Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,316
- 33,112
Picha kutoka katika maktaba ya nifahamishe | Sunday, January 08, 2012 9:22 PM Vyombo vya habari vya Tanzania vimeripoti tukio la kuhuzunisha lililotokea mkoani Shinyanga. Tukio hilo linahusiana na fisi aliyevamia na kumnyakua mtoto wa miaka minne na kumjeruhi vibaya kiasi cha kupelekea mtoto huyo apoteze uhai. |
Kamanda wa polisi mkoani Shinyanga Diwani Athumani alisema majira ya saa 12 za jioni huko katika kijiji cha Giriku kata ya Bunamhala wilaya ya Bariadi, mtoto Wande Manjale (4) akiwa anacheza na dada yake Sabuhi Manjale (10) mwanafunzi wa darasa la tatu katika shule ya msingi ya Giriku walivamiwa na fisi. Watoto hao wakiwa umbali wa mita 50 kutoka nyumbani kwao walivamiwa na fisi. Fisi huyo alimrukia Wande na kumngata shingoni na kukimbia nae vichakani, ndipo dada yake Sabuhi alipopiga kelele za kuomba msaada na baba yao mzee Manjale Giriku (40) alipojitokeza kwa kushirikiana na wananchi wengine kumkimbiza fisi huyo. Fisi alimuacha mtoto huyo na kukimbilia vichakani baada ya kuwa amemjeruhi kichwani na sehemu za siri na kusababisha kifo chake. Kwa wasiojua mazingira ya Tanzania wanweza kushangaa sana kusikia habari hizi. Lakini ukweli ni kuwa, vijiji vya Tanzania vina hatari nyngi, na hii ni kutokana na mazingira duni ya vijijini. |