Stroke
JF-Expert Member
- Feb 17, 2012
- 38,539
- 48,856
Leo nimeona sio vibaya kila mtu akashiriki kusimulia matukio ambayo unayakumbuka ulipokua boarding school, either ya kusikitisha au kufurahisha.
Kwa uchache haya ni ya kwangu.
1.Tabia za kutokupenda kuoga: Kutokana na hali ya hewa kuwa baridi sana pale shuleni kwetu, wengi wa wanafunzi walikua wanapiga , " Passport" au " Kogo",kuosha sehemu chache tu za mwili, bila kuoga kabisa. Kuna mwanafunzi mwenzetu huyu yeye alikua na uwezo wa kutokuoga semester nzima. Yeye alikua ananawa uso tu na kwenda parade. Baada ya wanabweni wenzake kuona tabia yake. Kikakaa kikao kisicho rasmi ambacho maamuzi yake ilikua lazima jamaa aoge. Kwa pamoja wakamkamata mhusika na kumwogesha.
2. Tabia za kupigana makofi wakati wa kulala: Kulikua na tabia ya kila mwanafunzi mgeni kupata ukaribisho kwa kupigwa kofi usiku na kupakwa colgate mdomoni usiku wa kwanza anapoingia bording. Wanachumba wote kwa pamoja humtegea mgeni na kusubiri alale. Halafu taa huzimwa zote bweni zima. Mhusika hulishwa colgate akiwa amelala na kupigwa kofi la ukaribisho.
3. Utoro kwenda kwenye maulidi na harusi: Jamii ya watu walioizunguka shule wengi walikua wa dini ya kiislamu, hivyo kulikua na sherehe nyingi za maulidi, hivyo pale kunapotokea maulidi basi vijana usiku hutoroka na kurudi na mifuko na plastiki yenye pilau. Vile vile kila kunapotokea harusi maeneo ya jirani na shule basi usiku wa sherehe husika watu huzamia harusini, kubadilisha menyu.
Kwa uchache yangu ni hayo tu, karibuni nanyi mlete ya kwenu.
Kwa uchache haya ni ya kwangu.
1.Tabia za kutokupenda kuoga: Kutokana na hali ya hewa kuwa baridi sana pale shuleni kwetu, wengi wa wanafunzi walikua wanapiga , " Passport" au " Kogo",kuosha sehemu chache tu za mwili, bila kuoga kabisa. Kuna mwanafunzi mwenzetu huyu yeye alikua na uwezo wa kutokuoga semester nzima. Yeye alikua ananawa uso tu na kwenda parade. Baada ya wanabweni wenzake kuona tabia yake. Kikakaa kikao kisicho rasmi ambacho maamuzi yake ilikua lazima jamaa aoge. Kwa pamoja wakamkamata mhusika na kumwogesha.
2. Tabia za kupigana makofi wakati wa kulala: Kulikua na tabia ya kila mwanafunzi mgeni kupata ukaribisho kwa kupigwa kofi usiku na kupakwa colgate mdomoni usiku wa kwanza anapoingia bording. Wanachumba wote kwa pamoja humtegea mgeni na kusubiri alale. Halafu taa huzimwa zote bweni zima. Mhusika hulishwa colgate akiwa amelala na kupigwa kofi la ukaribisho.
3. Utoro kwenda kwenye maulidi na harusi: Jamii ya watu walioizunguka shule wengi walikua wa dini ya kiislamu, hivyo kulikua na sherehe nyingi za maulidi, hivyo pale kunapotokea maulidi basi vijana usiku hutoroka na kurudi na mifuko na plastiki yenye pilau. Vile vile kila kunapotokea harusi maeneo ya jirani na shule basi usiku wa sherehe husika watu huzamia harusini, kubadilisha menyu.
Kwa uchache yangu ni hayo tu, karibuni nanyi mlete ya kwenu.