Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 16,818
- 62,029
Ndugu Freeman Mbowe, kumbuka kwa miaka takriban 20 ulikuwa kwenye familia inayokupenda, kukuheshimu na hata wengine kuwa tayari kuyatoa maisha yao kwa ajili yako na uongozi wako.
Ulipotuhumiwa kwa makosa mabaya kabisa ya kuuza madawa ya kulevya na Ugaidi ni wanachadema waliopambana kukutetea na kuilinda heshima yako. Tafadhali kumbuka wema huu na imani hii. Siyo serikali ya CCM.iliyokusafisha mbele ya umma bali ni wanachadema na umma uliosimama kulinda heshima yako.
Ulipokuwa Jela ni Wanachadema waliosimama na KUSEMA WEWE SIYO GAIDI, Serikali ya awamu ya Tano iliposema kuwa wewe unauza Ngada ni Wanachadema waliosema hatukubaliani na tuhuma hizo.
Sasa Ndugu Mbowe kweli unaweza kuwaangusha watu wa aina hii?
Tafakari sana.
Hapa Chini naweka video wanachadema wakisali kumlilia Mungu akuokoe na kesi ya Ugaidi. Jiulize wakati huu Samia alikuwa wapi?
View: https://youtu.be/fJf-65LEICk?si=9yYYuLmi6PuHlf3P
Ulipotuhumiwa kwa makosa mabaya kabisa ya kuuza madawa ya kulevya na Ugaidi ni wanachadema waliopambana kukutetea na kuilinda heshima yako. Tafadhali kumbuka wema huu na imani hii. Siyo serikali ya CCM.iliyokusafisha mbele ya umma bali ni wanachadema na umma uliosimama kulinda heshima yako.
Ulipokuwa Jela ni Wanachadema waliosimama na KUSEMA WEWE SIYO GAIDI, Serikali ya awamu ya Tano iliposema kuwa wewe unauza Ngada ni Wanachadema waliosema hatukubaliani na tuhuma hizo.
Sasa Ndugu Mbowe kweli unaweza kuwaangusha watu wa aina hii?
Tafakari sana.
Hapa Chini naweka video wanachadema wakisali kumlilia Mungu akuokoe na kesi ya Ugaidi. Jiulize wakati huu Samia alikuwa wapi?
View: https://youtu.be/fJf-65LEICk?si=9yYYuLmi6PuHlf3P