Fomu za Edward Lowassa zilitimia?

Fomu za Edward Lowassa zilitimia?

Sheria iko wazi sana. Ufafanuzi ni kwamba mgombea anatakiwa apate wadhamini kwenye mikoa isiyopungua minne na isiyozidi kumi.
 
Wakati Prof. Muhongo anarejesha form kuomba ridhaa ya MaCCM alileta hadi CD wakamwambia aache mbwembwe...
 
Jana,wagombea wa CCM na CHADEMA walikwenda Mahakama Kuu ya Tanzania kusaini fomu za kuwasilisha Tume ya Taifa ya Uchaguzi kulingana na matakwa ya Sheria za Uchaguzi. Wote wawili walijitokeza mbele ya Jaji Kihiyo.

Wakati Magufuli akiwasilisha fomu 40 za kusainiwa,Lowassa aliwasilisha fomu 6. Hiyo ni kwa mujibu wa Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania,Mh.Kayoza. Kimahesabu,Lowassa hakuwasilisha fomu 34.

Fomu nyingine za Lowassa ziko wapi? Kwanini siziwasilishwe nazo kwa kusainiwa? NEC yaweza kumuengua asipotimiza masharti.

=================================



Chanzo: Mtanzania
safi sana mko makini sana, kweli mwaka huu lazima kieleweke hatua kwa hatua
 
Mkuu, hiyo hoja hata mimi imenichanganya. Ina maana NEC walifanya makosa kumpatia fomu pungufu ama kuna fomu ambazo hakutimiza masharti yake? Tatizo ninaloliona mimi kwa miaka mingi ni masharti ya ujazaji fomu kuwachanganya wagombea. Nakumbuka kesi ya Sambwee Shitambala

Attention ilikua kwenye mafuriko tu
 
Magufuli ana kichwa kigumu sana kuelewa mambo.kichwa kubwaaaa limejaaa maji
 
Kimsingi hua wanapewa fomu zote 40 kwa ajili ya kukusanya wadhamini lakini fomu 6 tuu ndizo zinakua na haja sana NEC ingawaje hata ukipeleka zote 40 wanapokea
Mbona mwanzo walipeleka fomu 4? Akilii yote imeelekezwa kwemye mafuriko,haya umepewa fomu 40 unarudisha 6.tutaona
 
Mkuu, hiyo hoja hata mimi imenichanganya. Ina maana NEC walifanya makosa kumpatia fomu pungufu ama kuna fomu ambazo hakutimiza masharti yake? Tatizo ninaloliona mimi kwa miaka mingi ni masharti ya ujazaji fomu kuwachanganya wagombea. Nakumbuka kesi ya Sambwee Shitambala
Nafikiri Sambwe si mfano mzuri kwa sababu inaonekana alifanya makusudi. Sheria inasema unaapa kwa hakimu, wewe unaenda kwa wakili n ukiwa mwanasheria?
 
Kuna watu humu hata cjui tuwaiteje hamjui hata sheria za uchaguzi wa mgombea urais ...umesoma kwenye magazeti umeelewa bado unakuja na huku ....hata ukipewa fomu 100 zinatakiwa zisainiwe 4 au 6 tuu...sasa umeshaelewa bado unaleta jf
 
Wakuu angalieni lisijekuwa ndo bao la mkono lenyewe hilo!! Wakizingua tunahamishia kura zetu kwa Mwigamba (ha ha ha ha haaaaaaa!!)

Kwa akili za kawaida tu tume ya uchaguzi kupitia maagizo ya bwana wao CCM wakithubutu kukata jina la Lowasa ndo mwanzo wa kuvuruga zoezi zima la uchaguzi
 
Mimi sijuhi sheria lakini ushahidi wa mazingira unaonesha kuwa Lowassa yupo sahihi...
Wanasheria wake walimwambia apeleke fomu nne kwa mujibu wa sheria..... Kule mahakama kuu wakashauri waongeze zingine mbili zikawa sita.

Sidhani kama huu ni wakati wa kuruhusu mapungufu kama hayo...
Bw. Petro kuwa na amani..!!
 
Kimsingi hua wanapewa fomu zote 40 kwa ajili ya kukusanya wadhamini lakini fomu 6 tuu ndizo zinakua na haja sana NEC ingawaje hata ukipeleka zote 40 wanapokea

Sasa hiyo ni kufuatana na matakwa ya sheria kwa maana kwenye sheria hiyo option hiyo ipo au ndivyo alivyoona huyo mwanasheria Marando? Kama hata ukipeleka zote 40 ulizokabidhiwa na tume zitawekwa saini waliona ugumu gani kupeleka zote wakielewa wanavyowindwa kuenguliwa wakikosea taratibu? Tusubiri maamuzi ya tume maana kama sheria ni ya 2015 haijazoeleka bado.
 
Petro E. Mselewa umeshajibiwa huku mkuu, shida una nyuzi nyiingi kweli hadi unasahau kutembelea nyingine
 
Last edited by a moderator:
Hivi alizunguka mikoa minne au Sita? Hizo fomu mbili zaidi alizowasilisha alisainisha wapi???

Queen Esther

Mimi sijuhi sheria lakini ushahidi wa mazingira unaonesha kuwa Lowassa yupo sahihi...
Wanasheria wake walimwambia apeleke fomu nne kwa mujibu wa sheria..... Kule mahakama kuu wakashauri waongeze zingine mbili zikawa sita.

Sidhani kama huu ni wakati wa kuruhusu mapungufu kama hayo...
Bw. Petro kuwa na amani..!!
 
Tume ya uchaguzi kesho itatangaza wagombea, kwa hiyo tusubiri tuone kama kuna atakayekatwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom