Gari “Namba D” zimeenda wapi?

Gari “Namba D” zimeenda wapi?

Mimi kwangu gari si plate namba sababu mimi sio dalali kwamba nanunua gari ili niuze , mimi gari i kwa matumizi yangu hivyo hata gari ikiwa namba T 101 AAA ili mradi tu board yake imenyooka iko vizuri nachukua, maana nina kigari cha field nilikichukua kwa padre mmoja hapa Rav 4 old nambaT 1** A** aisee gari ilikuwa bado mpya kabisa kuanzia board hadi engine ,naipenda kuliko nyingine nilizo nazo, na huwa na kuwa na uhakik wa safari nikiwa na hii Rav 4 kuliko hilo lingine la kisasa ambalo umeme kila sehemu
Plate number sio ubora wa gari, mana unakutana gari no. E au D iko garage wanafanya ukarabati wa Engine au gear box. Aidha, gari ni matunzo but likely old car inaweza kua na changamoto zaidi kuliko mpya.
Mimi pia ni Mzee wa T 3 .... A.... hilux ln166 imekula vumbi la mererani na vumbi la Mpwapwa na hakuna shida kabisa plus safari za Arusha - Dodoma za kutosha.
 
Back
Top Bottom