Freemasonry Wametushika kila kona

Freemasonry Wametushika kila kona

Tafadhali kama una msimamo mkali wa dini ishia hapa usiendelee kusoma.

Nilikuwa kijiweni muda mfupi uliopita nacheza mchezo wa Draft. Kaja jamaa mmoja baada ya salamu jamaa mungine akauliza muda ili awahi kuondoka, akajibiwa kwamba ni saa moja na robo.
Sasa shida ikaanza kwa yule mgeni wetu, akatuuliza munawajua Freemasons? Nikajibu nawasikia kwamba ni mtandao wa matajiri wakubwa duniani. Jamaa akanicheka akasema umepotea kaka, hao ni waabudu shetani na wametushika kila kona. Nikambishia nikasema si kweli. Ndipo akaja na somo la saa au mfumo wa kusoma saa.

Akaanza kwa kuuliza sasa ni saa ngapi? nikamjibu saa moja. Akaniuliza hapo kwenye saa yako imeandikwa ngapi? Nikamjibu saba. Akasema emheeee hapahapo ndipo wametushika. Akauliza munajua kwa nini saa moja iandikwe saba? Nikajibu sijui. Akauliza munajua 666 alama ya mpinga kristo? Nikamjibu nasikiaga. Ndo sasa akaanza hesabu zake kama ifuatavyo.

1. Saa moja inaandikwa saba: 7-1= 6
2. Saa mbili inaandikwa nane: 8-2= 6
3. Saa tatu „ Tisa: 9-3= 6
4. Saa nne „ kumi: 10-4=6
5. Saa tano „ 11: 11-5 =6
6. Saa sita „ 12: 12-6= 6
7. Saa saba „ 13: 13-7=6
8. Saa nane „ 14: 14-8=6
9. Saa tisa „ 15: 15-9= 6
10. Saa kumi „ 16: 16-10=6
11. Saa kumi na moja „ 17: 17-11=6
12. Saa kumi na mbili „ 18: 18-12=6
Hapo akauliza mumenisoma? Wote tukajibu ndio mzeee.
Akasema kwa masaa 12 mengine Freemason wamefanya kama ifuatavyo.
1. Saa moja inaandikwa 19: 19-1=18=6+6+6
2. Saa mbili „ 20: 20-2=18=6+6+6
3. Saa tatu „ 21: 21-3=18=6+6+6
4. Saa nne „ 22: 22-4= 18=6+6+6
5. Saa tano. „ 23: 23-5= 18=6+6+6
6. Saa sita „ 24: 24-6= 18= 6+6+6
Hivyo kuanzia saa saba usiku inarudia tena kama hapo juu kabisa kuanzia namba 1-6. Hivyo tukabaki kimyaaa. Akasema ndo maana yeye hatumii mfumo wa 24hrs anatumia 12hrs system.

Sasa niwaulize wanajamvi kuna ukweli wowote hapa? Je nikweli Freemasons walivuruga saa makusudi? Je kuna ubaya kutumia 24hrs system?.

Ni kweli wamevuruga wao ....kuna cku jmaa mmoja alielezea clouds tv
lkn kwa kingereza
 
An idle mind is a workshop of the devil.... Huu upuuzi unaweza ukawa umeanzishwa na mtu mmoja anayejiita mkristu, licha ya wajibu wa kujenga ufalme wa Mungu ('ufalme wako ufike') yeye yuko busy kujenga ufalme wa giza..'

ishikilie sana elimu kristu anataka wagonjwa mleta thread kasikia mimi wananiandama day to day,hujielewi maisha ni vita ya kiroho utawaelewa tu ni roho gani
 
Wanajamvi matusi yanini. Tuelimishane kuhusu hawa Freemasons matusi hayatasaidia kitu.
 
wasabato......

ufunuo 13:18,"Hapa ndipo penye hekima.Yeye aliye na akili,na aihesabu hesabu ya mnyama huyo,maana ni hesabu ya kibinadamu.Na hesabu yake ni mia sita.sitini na sita."hii habari ya 666 imeandikwa kwenye biblia.Kwa hiyo maana ya kauli yako ni kwamba wasabato ndio wanaoijua vizuri biblia,sivyo?au biblia ni kitabu cha wasabato tu?hilo fungu limezungumza jambo moja zito msilolijua,si wote watakaojua mambo haya,bali ni wale wenye "akili" ya kuielewa "hekima" inayozunguka elimu hii.kama huna hiyo "akili" hata ufundishwe vipi "hekima" hii hautaelewa.sasa nadhani ndugu yangu utaitafsiri vizuri kauli yako kwa mapana yake.
 
