Fraternity: Muda wa Kuanza Upya {DINI}

Fraternity: Muda wa Kuanza Upya {DINI}

Mkuu hilo fungu halijasema matajiri hawataingia mbinguni. imesema itakuwa vigumu, bali siyo hataingia. Kiswahili hicho mkuu.

Wewe sijajua hiyo dini yako unayoanzisha unataka kupeleka watu wapi. Kama ni mbinguni na umepata fomula rahisi ya kutufikisha huko, tutajiunga
Hakuna kitu kiitwacho mbinguni ni utunzi wa wajanja kuwaingiza mjini
 

Attachments

  • IMG-20190622-WA0005.jpg
    IMG-20190622-WA0005.jpg
    54.3 KB · Views: 16
Kwa hiyo wewe mkuu unataka tuamini maoni yako na misimamo yako tu, ambayo haina kichwa wala mkia. Kila la heri
My point is clear, huwezi kuquote kitu nisichokikubali na sitokikubali. Leta hoja yako wewe kama wewe. Mana kuna dini zaidi za 2000 sasa tukiquote kwa mabudha huko utakubali
 
Mimi ni mkristo ila sijawahi kuelewa ukristo na nilishaachana nao kitambo sana.
Katika pitapita zangu mtaani na ndg na jamaa nimegundua asilimia kubwa ya vijana hawajihusishi tena na masuala ya dini. Hii ni either baada ya kuvunjwa moyo na viongozi wao wa kidini na kutokubaliana na mambo wadini wanafanya.
Mfano. Pasta anamuombea muumini kwa kumshika nyeti, kutembea na waumini (wake za watu), kutumia nguvu za giza katika huduma n. K
Hizi zimewapa watu wengi hofu kubwa na kukosa imani na dini.
Wakati tukiamini Israel ni Taifa la Mungu na tunaenda kuhiji huko wao wanasema kabisa kwenye maandiko yao Mtu mweusi ni mtu aliyelaaniwa.
Kuna haja sasa ya kuanzisha Fraternity au kundi la watu tusioabudu na kuamini katika misingi ya dini zao ila tunaamini uwepo wa Mungu muumba. Na msingi wa Imani hii mpya ni Afrika na sio hizi zilizoletwa na watu wa magharibi.
Msingi wa mkuu wa Imani hii ni kuwasaidia wasio jiweza kama ibada takatifu ya kumtukuza Mwenyezi Mungu.
Itaanza kama Taasisi isiyo ya kiserikali na baadaye itasajiliwa kama taasisi ya kidini{Kwa mjibu wa sheria}

Wale ndugu zetu wanaoamini sana katika dini zao waendelee ila kuquote vifungu vya maandiko yao huku sio mahali pake.

Soon Tutawaletea Taarifa kamili. ASANTENI.
Haya yote unayataka kwenye kundi lako jipya yapo kwenye hilo kundi la zamani ulilokuwa unaliamini (ukristo), na sasa unalikimbia
Tatizo naona ni utekelezaji tu, na wewe kama muumini ulikuwa na wajibu wa kuyatekeleza, lakini unataka kuanzisha kundi lingine la kusaidiana. Kuna tofauti gani. Hivyo vya kusaidiana utavipataje, si ndo utarudi kwa wanachama wenzio kuomba sadaka? Au nini chanzo cha mapato ya hilo kundi lako jipya mkuu. Sioni tofauti ya kundi lako na hilo lingine.
Fafanua
 
Haya yote unayataka kwenye kundi lako jipya yapo kwenye hilo kundi la zamani ulilokuwa unaliamini (ukristo), na sasa unalikimbia
Tatizo naona ni utekelezaji tu, na wewe kama muumini ulikuwa na wajibu wa kuyatekeleza, lakini unataka kuanzisha kundi lingine la kusaidiana. Kuna tofauti gani. Hivyo vya kusaidiana utavipataje, si ndo utarudi kwa wanachama wenzio kuomba sadaka? Au nini chanzo cha mapato ya hilo kundi lako jipya mkuu. Sioni tofauti ya kundi lako na hilo lingine.
Fafanua
Utofauti mkubwa sana. Labda kama hujataka kuuona. Kuna tofauti kubwa kati ya sadaka na msaada. Fraternity ni watu wenye mtazamo mmoja na lengo lao ni moja. Kumsaidia asiyejiweza sio lazima utoe hata wewe unaweza ukatoa bila kujiunga. Na utakuwa umetekeleza nguzo yetu bora kabisa katika imani hii. Wakati watu wakienda kuhiji huko Israeli kwa kutumia dola 3,000 na wakirudi wanafikiri wamekuwa nao wayahudi sisi tunasema hapana tutaenda kuwatembelea maskini huku ulikozaliwa kijijini.
 
