Bwana acheni ushabiki maandazi, hakuna timu duniani imewahi kuwa kwenye form siku zote na haitakaa itokee asilani.Me nakanusha unavyosema kuwa wanaolalamika ni mashabiki maandazi
Kwa mfano hizo timu ulizozitaja Liverpool,Chelsea na nyinginezo zote mashabiki wake kindakindaki wanalalamika
Njoo uchukue mfano halisi jinsi mashabiki wa Manchester United wanavyopiga kelele glazer waachie timu yao hiko ndicho kinatokea kwa Simba mashabiki wanaona kuwa uongozi ndiyo kiini cha matatizo Kwahiyo wanataka ubadilishwe
Kwahiyo ni jambo la kawaida mashabiki kupiga kelel duniani kote
Eti mnashangaa leo Simba haifanyi vizuri hata hamfahamu kwamba hii Simba kwenye miaka ya themanini ilikuwa kabisa inashuka daraja kwenye ligi hadi ikaokolewa na Yanga tena sio mara moja lakini mbona ilitoka hapo na kuzinduka.
Acheni ushamba nyie vijana.