CUF Habari
JF-Expert Member
- Dec 12, 2019
- 239
- 234
FURAHA NA HAKI SAWA KWA WOTE
Waasisi wa The Civic United Front(CUF-Chama Cha Wananchi) walikutana katika Ukumbi wa Starlight Hotel, Mjini Dar es Salaam tarehe 20-21 Novemba 1992 walitoa Tamko ambalo ni Utangulizi wa Katiba ya Chama Chetu. Katika Tamko hilo walieleza kuwa:-
"Sisi Watanzania tuliokutana Dar es Salaam kwa muda wa siku mbili, tarehe 20-21 Novemba 1992 tunaamini kuwa Haki za Binadamu na Haki za Watu, kama zilivyotangazwa katika Tangazo la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa , na HATI ya Umoja wa Nchi Huru za Afrika juu ya Haki za Binadamu na Haki za Watu , ndiyo msingi wa Sheria na Kanuni zinazotakiwa kuongoza nchi....
Tumeamua kuunda Chama hiki, THE CIVIC UNITED FRONT(CUF-Chama Cha Wananchi), kwa nia ya kuwaunganisha watu wa Tanzania wenye kuamini kwa dhati juu ya kuwepo kwa demokrasia ya kweli ambapo wananchi wenyewe ndio wenye mamlaka, madaraka na uamuzi wa mwisho kuhusu mambo yao na nchi yao.
Tumechukua uamuzi huo wa kihistoria ili kutekeleza Imani yetu juu ya Haki za Binadamu na Haki za Watu, kwa kutumia itikadi, au falsafa yetu mpya itakayojulikana kwa jina la UTAJIRISHO, yenye Maana pana ya Haki Sawa kwa Wote na Neema kwa Wote.
ITIKADI YETU NI UTAJIRISHO
Waasisi wa The Civic United Front(CUF-Chama Cha Wananchi) walikutana katika Ukumbi wa Starlight Hotel, Mjini Dar es Salaam tarehe 20-21 Novemba 1992 walitoa Tamko ambalo ni Utangulizi wa Katiba ya Chama Chetu. Katika Tamko hilo walieleza kuwa:-
"Sisi Watanzania tuliokutana Dar es Salaam kwa muda wa siku mbili, tarehe 20-21 Novemba 1992 tunaamini kuwa Haki za Binadamu na Haki za Watu, kama zilivyotangazwa katika Tangazo la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa , na HATI ya Umoja wa Nchi Huru za Afrika juu ya Haki za Binadamu na Haki za Watu , ndiyo msingi wa Sheria na Kanuni zinazotakiwa kuongoza nchi....
Tumeamua kuunda Chama hiki, THE CIVIC UNITED FRONT(CUF-Chama Cha Wananchi), kwa nia ya kuwaunganisha watu wa Tanzania wenye kuamini kwa dhati juu ya kuwepo kwa demokrasia ya kweli ambapo wananchi wenyewe ndio wenye mamlaka, madaraka na uamuzi wa mwisho kuhusu mambo yao na nchi yao.
Tumechukua uamuzi huo wa kihistoria ili kutekeleza Imani yetu juu ya Haki za Binadamu na Haki za Watu, kwa kutumia itikadi, au falsafa yetu mpya itakayojulikana kwa jina la UTAJIRISHO, yenye Maana pana ya Haki Sawa kwa Wote na Neema kwa Wote.
ITIKADI YETU NI UTAJIRISHO