Fikiria kama ARV zingekuwepo miaka ya 80 au 90

Fikiria kama ARV zingekuwepo miaka ya 80 au 90

DiasporaUSA

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2016
Posts
23,503
Reaction score
29,912
Umeshawahi Kuwaza ARVs zingekuwepo Miaka ya 80,90 Mwanzoni wa 2000 zingeokoa Maisha Ya Watu wangapi. ?

Raymond Titus Nyagori, binamu yangu niliempoteza Kwa HIV miaka 16 iliyopita, Ray was smart shuleni alikuwa namba 1 kila siku mpaka Tunamuonea wivu Sababu Alipendwa Sana na Bibi Yetu He was One of my favorite brothers, (cuzo)


Alikua akiishi Arusha na Baba Na Mama Yake na Wadogo zake 2. Mama ake Ray, (Aunt yangu) alikuwa Mgonjwa na kipindi chote anaumwa anapona Anaumwa anapona Hakuna aliekuwa akijua kama Ameathilika,


Ray alikuwa karibu sana na Mama Ake, Ray alikua anamuhudumia kwa Ukaribu Mama Ake hata alikua anaweza Mkata kucha Mama ake na Yeye akatumia Kiwembe kicho hicho kujikatia kucha zake.



Aunt alipojifungua Mtoto wake 3 aliumwa sana akafariki na Kumuacha Mtoto wake wa 3 mdogo ake wa Mwisho na Ray akiwa na Miezi 7, miaka hiyo kama Watoto tulikua hatuambiwi kwa Uwazi Juu ya Ugonjwa Huo.


Ray alikuja Dar Baada ya kuanza Kuumwa umwa Mara Kwa Mara. alikuwa form 1 anaelekea Form 2 lakini hakuweza Kwenda Shule Kwani Hali yake Ilikuwa inabadilika Badilika mno, Ray alikaa Nyumbani Mwaka Mzima bila Kwenda Shule.

kazi Yangu Kubwa Ilikuwa ni kumletea Madaftari nikirudi Likizo asome, na alikua akinifundisha vitu ambavyo sielewi japo yuko nyumbani alikua bado anaweza kusoma Na Kunisaidia Masomo mimi ninae enda Shule Kila Siku.

Acknowledgement.

Story hii ni kisa cha kweli kama ilivyosimuliwa na mwanadada mmoja.

Uzi tayari.
 
Sijaona heading Phrase kwenye Story. So inamaanisha ARVs vingekuwepo ina 80s and 90s Ray angekuwa anaishi kwa matumaini
 
hakika ARV ni moja ya mafanikio makubwa kwenye ulimwengu wa kitabibu.... I lost my aunt and my nephew dah...RIP.
 
Namkumbuka Shangazi yangu Mwalimu Rose. Aliondoka kwa ugonjwa huu miaka 19 iliyopita. ARV ingemsogezea maisha walau miaka kadhaa.
 
Inawezekana bado angekuwa amekufa kwa ugonjwa mwingine au sababu nyingine
 
Tupe ukweli. Hamna HIV wakati watu wanakufa kwa HIV. em tupe huo ukweli
ARV ndiyo zinazosababisha ukimwi nyie amkeni wabongo,hamjiulizi kwa nini zaidi ya 70% ya waathirika wanatoka Africa?? hakuna kitu kinachotwa hiv duniani,tafuteni ukweli, ukweli utawaweka huru
 
Tupe ukweli. Hamna HIV wakati watu wanakufa kwa HIV. em tupe huo ukweli
Maana ARV zmekuja baada ya HIV so kivipi ARV zisababishe UKIMWI. pia nnavojua wenye ukimwi ndio wanakunywa ARV.
 
ARV ndiyo zinazosababisha ukimwi nyie amkeni wabongo,hamjiulizi kwa nini zaidi ya 70% ya waathirika wanatoka Africa?? hakuna kitu kinachotwa hiv duniani,tafuteni ukweli, ukweli utawaweka huru
Huoni aibu kuleta ubishi wa kiswahili kwenye vitu serious?
 
ARVs ni muujiza mkubwa sana wa kibanadam,sababu toka mgonjwa wa Kwanza miaka ya 60 hadi leo watu zaidi ya milioni 30 wamekufa kwa sababu ya HIV.
 
Back
Top Bottom