Wadau mambo niaje,
ebhana jamani mwenzenu nimeingizwa cha kike, nimenunua Galaxy s5 nikadhani original maana njia zote za kutest simu original nilifanya na iyo simu ikakubali ndipo nikainunua kwa mihela mingi tu...Ila nilipoenda kuitumia ndo nikagundua ni tofauti na galaxy s5 original, maana niliangalia features za original kwenye youtube nikagundua ya kwangu haina features za namna iyo..ndipo nikaangalia kwenye mitandao nikaona kuna galaxy s5 model kama yangu ( G 9006V ) wanaizungumzia wenyewe wanasema sijui ni clone ya s5, daah imeniuma sana wadau.
NATAFUTA MTU kama anaitaka anirudishie hata nusu ya ela yangu tu..maana sijazoea kutumia fake na pia stimu zote za kuitumia hii simu zimekata.