Gari ya mikosi, njooni mnisaidie

Gari ya mikosi, njooni mnisaidie

co fm

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2016
Posts
1,569
Reaction score
2,584
Habari wadau? Kuna notion kwamba unaweza kununua gari kwa mtu yaani second hand inaweza kuwa imebeba laana au mikosi au mabalaa. Ipo hivi mwaka huu nimenunua gari ni kama mwenye gari yeye hajatembelea sana ila cha kushanganza toka ninunue hii gari nilishapata nayo ajali like 4 times.

Ajali ya kwanza nikugonga chombo tena kina mtu, ajali ya pili bajaj kunikwaruza ajali ya tatu mtu mwenye gari kunigonga ajali ya nne just tu gari imekosa control na kugonga.

Nimewahi kuwa na gari ila hii naona mpya. Je ninaweza kutestify vipi hiyo gari ndo yenye majanga au mtu aliyeniuzia ndo kaweka kinyongo.
 
chek machanical issue za gar pia na ustad wako wa uendeshaj uboreshe chombo hakina shida
 
kuwa makini barabarani ukiwa waruwaru hata iwe odometer isome 0 baada ya muda utaishangaa imechoka
 
Mkuu umenunua gari na pesa zako za mwisho uliokuwa nazo, unatembea na kidumu, taa nyekundu inawaka, nyumbani umeacha unga na sukari robo na unadaiwa na washkaji. Hakuna laana Wala mikosi hapo ni mawenge na mawazo yako. Nakushauri paki gari hadi utakapokuwa sawa.
 
kuwa makini barabarani ukiwa waruwaru hata iwe odometer isome 0 baada ya muda utaishangaa

Mkuu umenunua gari na pesa zako za mwisho uliokuwa nazo, unatembea na kidumu, taa nyekundu inawaka, nyumbani umeacha unga na sukari robo na unadaiwa na washkaji. Hakuna laana Wala mikosi hapo ni mawenge na mawazo yako. Nakushauri paki gari hadi utakapokuwa sawa.
Wapi nimesema taa nyekundu inawaka? Hujasoma vizuri uzi wangu.
 
Au unaendesha ukiwa umelewa? Pole usiwazie vitu vibaya ni majanga tu yanatokea, omba Mungu pia.
 
Back
Top Bottom