Forex Tutorials for Beginners: Pitia hapa kujifunza

Forex Tutorials for Beginners: Pitia hapa kujifunza

Status
Not open for further replies.

Jumax

Senior Member
Joined
Mar 4, 2017
Posts
117
Reaction score
229
Habari za muda ndugu zangu wana JF, natumai mu wazima wa afya.

Awali ya yote ningependa kutoa shukrani zangu za dhati kwa mkuu ONTARIO na wachangiaji wengine wengi kama mashujaa wetu katika suala zima la kufamishana na kuelimishana kuhusu biashara hii ya Forex.

Katika pita pita na harakati zangu za kuhakikisha tonge linaenda kinywani ndipo nikabahatika kukutana na mnaijeria mmoja ndani ya bus la kuelekea mjini Mbabane nchini Swaziland kutokea Maputo nchini Msumbiji akiwa ameshika simu yake busy huku akifurahi mwenyewe na kucheka.
Ghafla uvumilivu ulinishinda na kutaka kufahamu ni nini haswa jamaa yule alikuwa akifanya maana alipatwa na furaha isiyo na kifani.

Baada ya kutupia jicho ndipo nikaona namba za bluu na nyekundu zikisoma kwenye kioo cha simu yake, kutazama kwa umakini ndipo nilipogundua kuwa alikuwa anatrade forex na kwa kuwa nilikuwa nimeshapata mwangaza wa taarifa kadhaa kutoka kwa boss ONTARIO miezi kadhaa iliyopita humu JF ikanibidi nimsalimie bwana yule na kumuuliza ni nini haswa kiini cha furaha yake.

Katika maongezi ikabidi nimueleze ukweli kuwa mimi ni 'mweupe' kabisa yaani sifahamu ni jinsi gani ya kutrade forex ingawa nilikuwa nimeshapata kusikia kidogo ni nini forex.
Ndipo hapo aliponiambia kuwa laiti kama ungalijua utamu wa kitu hii wala usinge poteza muda wako kufanya mambo mengine. Baada ya kufika Mbabane akanipatia namba yake pamoja na FOREX pdf file ambayo nitaiattach hapa kwa ajili ya kujifunza na akaniomba nisisome kwa pupa wala haraka na pindi nitakapo maliza nisisite kumtafuta kwa msaada wowote ule.

Nimejaribu kuanzia mbali kidogo ili nanyi ndugu zangu muweze kupata picha halisi how really this Forex thing is, katika kipindi hiki ambapo tunasubiri Mafunzo zaidi kutoka kwa mkuu ONTARIO .

This PDF file is very informative kwa beginners wote ambao wana nia ya kufahamu na kufanya FOREX TRADING.

Na pia si vibaya kuongezea hapa resources zozote ambazo zitasaidia kujinoa kuhusiana na forex trading maana walio wengi bado hawajapata mwangaza katika forex trading, maana haitakuwa vizuri kuingia darasani tukiwa vichwa vitupu.

Napenda kuwasilisha. Ahsanteni.

==========================
An introduction to the Basics of Forex Trading


How to manage a Forex Account


=========• UPDATE •==========

Nimebahatika kupata hii link ya group Maarufu kwaajili ya materials na Books kuhusu Forex Trading so nikaona si mbaya kushare nanyi tena ingawa hapo awali kuna baadhi ya wachangiaji walijitokeza kunishambulia kwa maneno makali wakidhani kwamba kila mtu anaeleta uzi au mada yoyote humu JF kuhusu Forex trading basi anamuonea wivu au Kumpinga ndugu Ontario wakati kiukweli si hivyo bali tunajaribu kusaidiana ili kuhakikisha sisi sote tunasonga mbele.

Hili ni group la TELEGRAM so ili kujiunga inabidi kwanza upakue App ya telegram kwa wale ambao watakuwa hawana.

FOREX LIBRARY


fd1f21f6268d1572fc4491a05e64aeb2.jpg


0b9ef40c8c37844d34cad7e4da9097c3.jpg
 

Attachments

mkuu tupia kwenye uzi wetu wa matrader... itapendeza zaidi maana kule ndo tutajifunza zaidi.
 
Ungekua muungwana ungeandika haya yote kulekule kwa ONTARIO page mana hakuna jipya hata moja pia Pdf uliyoo attach ni sehemu ndogo sana ya forex bible, hakuna atayekuja kutoa info za forex TZ baada ya ONTARIO sababu yeye ndo aliyetuamsha usingizini mzito na kutuonyesha njia juu ya Forex, hata kama nitakosa training yake lakini amesha nionyesha njia, Lets join newbie
 
Ungekua muungwana ungeandika haya yote kulekule kwa ONTARIO page mana hakuna jipya hata moja pia Pdf uliyoo attach ni sehemu ndogo sana ya forex bible, hakuna atayekuja kutoa info za forex TZ baada ya ONTARIO sababu yeye ndo aliyetuamsha usingizini mzito na kutuonyesha njia juu ya Forex, hata kama nitakosa training yake lakini amesha nionyesha njia, Lets join newbie

Mkuu ni jambo lipi linanitoa uungwana hapo? Nimeshindwa kutoa credits kwa mkuu Ontario ? Au kosa langu ni kushindwa kumerge threads ? Na kama ni hivyo basi naomba mods watusaidie. Kingine hiyo PDF hapo ni very recommended kwa watu wanaoanza kujifunza kama mimi nikaona si vibaya kushare na ndugu zangu ila kama nimekosa naomba nitangulize samahani mkuu
 
This thread is very crucial,, Asante mkuu hasa kwa hiyo attachment
 
Habari za muda ndugu zangu wana JF, natumai mu wazima wa afya.

Awali ya yote ningependa kutoa shukrani zangu za dhati kwa mkuu ONTARIO na wachangiaji wengine wengi kama mashujaa wetu katika suala zima la kufamishana na kuelimishana kuhusu biashara hii ya Forex.

Katika pita pita na harakati zangu za kuhakikisha tonge linaenda kinywani ndipo nikabahatika kukutana na mnaijeria mmoja ndani ya bus la kuelekea mjini Mbabane nchini Swaziland kutokea Maputo nchini Msumbiji akiwa ameshika simu yake busy huku akifurahi mwenyewe na kucheka.
Ghafla uvumilivu ulinishinda na kutaka kufahamu ni nini haswa jamaa yule alikuwa akifanya maana alipatwa na furaha isiyo na kifani.

Baada ya kutupia jicho ndipo nikaona namba za bluu na nyekundu zikisoma kwenye kioo cha simu yake, kutazama kwa umakini ndipo nilipogundua kuwa alikuwa anatrade forex na kwa kuwa nilikuwa nimeshapata mwangaza wa taarifa kadhaa kutoka kwa boss ONTARIO miezi kadhaa iliyopita humu JF ikanibidi nimsalimie bwana yule na kumuuliza ni nini haswa kiini cha furaha yake.

Katika maongezi ikabidi nimueleze ukweli kuwa mimi ni 'mweupe' kabisa yaani sifahamu ni jinsi gani ya kutrade forex ingawa nilikuwa nimeshapata kusikia kidogo ni nini forex.
Ndipo hapo aliponiambia kuwa laiti kama ungalijua utamu wa kitu hii wala usinge poteza muda wako kufanya mambo mengine. Baada ya kufika Mbabane akanipatia namba yake pamoja na FOREX pdf file ambayo nitaiattach hapa kwa ajili ya kujifunza na akaniomba nisisome kwa pupa wala haraka na pindi nitakapo maliza nisisite kumtafuta kwa msaada wowote ule.

Nimejaribu kuanzia mbali kidogo ili nanyi ndugu zangu muweze kupata picha halisi how really this Forex thing is, katika kipindi hiki ambapo tunasubiri Mafunzo zaidi kutoka kwa mkuu ONTARIO .

This PDF file is very informative kwa beginners wote ambao wana nia ya kufahamu na kufanya FOREX TRADING.

Na pia si vibaya kuongezea hapa resources zozote ambazo zitasaidia kujinoa kuhusiana na forex trading maana walio wengi bado hawajapata mwangaza katika forex trading, maana haitakuwa vizuri kuingia darasani tukiwa vichwa vitupu.

Napenda kuwasilisha. Ahsanteni.
Shukrani sana kaka

Ubarikiwe tena tena...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom