Francinsco Nguema: Rais kichaa.

Francinsco Nguema: Rais kichaa.

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,650
Reaction score
20,994
Huyu jamaa alikuwa Rais wa Equatorial Guinea toka waka 1968 hadi 1979 alipopinduliwa na Mpwa wake Teodoro Nguema ambaye ndiyo Rais wa sasa. Vituko vyake.

1.Jamaa alikuwa mtumiaji mkubwa wa bangi na mmea uitwao iboga ambao nao ni kama bangi.

2. Alipochukua urais alichukua madaraka yote ya Bunge na Mahakama na kujimilikisha.

3.Kumsema vibaya Rais au baraza lake lilikuwa ni kosa la kufungwa mika 30 jela.

4. Ali piga marufuku vyama vyote isipokuwa chake ambacho yeye ndiye alikuwa rais wa maisha.

5. Alitoa amri ya kuua wote wanaovaa miwani.

6.Alikataza matumizi ya dawa za kizungu akisema siyo utamaduni wa muafrika.

7.Ili kuzuia watu wasikimbie nchi aliharibu boti zote na kupiga marufuku uvuvi. pia aliharibu barabara zinazotoka nje ya nchi.

8.Alibadilisha Motto wa nchi kuwa "hakuna Mungu mwingine bali Marcias Nguema"

9. Jamaa alimuua gavana wa benki kuu na akawa anatembea na mabriefcase ya pesa.

10. Alikuwa anaua wasomi, pia aliua theluthi mbili ya wabunge na mawaziri wake 10.

11. Kwenye utawala wake karibu nusu ya raia walikimbia nchi. Inasemekana kwenye utawala wake watu 50,000 hadi 80, 000 waliuwawa.

Mwaka 1979 alipinduliwa na mpwa wake ambaye ndiye rais wasasa wa Nchi hiyo. Alipinduliwa baada ya kuanza kuua hadi ndugu zake, wakakaa chini wakaona wamuondoe. Aliuliwa kwa kupigwa risasi.

Wikipedia.

Nashauri mtu kabla ya kugombea urais atuonyeshe cheti cha daktari wa magonjwa ya akili kwamba hana tatizo lolote la akili🙂.

Palantir Malcom Lumumba mmemuona Nguema mkubwa!!??, Palpatine akasome!!.
 
Na kinachonishangazaga usalama wa Taifa uwa wanatii tu ilimradi alietoa Amri ni Rais. Kuna wakati nashawishika kuamini alichosema plato watu wa majeshi ni Iron huwa hawatumii akili bali nguvu.

Nchi kama Iyo unajiuliza usalama wa Taifa walikuwa wapi kudhibiti hilo? Utakuta ndio waliokuws wanatumika kuua hao watu.

Upone haraka Tundu Lissu. Mliotangulia mbele za haki Mlale kwa Amani.
 
Trump naye inadaiwa alijiandikia mwenyewe cheti cha afya ya akili yake. Kulikuwa na thread humu ikizungumzia hiyo kitu. Inaonekana afya ya ubongo ni tatizo linaloenea kwa kasi duniani.
 
Aliyepinduliwa alikuwa kichaa wa madaraka, aliyepindua ni mlevi wa madaraka hadi leo. Afrika ni shithole kweli!
Noma sana Afrika yetu. Kazi kubwa ya Rais ni kuhakikisha anabaki madarakani. Kazi zingine zote huwa ni kusupport hilo la kubaki madarakani. Huyu Teodoro naye anaelekea kumrithisha mtoto wake, Brothermen fisadi.
 
Huyu jamaa alikuwa Rais wa Equatorial Guinea toka waka 1968 hadi 1979 alipopinduliwa na Mpwa wake Teodoro Nguema ambaye ndiyo Rais wa sasa. Vituko vyake.

1.Jamaa alikuwa mtumiaji mkubwa wa bangi na mmea uitwao iboga ambao nao ni kama bangi.

2. Alipochukua urais alichukua madaraka yote ya Bunge na Mahakama na kujimilikisha.

3.Kumsema vibaya Rais au baraza lake lilikuwa ni kosa la kufungwa mika 30 jela.

4. Ali piga marufuku vyama vyote isipokuwa chake ambacho yeye ndiye alikuwa rais wa maisha.

5. Alitoa amri ya kuua wote wanaovaa miwani.

6.Alikataza matumizi ya dawa za kizungu akisema siyo utamaduni wa muafrika.

7.Ili kuzuia watu wasikimbie nchi aliharibu boti zote na kupiga marufuku uvuvi. pia aliharibu barabara zinazotoka nje ya nchi.

8.Alibadilisha Motto wa nchi kuwa "hakuna Mungu mwingine bali Marcias Nguema"

9. Jamaa alimuua gavana wa benki kuu na akawa anatembea na mabriefcase ya pesa.

10. Alikuwa anaua wasomi, pia aliua theluthi mbili ya wabunge na mawaziri wake 10.

11. Kwenye utawala wake karibu nusu ya raia walikimbia nchi. Inasemekana kwenye utawala wake watu 50,000 hadi 80, 000 waliuwawa.

Mwaka 1979 alipinduliwa na mpwa wake ambaye ndiye rais wasasa wa Nchi hiyo. Alipinduliwa baada ya kuanza kuua hadi ndugu zake, wakakaa chini wakaona wamuondoe. Aliuliwa kwa kupigwa risasi.

Wikipedia.

Nashauri mtu kabla ya kugombea urais atuonyeshe cheti cha daktari wa magonjwa ya akili kwamba hana tatizo lolote la akili🙂.

Palantir Malcom Lumumba mmemuona Nguema mkubwa!!??, Palpatine akasome!!.
Chancellor Palpatine a.k.a Lord Voldermort . Bwahahahahaha, Giant umenivunja mbavu leo: Nacheka kama mazuri vile lakini tumefika pabaya sana.
 
Kwa wanaosikiliza nyimbo za kikongo sanasana bendi ya extra musica,,, huwa wanamtaja mtoto wa rais wa sasa wa equatorial Guinea,,,, anaitwa papaa teodore nguema obiang
 
Siyo uchochezi mkuu. Uelewa wetu kuhusu magonjwa ya akili upo chini sana na watu wenye viashiria vya magonjwa ya akili wamekuwa wakipata nguvu sana. Angalia mtu kama babu wa Loliondo na Dr shika? Inabidi tuwe na utaratibu ili watu wa dizaini hiyo wasishike nchi.
 
"Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa".

Ufunuo wa Yohana 2:29
 
Very interesting, why Francisco Nguema now? Hii ni witch hunting
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Yote juu ya yote miaka kumi ya utawala wa MAGUFULI mpaka iishe ndio atoke madarakani.
 
Ndiyo maana mimi siku zote nakuwa na mashaka na wavuta bangi. We mtu ubongo umejaa moshi wa sumu kisha unatawala nchi?
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Back
Top Bottom