Freeman Mbowe akabidhiwa fomu za kugombea uenyekiti CHADEMA Taifa

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
1781998_281214708736026_1532175360790364052_n.jpg

10580106_281172308740266_4070475535305422720_n.jpg


WanaJF

Karibuni katika tukio la kihistoria la kumuomba na kumkabidhi fomu za kugombea Uenyekiti wa Chadema Taifa shujaa na mpambanaji asiyechoka Kamanda Freeman Aikael Mbowe.

Tukio hili linafanyika katika hoteli ya Protea Upanga jijini DSM.Itakumbukwa wazee kutoka sehemu mbalimbali nchini wameunganisha nguvu kumuomba Kamanda Mbowe kugombea nafasi hii.

Mpaka siku ya leo Kiongozi huyu anayejivunia mafanikio lukuki ndani ya Chadema alikuwa hajatangaza rasmi kama atatetea nafasi yake.Hali hii imewatia kiwewe wanachama kote nchini.

Updates...1

Mwenye shughuri ni mzee athumani yassini mzigo mapigo saba kutoka kigoma.

Kutakuwa na statement ya wazee wa Pwani walio amua kumsindikiza na kudhamini fomu ya mwenyekiti

Aidha kutakuwa na tamko la bawacha na tamko la vyuo vikuu kutoka kwa mwenyekiti Gango Kidela

Waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari wameshafika ukumbuni kushuhudia tukio hili ili kuwajuza watanzania nchini kote.

Updates 2..

Kamanda wa Anga Shujaa Mpambanaji asiyechoka Freeman Mbowe anawasili hapa ukumbini.Ni shamrashamra kubwa sana zinatawala hapa ukumbini.Hakika ni hoihoi na nderemo kutoka kwa wazee na umati mkubwa wa wanachama uliofika hapa.

Itakumbukwa historia fupi ya Mzee Athumani mapigo saba ana miaka 20 ndani ya chadema

Wamesukumwa na jitihada za mwenyekiti kwenye kukijenga chama.Anataja mafanikio anasema tulikuwa na madiwani 40 leo wako zaidi ya 500

Anataja idadi ya wabunge walio anza na chadema hadi waliopo sasa.Mzee anasema amefungwa kwa ajili chadema, amelala nje kwa ajili ya chadema kutokana na kusakamwa na ccm

Anasema Mbowe ana historia na mageuzi ya nchi hii na hakuwahi kukubali kukata taama kwa kuwav anataka na amini kwenye mabadiliko

Sasa anafuata muwakilishi wa kinondoni Mama Esther Samanya

Anataja sababu

1. Hali ya chama ilivyo kuwa na kilivyo sasa ambapo kimefanya chaguzi kuanzia misingi, matawi, wilaya hadi mikoa ikiwa ni mara ya kwanza katika historia ya chama.

2. Utashi wa mwenyekiti kukikuza chama na kuwa mbunifu .

Sasa anatuata peter chacha muwakilishi wa wazee wa ilala.

Anasema wazee wa kigoma wametuwahi maana wao walitaka kumchukulia fomu kabla yao

Wanamfahamu mwenyekiti Mbowe tangu akiwa kijana kwenye chama mpaka hapa alopofikia sasa akikaribia uzee

"...Tuna upendo na tunamuamini sana mbowe na tunaamini atakipeleka chama hadi kuchukua dola" "..una watu wanao kipenda chama nyuma yako.. chapa kazi kamanda.."

Sasa wanafuata wa wazee wa Temeke.Waziri Mkumuna mwenyekiti wa wazee mkoa wa Temeke.

Anatoa shukrani kwa wazee wa kigoma hususani mzee mapigo saba kwa hatua walizo chukua

Anamuomba mwenyekiti apokee fomu na kutimiza malengo ya chama kuelekea kushika dola.Tanzania nzima ina ona kazi aliyofanya Mbowe

Anafuata muasisi wa chama wilaya ya temeke anawapongeza wazee wa kigoma, alikuwa miongoni mwa wazee 60 walioasisi chama hiki.Amemtaka kila mzee wa chadema kupeperusha bendera kwenye nyumba yake

Anafuata mzee kutoka Pwani Said Bakari Mazoea.Anasema Pwani yote inamuunga mkono Mbowe kwa kazi kubwa anayofanya.

