Gazeti la Jamhuri: Nyani walewale msitu tofauti

Hivi Balile, Manyerere na Kibanda hawawezi kuanzisha gazeti lao mpaka wafadhiliwe na Lowassa? Mbona ni Wahaririri wa siku nyingi na Waanzilishi wa Tanzania Daima?
 
u
Hivi Balile, Manyerere na Kibanda hawawezi kuanzisha gazeti lao mpaka wafadhiliwe na Lowassa? Mbona ni Wahaririri wa siku nyingi na Waanzilishi wa Tanzania Daima?
Kamura nakuunga mkono asilimia 100% kuwa hawa jamaa are old enough to stand on their own feet.

Kwa maoni yako tatizo liko kwenye mindset. Ukizoea vya kunyonga, vya kuchinja hawaviwezi. Wamezoea vya kupewa, vya kutafuta hawaviwezi.

Hawa wote watatu mimi nawaita ni ma comred katika fani tena wengine tunaitana ni 'makamanda' wakiwasimamia 'wapiganaji'.

Kuajiriwa sio jambo baya ni jambo jema, ila kuendelea kuajiriwa tuu ili kufanya jambo ambalo ungeliweza kwa kijiajiri mwentewe huu ni utunwa!.

Kama ni kweli makamanda hao wanakwenda kuanzisha gazeti la EL, then mimi nawaitwa ni watumwa wa pesa. Hii inanaana RA amekubali New Habari ife ili amuinue msharika wake EL.

Manyerere na Balile wanajua kusoma dalili za nyakati wameshajua baada ya kifo cha kisiasa cha RA, kifo rasmi New Habari hakiko mbali, na kwa vile wao ni watunwa wa kuajiriwa, mind set yao iko kwenye kutumika tuu sio kujituma, auamuzi wa kujump ship kabla jahazi lao halijazama ndio salama yao pekee kuendelea kuchumia tumbo!.

Wakati its a good move kwa Balile na Manyerere, kwa wao are good at puppeteering, its a mistake kwa Kibanda kwasababu Kibanda can be himself wakati puppets can never be themselves bali ni hufuata msimamo wa puppet master!.

Na kwa wasiomjua vizuri EL, nawashauri don't ever under estimate him. Abilities na capabilities zake zinafahamika, you just sit and watch.
 
kua watu wanaweza kukuchukia tu ata kama umetenda mengi mema na mabaya machache, cha msingi ukitaka kufanikisha malengo yako inabidi uwe ndani ya treni la chuma ambalo watalazimika kulipisha njiani
 
Kibanda is very smart kuungana na mchumia Tumbo Balile .Yaani Balile hana tofauti na Nape na FF haoa jamvini.Kibanda siamini kwamba naye anachumia tumbo .

Kama unamzungumzia Absalom Kibanda, Mhariri Mtendaji wa Tanzania Daima, basi yaelekea humjui vizuri. Nadhani unamanisha huyu ambaye pia ni mhariri mtendaji wa jarida la Umoja ambalo ofisi zake ziko kule Mikocheni ambako amelipiwa pango ya ofisi na kunuliwa fenicha na vifaa vya Ofisi na Lowassa ili aendeshe jarida hilo na hatimaye ligeuzwe kuwa gazeti na tool ya kampeni za huyo bwana Mkubwa. Nadhani unamzungumzia Kibanda ambaye alianza kazi za kumtakasa Lowassa kupitia gazeti hilo la Tanzania Daima siku nyingi na sasa inasemekana hata gharama za kuchapa gazeti zinatoka kwake (japo Kibanda anazitia mfukoni).

Ni dhahiri unamzungumizia Kibanda huyuhuyu ambaye Mbowe anamtafutia namna ya kumfukuza kwa sababu ya usaliti lakini hajapata namna muafaka. Ni huyu Kibanda ambaye sasa ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri.
 
kama manyerere naye ameingia kuupepea ufisadi wa EL basi nguvu ya pesa ni zaidi ya tsunami. huyu kijana alikuwa mzalendo safi, BASI TENA...echaro chafwaa!!!!

Unamzungumzia Manyerere wa mwaka gani? Maana Manyerere wa muongo mmoja sasa amekuwa ni Yuda Iskarioti kupita maelezo.
 
Ni kweli hilo gazeti la Jamhuri lipo
Karibu sana Balile,

Naona walau tunaweza kuelewa kilicho nyuma ya kuanzishwa kwa gazeti hili.

