"FLYCATCHERS" hatari kwa utalii Arusha

Tembomtata

JF-Expert Member
Oct 3, 2011
266
426
Ongezeko la vijana wanaojulikana kama flycatchers hapa Arusha linaonekana ni tishio kwa utalii wa mji wetu na kwa nchi yetu kwa ujumla.Mwanzo walianza kama njia yakusaidia watalii kuwafahamisha sehemu za mji huu lakin kujipatia riziki, lakin sasa wamezidi mipaka.Vijana hawa wengi wao wanapendelea kuweka style ya rasta kuwa vutia wanawake wakizungu wamekuwa wakisimama nje ya ofisi za Tanzania Tourist Board wakisubiri watalii wanaoenda kuulizia habari za utalii katika ofisi hizo,wakiamini kwamba watalii hawa hawana ufahamu wowote kuhusu mji huu.

Wamekuwa wakiwang'ang'a nia watalii pindi watokapo tu kwenye ofisi hizo,nakuwafuata kokote watalii hawa waendapo hata kama mtalii hataki.Mimi kama mdau wautalii nimekuwa nikipokea malalamiko mengi kutoka kwa watalii pindi wanapoamua kuzunguka mji wenyew.Naomba TTB washughulikie swala hili kwan litaadhiri utalii wetu siku zijazo,kwani watalii hujiona kuwa hawako safe.Ikibidi Tanapa,Ngorongoro Conservation Area waingilie kati.
 
Kwani hao TTB , TANAPA at al sio malegelege yanayoongozwa na magamba matupu? What do u expect from such loosers.
 
Asante kwa taarifa mkuu,ila siku nyingine ningependa unieleweshe ni kwa nini kuna NCAA na hakuna SCAA? Nikimaanisha Serengeti Conservation Area Authority au hifadhi nyingine yoyote yenye kitengo kama hicho.
 
we have diferent categories za protected areas according to the activities allowed in these areas such as national parks(16),Conservation area(1),game reserves(severals),forests reserves,nature reserves, game sanctuary and other which makes a total of 520 protected areas in tz covering more than 25% ya ardhi yetu
Ngorongoro sio national park ina fall under Conservation Area Authority that means inajitegemea, na ipo yenyewe as ina support both wildlife and human being while other protected areas which fall under national parks authority zina deal na wildlife tu na watu hawaruhusiwi kuishi huko kama ngorongoro
 
Back
Top Bottom