Form 4 ya 2008 na 2012 ipi ilikuwa ya moto?

Form 4 ya 2008 na 2012 ipi ilikuwa ya moto?

Et wanaJF kati Ya form Four Ya 2008 na 2012 ipi ilikuwa Ya moto Sana

2008 chini Ya Jumanne Maghembe

2012 chini ya Joyce Ndalichako.
Ndalichako amekua waziri 2015. Zote mbili kasimamia Ndalichako kama katibu wa NECTA. Waziri 2012 alikua Shukuru Kawambwa. As ipi Kali 2008 japo nimefanya mtihani after that but before 2012.
 
Madogo wa 2012 walipitia changamoto ya kufeli kutokana na kulikuwa na mgomo wa kati ya walimu na serikali, hasira zao wakizihamishia kwenye kusahihisha mitihani.

Pia grades walipandishiwa A 85-100, B 65-74 nk
 
T
2008 nimemaliza form 4 azania secondary. Nakumbuka pepa la hesabu lilivuja likabandikwa mpaka kwenye nguzo ya umeme mchikichini. Ilifika hatua ikabidi serikali ihailishe mtihani wa hesabu. Nilifanya maangamizi mazito sana form 5 nikapangiwa EGM mzumbe morogoro
TAyari ushajulikana, hata hivyo Mzumbe sec miaka hiyo hakukuwa na EGM
 
Inahusu nini madam😅
Bado sijaielewa ila kuna Jamaa mmoja mzembe mzembe sana hivi. Hajui hata kujificha, kila chaka analojificha lazima aache alama hadi maadui wanajua yupo hapo. Khaa ngoja niendelee kuiangalia nitakuja kukuhadithia vizuri.
 
Form four zote mbili za 2008 na 2012 zote zilikuwa chini ya Joyce Ndalichako kama katibu mkuu wa baraza la mitihani la Taifa(NECTA).
Hata hivyo, kila moja ina kumbukumbu yake.
Form four ya 2008 inakumbukwa kwa mitihani yake kuvuja hasa mtihani wa Basic Mathematics hadi kusababisha mtihani huo kuahirishwa. Nadhani iliahirishwa mwezi mmoja mbele.
Mitihani mingine iliendelea kama kawaida isipokuwa Basic Mathematics. Inasemekana pia mitihani mingine ilikuwa ikibadilishwa kimya kimya ili kuzuia kuvuja.
Form four 2012 ni maarufu kwa wanafunzi wengi kufeli hali iliyosababisha matokeo ya mwanzo kufutwa na baadae yakatoka mengine(Standardization effect).
 
Bado sijaielewa ila kuna Jamaa mmoja mzembe mzembe sana hivi. Hajui hata kujificha, kila chaka analojificha lazima aache alama hadi maadui wanajua yupo hapo. Khaa ngoja niendelee kuiangalia nitakuja kukuhadithia vizuri.
Hahahaha huyo anaonekana ata die tu
 
Madogo wa 2012 walipitia changamoto ya kufeli kutokana na kulikuwa na mgomo wa kati ya walimu na serikali, hasira zao wakizihamishia kwenye kusahihisha mitihani.

Pia grades walipandishiwa A 85-100, B 65-74 nk
Kweli. Kipindi kile mgomo wa walimu ulisababisha ila sio kwenye kusahihisha mitihani. Mgomo wa walimu nadhani ulianza kati ya 2009 na 2010(nipo tayari kwa marekebisho). Walimu walikuwa wanaenda kazini kama kawaida ila ilikuwa ni kutimiza ratiba tu. Darasani hakuna cha maana sana kilichokuwa kinafanyika. Matokeo yake wanafunzi hawakuwa na uelewa mzuri kujibu mitihani ya taifa
 
Back
Top Bottom