Do you have any clues? Alivyosema mkuu Kiranja kwenye post yake ya awali ni kweli? Unaionaje future ya tasnia ya habari Tanzania?
 
Wapendwa wanachama wa Jamii Forum salaam.

Kwanza naomba kutangaza kwa mara ya kwanza kuwa leo hii nimejiunga katika mtamdao huu. Miaka yote nimekuwa nikisoma postings kama wasomaji wengine napenda kuwapongeza waanzilishi wa mtandao huu wenye nafasi ya pekee katika jamii tunayoishi.

Kubwa lililonifanya nijiunge leo ni taarifa inayoendelea kujadiliwa humu ndani juu ya uanzishwaji wa gazeti la Jamhuri. Kwa kuwa siku zote mimi ni muwazi, nimeona ni vyema kwanza nisiingie humu kwa majina bandia, bali nitumie jina langu halisi. Pili, napenda kuwafahamisha wanajamii kuwa ni kweli tumeanzisha gazeti la Jamhuri. Ni kweli pia wakurugenzi wa kampuni iliyoanzisha gazeti hili; Jamhuri Media Limited ni Deodatus Balile, Manyerere Jackton, Absalom Kibanda na Mhariri mwingine ambaye jina lake nitalitaja siku za usoni.

Gazeti hili tunalimiliki sisi waandishi wanne asilimia 100. Nawahakikishia hakuna mkono wa mwanasiasa yoyote. Hawa wanaomtaja Edward Lowassa kuwa ndiye mmiliki, napenda kuwahakikishia kuwa wamekosea. Tunao uzoefu wa kutosha katika kuanzisha magazeti. Nimeshiriki kuanzisha gazeti la Mwananchi na Mwanaspoti mwaka 2000, nikashiriki kuanzisha gazeti la Tanzania Daima na Sayari, mwaka 2004. Hakika nilipata uzoefu wa kutosha katika taaluma hii.

Yapo mambo si msingi wa mada hii leo, kwamba kwa nini nilitoka Free Media Ltd, hapa sitayajadili lakini niliokwishazungumza nao kwa njia ya simu, hakika walinihurumia na kunipongeza kwa uamuzi niliouchukua. Kosa nililofanya mwaka 2004 la kuanzisha taasisi ya kitaaluma bila kuwa na maandishi ya kimkataba, lilikuwa fundisho kubwa na hili nimelizingatia katika kuanzisha Jamhuri Media Limited, kuwa si vyema katika biashara ya habari kama kweli una nia ya kuitumikia jamii, kushirikisha wanasiasa.

Wanasiasa kama raia wema, ni sehemu ya jamii hii. Sisi kama sisi hatuna mtaji. Wakati tunajiandaa kuanzisha na hatimaye kukopa benki, tumepata wasamaria ambao hawana masilahi ya kisiasa. Hatuko tayari kufanya kazi kwa mashinikizo ya kisiasa. Tutaitumikia jamii, kwa uadilifu mkubwa, ubunifu na kuweka mbele utaifa (kutetea rasilimali za nchi). Karibuni mtuunge mkono hata kwa kutuchangia sehemu ya mtaji (kifedha na hata kwa ushauri).

Ndugu zangu Watanzania, sisi tumefika mahala tumethubutu. Hakuna aliyezaliwa kuwa mmiliki wa vyombo vya habari, na wengine kuwa watumishi wake. Ikiwa kuna yeyote anatutilia shaka, kwa sasa tunaomba atupe nafasi. Kadri tutakavyochapisha nakala zetu, atatujuvya iwapo tupo kuchumia matumbo kama wanavyosema au la. Nawahakikishia mimi si mmoja wa wachumia tumbo.

Tuungeni mkono, tuliendeleze taifa letu kwa kukupeni habari sahihi bila mikingamo. Sisi kauli mbiu yetu ni kuwa TUNAANZIA WENGINE WANAPOISHIA.

Asanteni
 
Wapendwa wanachama wa Jamii Forum salaam.

Kwanza naomba kutangaza kwa mara ya kwanza kuwa leo hii nimejiunga katika mtamdao huu. Miaka yote nimekuwa nikisoma postings kama wasomaji wengine napenda kuwapongeza waanzilishi wa mtandao huu wenye nafasi ya pekee katika jamii tunayoishi.