Hata hizo dini unazozilalamikia zilianzishwa na watu waliokuwa na mitazamo yako kama ulivyo na mtazamo tofauti wewe.....

Mwisho wa siku vyote vinaishia katika imani (kuamini) tu
 
Kadili dunia inapojitenga na Mungu hasa anapokiwa amekwisha tambulishwa kwao ndivyo maovu yanaongezeka Exponentially.
Hii ni kanuni.

Siku sio nyingi, utaona matukio ya ajabu sana. Sio waka sababu ya watu ila hata ardhi italalamika kama ile ya Sodoma na Gomora.

Huwezi kuachana na Mungu eti kisa mchungaji mzinzi, padri mlevi, sijui pastor mchawi.
Hii ni sababu dhaifu sana
 
Katika imani kuna mambo mengi ila katika yote jambo kubwa ni kuvishinda vishawishi na kusimamia pale unapoamini,kuwa mkristo au muisilamu sio kigezo cha kuingia peponi bali matendo yetu ndio funguo zetu na ndio maana kuna njia ya wema na ubaya,hapo utachagua mwenyewe na sio kufuata kile ukionacho kwa watumishi wa Mungu sababu wao pia ni binadamu na wanapitia changamoto na vishawishi
Very well said
 
Mkiri Yesu Kristo kama Bwana na Mwokozi wa Maisha yako nawe utapata raha nafsini mwako,acha mbwembwe za Mpinga Kristo
Ukichelewa soon as possible Mpka mende iliyo ndani kwako itamkiri kwamba Ni BWANA NA MWOKOZI.
 
Kadili dunia inapojitenga na Mungu hasa anapokiwa amekwisha tambulishwa kwao ndivyo maovu yanaongezeka Exponentially.
Hii ni kanuni.

Siku sio nyingi, utaona matukio ya ajabu sana. Sio waka sababu ya watu ila hata ardhi italalamika kama ile ya Sodoma na Gomora.

Huwezi kuachana na Mungu eti kisa mchungaji mzinzi, padri mlevi, sijui pastor mchawi.
Hii ni sababu dhaifu sana
Kuacha kusali na kuamini mnako amini sio kujitenga na Mungu. Ukristo sio Mungu. Watu wanaamini kama sio mkristo huna Mungu. Nenda China 99% sio wakristo hao siwangeshakuwa wamefika huko Gomora.
 
Ofcourse, hata mababu zetu waliotaka kulinda imani zao za kuabudu walitengwa na ndugu zao wa karibu kwa kuambiwa wanamwabudu shetani ila wao waliopokea yaliyoletwa na Mzungu na Mwarabu ndo wanamwabudu Mungu
Hizo dini za mababu watu walishaziacha wakafuata dini zengine na hivi sasa watu hawataki tena kufuata mambo ila wewe unataka kuwarudisha tena kwenye mambo ya dini,una kipi cha offer huko? Kama kuna watu wanaamini Mungu na kumuewa huyo Mungu pasina dini iweje tena waje kujiiingiza kwenye dini ili iweje? Huoni unarudisha watu katika mambo yaleyale tena ambayo ndio wanajitoa huko?

Kipi cha maana kutaka watu wawe na dini?
 
Utofauti mkubwa sana. Labda kama hujataka kuuona. Kuna tofauti kubwa kati ya sadaka na msaada. Fraternity ni watu wenye mtazamo mmoja na lengo lao ni moja. Kumsaidia asiyejiweza sio lazima utoe hata wewe unaweza ukatoa bila kujiunga. Na utakuwa umetekeleza nguzo yetu bora kabisa katika imani hii. Wakati watu wakienda kuhiji huko Israeli kwa kutumia dola 3,000 na wakirudi wanafikiri wamekuwa nao wayahudi sisi tunasema hapana tutaenda kuwatembelea maskini huku ulikozaliwa kijijini.
Je hizi dini zilizopo zinakuzuia kuyafanya hayo yote?
 
Back
Top Bottom