First born anapokuwa last born

First born anapokuwa last born

Mkuu nina kitabu cha Mwakasege alichoandika Namna ya kumuombea mzaliwa wa kwanza kaeleza mambo mengi sana.....mojawapo ni kuwa baraka za familia huingia kupitia mzaliwa wa kwanza na mzaliwa wa kwanza ndo lango kuu either la pepo au mikosi katika familia au hata mambo mazuri na yenye baraka
Je mtoto wa kwanza akifariki akiwa Mdogo tu itaathiri vipi wadogo zake!?
 
Mi nna mdogo wangu ni smart, handsome ana akili sanaa kuliko mimi, sija wahi ata mind, kwanza ndo namuombea afanikiwe zaid, pia na mi nakazana ki juhud zangu, halaf nafurah ata member wa familia mmoja atusue na wazaz wafurahi, pia naamini kutangulia kuzaliwa si kigezo cha mimi kuumia wenzangu wakifanikiwa, rizki mpaji ni Mungu, ni mtu mwenyewe tuu na attitude yake adi kujiua apo kazid
 
Yesu alikuwa first born kwa Maria.. Mafanikio yake yanafahamika vizuri... Musa pia vivyo hivyo kwa mama yake...
Wachina na ile sheria yao ya mtoto mmoja hiyo vita ya shetani imewapitia pembeni? Maana wanafanikiwa na uchumi wao unakua spidi..
Well,its open for discussion.Wewe kaka yako vp?
 
Mara nyingi first born hufa vifo vya ghafla.....

Au pale wanapoanza kufanikiwa unashangaa anapoteza maisha ghafla, aidha kwa ajali isiyotarajiwa, maradhi ya muda mfupi n.k
Mkuu usiguse mafanikio yenyewe nahisi kuyanusa nawe unaanza kufa kufa tu kwa first born!!!
 
Tafuta semina ya mchungaji Christopher Mwakasege juu ya mtoto wa kwanza.Anasema kuna vita kubwa sana kati ya shetani na uzao wa kwanza,mara nyingi mtoto wa kwanza huwa ni tatizo...sijui ni kwanini....Lakini hebu tuanze na uzao wa kwanza kabisa duniani wa Adam na Hawa ambae ni Kaini, Kaini alimuua mdogo wake kwasababu ya wivu,mdogo wake alifanya vizuri kuliko kaka yake ikawa bifu zito.Twende uzao ya Isaka..Esau na Yakobo,ilitokea timbwili kubwa sana baada ya Yakobo kubarikwa badala ya Esau,kwa kuogopa kuuliwa na kaka yake Yakobo ilimbidi akimbie nyumbani miaka na miaka..Uzao wa Yakobo, Yusuph ambae sio mtoto wa kwanza wa yakobo alifanya vizuri kuliko kaka zake wakataka kumuua.Na hata uzao wa Yesse,Daud alifanya vizuri kuliko kaka zake.The list is endless... Hivyo basi unaweza kuona watoto wa kwanza huwa hawafanyi vizuri sana,sijui ni kwanini.Lakini mchungaji Mwakasege anasema ni kwasababu ya kuwa mtoto wa kwanza ni malango ya wazazi.Hivyo shetani hupiga vita kubwa sana malango hayo.Hivyo ni vema sana kuwaombea na kuwasaidia

Na kuongezea hata wakati wana wa Israeli walipokuwa wakidai kurudi kwao ,farao kibri kilimtoka baada ya kifo cha mtoto wake wa kwanza kama ikiwa ni adhabu kwa kuufanya moyo wake kuwa mgumu.
 
Habari ya mwisho wa mwezi.

Kuna familia nyingi nimeziona zikihangaika au kumkatia tamaa mzaliwa wa kwanza.Huyu mzaliwa wa kwanza anaishi kama mzaliwa wa mwisho.

Ingawa umri wake ni mkubwa kuliko wadogo zake lakin atapitwa maendeleo na wadogo zake.Wengine hupenda kubaki akiwalea wazazi wengine huwa hawana ramani.Huzalia nyumbani,chanzo cha familia kuyumba labda kuweka rehani nyumba kupata mkopo lakini hushindwa kulipa.Kwa wanaume huwa walevi na mateja kwa mijini.

Wengi huhisi kuwa katolewa kafara kwa ajiri ya wadogo zake(kiimani).

Je ni malezi,imani au mzaliwa wa kwanza huwa hivi?

JF na jamii kwa ujumla kama tuna watoto wa kwanza bado wadogo tuwakunje wangali wabichi.
Tafuta kitabu kilicho andikwa na Mwal.Christopher Mwakasege. Ameeleza mambo mengi yahusuyo mzaliwa wa kwanza na changamoto zake.

Kiufupi mzaliwa wa kwanza ndio lango la familia MUNGU analiangalia kupitisha baraka zake na shetani naye analiangalia apitishe mambo yake.

Tafuta hicho kitabu ujifunze, usisome kwa mlengo wa dini ila soma kwa maana ya kujifunza.
 
Na kuongezea hata wakati wana wa Israeli walipokuwa wakidai kurudi kwao ,farao kibri kilimtoka baada ya kifo cha mtoto wake wa kwanza kama ikiwa ni adhabu kwa kuufanya moyo wake kuwa mgumu.
Unaona sasa!Na sio mtoto wa kwanza wa farao tu,na wamisri wenzake walikufa watoto wao wa kwanza wote!walitolewa kafara kwa kiburi cha mtu mmoja! Inabidi kuwaombea kila siku na kuwapa kipaumbele katika maombi.Maana wanakabiliana na vita kali sana wasiyoijua
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom