nyabhingi
JF-Expert Member
- Oct 12, 2010
- 15,638
- 20,248
Mgeni rasmi Waziri Mkuu mstaafu na Mbunge wa Monduli Mh.Edward Lowassa akiwa pamoja na Mbunge wa Mbinga Magharibi Mh. John Komba na wengineo wakitest ubora wa Studio hiyo kwa kusikiliza baadhi nyimbo kadhaa zilizorekodiwa na studio hiyo ambayo imezinduliwa hivi karibuni nyumbani kwakwe Flora Mbasha (mwenye gauni damu ya mzee) huko Tabata Kisukulu jijni Dar wikiendi hii
Baadhi ya vyombo vya studio hiyo ya Msanii Flora Mbasha vikiwa tayari vimefungwa. Studio hiyo itatumika kurekodi nyimbo za muziki wa Injili na hata kuwasaidia wasanii wachanga wenye vipaji kwa ajili ya kuviendeleza. Flora Mbasha anakuwa mwanamuziki wa kwanza wa kike wa nyimbo za Injili kufungua studio yake mwenyewe
Huyu dada ambaye watu wanaamini ana upako huwa simwelewi,..kwanza nilimwona kavaa manguo ya kijani mwaka jana kikwete alipotangazwa rasmi kuwa mgombea kwa tiketi ya ccm,..nafikiri ni mwanachama wa ccm sababu aliwapigia hata debe wakati wa uchaguzi!!sasa hii ya kumwalika lowasa ndo imeniacha hoi,.lowasa amethibitika beyond reasonable doubt kuwa ni fisadi papa,may be iam wrong lakini sina heshima na huyu dada na gospel zake nilishaacha kuzisikiliza