Kubwa lililonifanya nijiunge leo ni taarifa inayoendelea kujadiliwa humu ndani juu ya uanzishwaji wa gazeti la Jamhuri. Kwa kuwa siku zote mimi ni muwazi, nimeona ni vyema kwanza nisiingie humu kwa majina bandia, bali nitumie jina langu halisi. Pili, napenda kuwafahamisha wanajamii kuwa ni kweli tumeanzisha gazeti la Jamhuri. Ni kweli pia wakurugenzi wa kampuni iliyoanzisha gazeti hili; Jamhuri Media Limited ni Deodatus Balile, Manyerere Jackton, Absalom Kibanda na Mhariri mwingine ambaye jina lake nitalitaja siku za usoni.

Gazeti hili tunalimiliki sisi waandishi wanne asilimia 100. Nawahakikishia hakuna mkono wa mwanasiasa yoyote. Hawa wanaomtaja Edward Lowassa kuwa ndiye mmiliki, napenda kuwahakikishia kuwa wamekosea. Tunao uzoefu wa kutosha katika kuanzisha magazeti. Nimeshiriki kuanzisha gazeti la Mwananchi na Mwanaspoti mwaka 2000, nikashiriki kuanzisha gazeti la Tanzania Daima na Sayari, mwaka 2004. Hakika nilipata uzoefu wa kutosha katika taaluma hii.

Yapo mambo si msingi wa mada hii leo, kwamba kwa nini nilitoka Free Media Ltd, hapa sitayajadili lakini niliokwishazungumza nao kwa njia ya simu, hakika walinihurumia na kunipongeza kwa uamuzi niliouchukua. Kosa nililofanya mwaka 2004 la kuanzisha taasisi ya kitaaluma bila kuwa na maandishi ya kimkataba, lilikuwa fundisho kubwa na hili nimelizingatia katika kuanzisha Jamhuri Media Limited, kuwa si vyema katika biashara ya habari kama kweli una nia ya kuitumikia jamii, kushirikisha wanasiasa.

Wanasiasa kama raia wema, ni sehemu ya jamii hii. Sisi kama sisi hatuna mtaji. Wakati tunajiandaa kuanzisha na hatimaye kukopa benki, tumepata wasamaria ambao hawana masilahi ya kisiasa. Hatuko tayari kufanya kazi kwa mashinikizo ya kisiasa. Tutaitumikia jamii, kwa uadilifu mkubwa, ubunifu na kuweka mbele utaifa (kutetea rasilimali za nchi). Karibuni mtuunge mkono hata kwa kutuchangia sehemu ya mtaji (kifedha na hata kwa ushauri).

Ndugu zangu Watanzania, sisi tumefika mahala tumethubutu. Hakuna aliyezaliwa kuwa mmiliki wa vyombo vya habari, na wengine kuwa watumishi wake. Ikiwa kuna yeyote anatutilia shaka, kwa sasa tunaomba atupe nafasi. Kadri tutakavyochapisha nakala zetu, atatujuvya iwapo tupo kuchumia matumbo kama wanavyosema au la. Nawahakikishia mimi si mmoja wa wachumia tumbo.

Tuungeni mkono, tuliendeleze taifa letu kwa kukupeni habari sahihi bila mikingamo. Sisi kauli mbiu yetu ni kuwa TUNAANZIA WENGINE WANAPOISHIA.

Asanteni

100% lies!!!! Uwongo uliokithiri! Balile, temea mate chini Ndugu yangu, umejiingiza kichwa kichwa humu ndani, utaumbuliwa sasa hivi.

Kamuulize Mtatiro alivyojiingiza kichwa kichwa humu JF juzi tu na akaondola nduki!
 
Lowasa jamani anajisumbua. Uwaziri mkuu ulimshinda atawezaje uprezidaa. Anajisumbua. Hakuna wa kumchagua. Asidhani waTZ ni wajinga kiasi hicho. Aachane na kigazeti hicho. Rais wa 2015 anajulikana naye ni Dr.S......LA.

Huyo S....LA akagombee urais karatu sio tz.Ni mwaka wa vijana 2015 vikongwe hatuwataki magogoni.Jamani we need rais kijana kama Benard Membe.
 
Ni ukweli usiopingika kwamba EL hafikiriwi na wengi wala hapendwi na wengi, ila nadhani tunachotakiwa kuelewa hapa ni kwamba huyu EL ana imani kubwa kwamba ana uwezo mkubwa wa kupenyeza na kwenda Magogoni bila wasiwasi 2015.


Mkitaka kujua nguvu ya EL angalieni sakata zote zinazomhusu zilikoishia, hakuna hata moja iliyoenda popote na sasa ndio hivi tunaambiwa Mwakyembe kakimbizwa India baada ya Mwandosya kuwa huko kwa muda mrefu tuu. Mwakyembe alitoa taarifa kuhusu mipango ya kuwamaliza siku nyingi na ilidhihirisha wazi kwamba kundi la EL linahusika na ushahidi wa magari yao na makampuni yao wakisaidiwa na dola yenyewe uliwekwa wazi. Kuna ushahidi wa kutosha kuhusu ushawishi wa EL kwa NEC, ma-DC, ma-RC na madaraja mengine mengi... zaidi sana JK mwenyewe ni swahiba mkubwa kwa siri wakiendelea kula nchi hii bila wasiwasi. Pesa aliyonayo huyu jamaa kwa sasa anaamini anaweza kumnunua Mtanzania yeyote mwenye kelele mbele yake, ingawa si kweli lakini cha msingi hapa ni kwamba yeye anaamini hivyo na tukae tukijua kwamba ataitumia hiyo pesa kufanya lolote analoona litamsafishia njia kuelekea Magogoni.

Tutafakari ukweli kwamba hali ngumu tuliyonayo sasa hivi inachangiwa sana na pesa nyingi iliyotumika kumweka JK madarakani 2010, lakini kutokana na ukweli kwamba 2015 inaonekana kuwa ngumu... CCM wameshaanza tena mikakati ya ukusanyaji wa fedha za kutumia 2015. Ni pesa nyingi sana inahitajika na CCM 2015 na itakuwa ngumu kuikusanya kwa haraka, kwahiyo tusitarajie unafuu wowote haswa ikizingatiwa kutokea kwa chaguzi zingine zisizotarajiwa kama za Igunga na nyinginezo ambazo hatujui ujio wake kabla ya 2015.

Kama ikitokea Mungu akafumba macho ili EL achukue nchi (kwa lengo ambalo Mungu analijua mwenyewe), naamini pesa ambayo itatumika ili EL atinge Magogoni itakuwa mara 3 ya matarajio ya matumizi ya CCM kwa hiyo 2015. Ili kuzirudisha hizo pesa ikiwemo faida ya kukaa Magogoni itabidi Watanzania tuuzwe na tutanadiwa bila hata kusema chochote. Tukae tukielewa wazi kwamba EL ni mbabe kuliko hata Mkapa, kama Mkapa alifunga watu fulani fulani midomo basi EL atawazima kabisa.

Hizi za akina Mwakyembe na Mwandosya zitakuwa ni issue ndogo sana iwapo EL atakuwa hapo Magogoni. Kwa kifupi kama jamaa ataingia madarakani kuna watu itawabidi wakimbie kabisa nchi hii hadi EL atakapoiaga hii dunia ya Mwenyenzi Mungu, nitamuomba Mungu asiwe kama Gadaffi maana akiwa hivyo atawafuata hata huko waliko na atawamalizia mbali kama Mungu mwenyewe hatozuia hayo kutokea. Hatumwogopi lakini EL si mtu wa kumfikiria kwa haraka na kuondoka, ni mtu wa kumtafakari kwa umakini kabla ya kujua nini kifuate baada ya hicho ulichokiona.
 
Kubwa lililonifanya nijiunge leo ni taarifa inayoendelea kujadiliwa humu ndani juu ya uanzishwaji wa gazeti la Jamhuri. Kwa kuwa siku zote mimi ni muwazi, nimeona ni vyema kwanza nisiingie humu kwa majina bandia, bali nitumie jina langu halisi. Pili, napenda kuwafahamisha wanajamii kuwa ni kweli tumeanzisha gazeti la Jamhuri. Ni kweli pia wakurugenzi wa kampuni iliyoanzisha gazeti hili; Jamhuri Media Limited ni Deodatus Balile, Manyerere Jackton, Absalom Kibanda na Mhariri mwingine ambaye jina lake nitalitaja siku za usoni.

Bora umejitokeza, na wenzako waje. Hasa huyo uliyemficha. Ninaamini huyo ndo ngao yenu ili muonekane credible kumbe yale yale. Mtaje tu naye tunamjua in and out.
 
Taarifa ni kuwa Lowasa katika mkakati wa urais wa 2015 anaanzisha magazeti 5 kwa mpigo ili kufanya kampeini kuanzia sasa.

Gazeti la kwanza litaanza kuchapishwa wiki ijayo Linaitwa
Jamhuri litakuwa chini ya Deodatus Balile na waandishi wengine akiwemo Manyerere nk.Litaaanza likiwa linatoka kila wiki.

Chanzo ni mimi mwenyewe, niko jikoni.
 
Back
Top Bottom