Kweli Waliosema Njaa Mwanaharamu, hawakukosea. Si huyu huyu Nape aliyejigeuza vuvuzela na kupita kila kona na kuwatuhumu wale wote waliohusika na wizi wa EPA na kuwaita Majina! Si huyu huyu Nape aliyetaka Mafisadi wote waondoke ndani ya CCM na kuwaita ni Magamba na wanakichafua Chama!
Si huyu huyu Nape aliyekuja na Siku 90 za kukisafisha Chama kwa kuwaondoa Mafisadi ambao wengine walibatizwa jina la "Mapacha Watatu" Si huyu huyu Nape aliyepinga kwa nguvu zote Ufisadi uliopelekea Jengo la Umoja wa Vijana wa Magamba kukodishiwa Mtu kwa Bei ya Kutupa hata ikampelekea kukorofishana na Lowasa na hatimaye, Pamoja na Wenzake kuanzisha kwa Siri Chama cha Siasa cha CCJ!
Inamaana Leo hii Nape amesahau kwamba Jeetu Patel ni Miongoni mwa Mafisadi wakubwa ambao ndio waliopelekea hata yeye kutaka wale walioshirikishwa naye kwenye Wizi wa pesa za EPA wafukuzwe chamani!
Kinasaba, tunajua kabisa kwamba Nape hana Undugu wowote, au wa damu au wa kurithishwa na Jeetu Patel. Leo hii iweje Nape aibuke na kumwita Mtu aliyetupa mateso Watanzania "Baba"!
Ama kweli Penye udhia, Penyeza Rupia. Baada ya kulishwa vipande thelasini leo hii Nape Unakuwa Mtetezi mpaka wa Mafisadi na kutusaliti nduguzo kweli!
Nape amenikatisha tamaa zaidi ya alivyonikatisha toka mapema. Sintoshangaa siku nikimsikia Nape akimwita Rostam, Mjomba'ke, na Lowasa na Chenge Baba walezi.
Wonders shall never end.