Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,627
- 154,988
Kama Ye anatamka jina la Yesu katika kipindi kigumu zaidi cha maisha yake jua kuwa jina la Yesu lina nguvu kubwa zaidi kuliko kitu kingine chochote kile ulimwenguni. Lakini je, kwa kutamka jina la Yesu, Ye ana akili au hana?
Ye aliwahi kuutangazia umma kuwa alishauza nafsi yake kwa Shetani, kwa ajili ya pesa na umaarufu, mpaka mama yake akatolewa kafara, ili ajenda za wakubwa wa dunia hii zisonge mbele.
Mtu aliyeuza nafsi yake kwa Shetani anawezaje tena kusamehewa na Mungu? Anawezaje tena kumkimbia Shetani bwana wake mpya? Anawezaje tena kulitaja jina la Yesu, wakati katika mkataba wake na Wakubwa alikatazwa katakata kulitaja jina hilo?
Ajenda za wakubwa lazima zisonge mbele, na zinasonga mbele kwa vitisho na ukatili wa hali ya juu. Ukishasaini mkataba kuzilinda ajenda hizo, unaiweka familia yako rehani, na unakuwa mtumwa kamili wa wakubwa wa dunia hii.
Mathalani: Ye ana watoto wanne aliozaa na Kim Kardashian, mlimbwende wa Marekani. Kama Ye amekwenda kinyume na ajenda za wakubwa, hadi wakubwa hao kuanza kumpiga vita, kwa nini watoto wake bado hawajatolewa kafara hadi leo hii? Naam, watoto wa Ye hawawezi kutolewa kafara kwa sababu ya mama yao, Kim Kardashian! Nafasi ya Kim kwa Wakubwa ni sawa na ya Ye. Wakubwa wanamheshimu Kim kama wanavyomheshimu Ye. Kwa hiyo, inawezekana kabisa kwamba kuna mchezo fulani unachezwa hapo.
Lengo la kutoa kafara kwa wakubwa wa dunia hii si damu. Hawana shida na damu. Wakiitaka wanaweza kuipata popote! Lengo la kutoa kafara ni kuhakikisha msanii haendi nje ya ajenda za kidunia, ukiwemo Mpango Mpya wa Dunia au "New World Order".
Katika kitabu cha Thomas R. Horn wa Marekani kiitwacho "Zeigeist", serikali ya Mpango Mpya wa Dunia ("New World Order") itaanza rasmi kutawala dunia mnamo mwaka 2025. Je, inawezekana Ye anatayarishwa kwa ajili ya mpango huo? Je, inawezekana Ye anatayarishwa kuwa Rais wa Marekani?
Unapoona senema kama hizi za akina Ye na washirika wake zikichezwa hadharani, jambo la hekima unalopaswa kufanya ni kuamka kutoka usingizini na kuwa na akili.
Wewe ni mtoto wa Mfalme. Hakuna mfalme kama Baba yako! Jilimbilikizie imani katika kipindi hiki cha amani, ili amani itakapopotea ubaki na imani.
Mdanganyifu hudanganya wanaopenda kudanganywa.
—Enock Maregesi, mwandishi wa vitabu
Ye aliwahi kuutangazia umma kuwa alishauza nafsi yake kwa Shetani, kwa ajili ya pesa na umaarufu, mpaka mama yake akatolewa kafara, ili ajenda za wakubwa wa dunia hii zisonge mbele.
Mtu aliyeuza nafsi yake kwa Shetani anawezaje tena kusamehewa na Mungu? Anawezaje tena kumkimbia Shetani bwana wake mpya? Anawezaje tena kulitaja jina la Yesu, wakati katika mkataba wake na Wakubwa alikatazwa katakata kulitaja jina hilo?
Ajenda za wakubwa lazima zisonge mbele, na zinasonga mbele kwa vitisho na ukatili wa hali ya juu. Ukishasaini mkataba kuzilinda ajenda hizo, unaiweka familia yako rehani, na unakuwa mtumwa kamili wa wakubwa wa dunia hii.
Mathalani: Ye ana watoto wanne aliozaa na Kim Kardashian, mlimbwende wa Marekani. Kama Ye amekwenda kinyume na ajenda za wakubwa, hadi wakubwa hao kuanza kumpiga vita, kwa nini watoto wake bado hawajatolewa kafara hadi leo hii? Naam, watoto wa Ye hawawezi kutolewa kafara kwa sababu ya mama yao, Kim Kardashian! Nafasi ya Kim kwa Wakubwa ni sawa na ya Ye. Wakubwa wanamheshimu Kim kama wanavyomheshimu Ye. Kwa hiyo, inawezekana kabisa kwamba kuna mchezo fulani unachezwa hapo.
Lengo la kutoa kafara kwa wakubwa wa dunia hii si damu. Hawana shida na damu. Wakiitaka wanaweza kuipata popote! Lengo la kutoa kafara ni kuhakikisha msanii haendi nje ya ajenda za kidunia, ukiwemo Mpango Mpya wa Dunia au "New World Order".
Katika kitabu cha Thomas R. Horn wa Marekani kiitwacho "Zeigeist", serikali ya Mpango Mpya wa Dunia ("New World Order") itaanza rasmi kutawala dunia mnamo mwaka 2025. Je, inawezekana Ye anatayarishwa kwa ajili ya mpango huo? Je, inawezekana Ye anatayarishwa kuwa Rais wa Marekani?
Unapoona senema kama hizi za akina Ye na washirika wake zikichezwa hadharani, jambo la hekima unalopaswa kufanya ni kuamka kutoka usingizini na kuwa na akili.
Wewe ni mtoto wa Mfalme. Hakuna mfalme kama Baba yako! Jilimbilikizie imani katika kipindi hiki cha amani, ili amani itakapopotea ubaki na imani.
Mdanganyifu hudanganya wanaopenda kudanganywa.
—Enock Maregesi, mwandishi wa vitabu