ufunuo 13:18,"Hapa ndipo penye hekima.Yeye aliye na akili,na aihesabu hesabu ya mnyama huyo,maana ni hesabu ya kibinadamu.Na hesabu yake ni mia sita.sitini na sita."hii habari ya 666 imeandikwa kwenye biblia.Kwa hiyo maana ya kauli yako ni kwamba wasabato ndio wanaoijua vizuri biblia,sivyo?au biblia ni kitabu cha wasabato tu?hilo fungu limezungumza jambo moja zito msilolijua,si wote watakaojua mambo haya,bali ni wale wenye "akili" ya kuielewa "hekima" inayozunguka elimu hii.kama huna hiyo "akili" hata ufundishwe vipi "hekima" hii hautaelewa.sasa nadhani ndugu yangu utaitafsiri vizuri kauli yako kwa mapana yake.

sijui nikupe zawadi gani
666 ni utawala wa dunia ya sasa BIBLIA NI NGUZO YA KUSHIKILIA

TAFAKARI
 
Mkuu hapo jamaa kuna uhuni anafanya na hizo namba anazikorogakoroga anapata hiyo 666. Lengo kutuvuruga tu. Nilijaribu kubishananae lakini alinishinda kwasababu yeye anaongea na data zake na alijipanga wakati mimi nilikuwa sina data na sikujiandaa.

Umeona uje utuvuruge na sisi?Yaani hawa Freemason akiyanani nahisi wameshachoka sasa maana kila kitu ni chao!Diamond kufanikiwa kimuziki ni freemason, kifo cha Kanumba Freemason khaaaa!
 
Umeona uje utuvuruge na sisi?Yaani hawa Freemason akiyanani nahisi wameshachoka sasa maana kila kitu ni chao!Diamond kufanikiwa kimuziki ni freemason, kifo cha Kanumba Freemason khaaaa!

Freemason ni nini!?tuanzie hapa
 
Freemason ni nini!?tuanzie hapa

Dahh, we mbona mzito kuelewa hivyoo?Umeambiwa kule Jamii Intelligence kuna thread inayozungumzia kila kitu kuhusu Freemason, sa unaniuliza mi mwalimu wako?We vipi?
 
Kinanachonishangaza kuhusu huu uvumi wa 666 ni kuona watu wanakua na uoga usio na msingi. Miaka yote mtu uliyoishi mfano kama kweli hiyo 666 ina exist imekupunguzia au kukuongezea nini? The fear of the unknown ni kitu mbaya sana.
 
Dahh, we mbona mzito kuelewa hivyoo?Umeambiwa kule Jamii Intelligence kuna thread inayozungumzia kila kitu kuhusu Freemason, sa unaniuliza mi mwalimu wako?We vipi?

kila kitu?

nimembiwa au imeandikwa?

umetumia kipimo gani kujua mi simwelewa?

huwezi kuwa mwalimu


hujui hata nipo vipi au nalenga picha ipi?

unawajua FREEMASONS?

Unajua dunia upo kufanya nini?

NASIKITIKA SANA KWA UPEO WAKO
 
Kinanachonishangaza kuhusu huu uvumi wa 666 ni kuona watu wanakua na uoga usio na msingi. Miaka yote mtu uliyoishi mfano kama kweli hiyo 666 ina exist imekupunguzia au kukuongezea nini? The fear of the unknown ni kitu mbaya sana.

Dunia ni mahali pa kufanya nini?:

kwanini ivume???
 
ufunuo 13:18,"Hapa ndipo penye hekima.Yeye aliye na akili,na aihesabu hesabu ya mnyama huyo,maana ni hesabu ya kibinadamu.Na hesabu yake ni mia sita.sitini na sita."hii habari ya 666 imeandikwa kwenye biblia.Kwa hiyo maana ya kauli yako ni kwamba wasabato ndio wanaoijua vizuri biblia,sivyo?au biblia ni kitabu cha wasabato tu?hilo fungu limezungumza jambo moja zito msilolijua,si wote watakaojua mambo haya,bali ni wale wenye "akili" ya kuielewa "hekima" inayozunguka elimu hii.kama huna hiyo "akili" hata ufundishwe vipi "hekima" hii hautaelewa.sasa nadhani ndugu yangu utaitafsiri vizuri kauli yako kwa mapana yake.

Vipi unafahamu "Great Disappointment".......Unajua ni kina nani waliosababisha....???

Mama Hellena na wenzake kina Miller unawafahamu . ..?Are SDA Christians...???
 
akili yako inapimwa na nani?na nini?wapi?kipimo kipi?

AKILI NI NINI?

Tuanzie hapa

Sihitaji akili yangu ipimwe na mtu yeyote....!!!

Unadhani akili za Wasabato zilivyo shikiliwa na mwana mama Hellena White wako sawa...!!!??
 
Freemason ni nini!?tuanzie hapa

Na wewe ni zuzu tuu....Unajifanya "Tuanzie hapa" lakini ni mtupu kwenye kichwa chako....

Hivi kwanini Wasabato wanapenda habari za Freemason...??? Hivi na wewe ni Msabato Masalia(Mjukuu wa mama Hellena Mweupe)..?
 
Back
Top Bottom