Sasa anazungumza mwenyekiti wa bavicha kutoka Njombe.

Kwa niaba ya vijana anatambua mchango wa mh mbowe kutupeleka vijana nchi ya ahadi.Anatambua mchango wa waasisi kama kina mzee kimesera, kina mzee Athumani mapigo saba.

Anafuata mzee Peter Kimesera muasisi wa chama.

Tumeanza na watu 30 tukafanya mikutano 67. Wakati huo Mbowe akiwa kijana. Mbowe amepewa jina la Freeman ana wajibu wa kuwafanya watanzania kuwa Freeman.

Aliposhika chama akazindua chama upya, kuanzia mavazi mpaka aina ya siasa hadi hapa chama kilipo fikia.Kuanzia ongezeko la madiwani, wabunge na wanachama ni kutokana na mafanikio yaliyo fikiwa ndani ya chama

Sasa anafuata mratibu wa kanda ya Pwani.

Sisi waratibu tumekaa na kuamua hatma ya chama kwa kukuomba ugombee uwenyekiti.
Tunakuomba uchukue fomu uendelee kuwa mwenyekiti wetu

Sisi chadema ndio tuna mamlaka ya kichagua kiongozi wetu, msajali na mawakala wengine hawana mamlaka ya kuingilia mambo yetu.

Umejitolea mhanga, walitaka kukutoa roho soweto na bado hukuridi nyuma.

Updates 3...

Sasa anafuata Kamanda Mbowe.

1. Chadema imesheheni watu wenye vipawa na taaluma mbalimbali kwanini iwe mimi?

2. Sikukusudia kugombea uenyekiti wa chadema na kauli yangu niliitoa kwenye kamati kuu. Na niliwaambia tutafute mtu mwingine tunayemuamini lakini kamati kuu ikaja na azimio na ikakataa.

Kamanda Mbowe kwa heshima kubwa anakabidhiwa Fomu hapa huku ukumbi mzima ukizizima kwa hoihoi nderemo na vifijo.

Baadhi ya akina mama wanaangua kilio cha Furaha.

MWISHO
 
Namtakia ushindi na kumuombea kila la heri...
Huyu ni zaidi kamanda... ni jemedari...
 
Na Mungu Mwenyezi amlinde, amjalie hekima na maarifa. Kama anavyolilinda taifa la Israel, vivyo hivyo, mkono wake uwe pamoja na Mh. M/kiti wetu ili atuongoze tena katika kipindi hiki cha misukosuko inayozalishwa namaccm ka ebola.
Bwana na awabariki hao Wazee, vijana nao waone mema alotenda wamuunge mkono. Virusi woote awamalize kabisa kutoka CDM yetu. Ameeen
 
WanaJF

Karibuni katika tukio la kihistoria la kumuomba na kumkabidhi fomu za kugombea Uenyekiti wa Chadema Taifa shujaa na mpambanaji asiyechoka Kamanda Freema Aikaek Mbowe.

Tukio hili linafanyika katika hoteli ya Protea Upanga jijini DSM.Itakumbukwa wazee kutoka sehemu mbalimbali nchini wameunganisha nguvu kumuomba Kamanda Mbowe kugombea nafasi hii.

Ufalme unagombewa siku hizi? Chama ni chake na baba mkwe wake ( MTEI)
 
Sjui hii inamaana gani,yaani tukio lenyewe linamaana gani?..tabia hio wanayo ccm kwann tena chadema? Mie sjaipenda na kama mtakubaliana namm chukueni note juu ya hili,then utaja kujua madhara yake hata kama sio leo!..yeye hajaamua hadi anaombwa?...no ningekuwepo ningetofautiana kidogo na walioibariki hatua hii.Yeye angechukuwa form yeye kama yeye,kama alivyokuwa akichukua sku za nyuma..unless tell me kuwa tunataka kuiga mambo ya ccm
 
Kwani form zinatolewa hotelini au Makao makuu ya chama?au mimi ndo sijaelewa......Tafadhali nifahamisheni kulikoni hadi waende kumkabidhia huko...
 
Kila la Kheri kamanda Mbowe,najua leo ni Msiba kule Lumumba.Kamanda Mbowe bado tunakuhitaji,tunakuamini katika kulipigania taifa hili kutoka kwa Mkoloni mweusi
 
Back
Top Bottom