mstaafu yataongezeka maradufu kama nikweli
 
Back
Top Bottom