FIFA yamuidhinisha Okwi kuichezea Young African

FIFA yamuidhinisha Okwi kuichezea Young African

Sijui mwenyekiti ataibuka na madai gani tena wakati huu! Safi sana YANGA
 
1. Dida / Barthez
2. Juma Abdul
3. Oscar Joshua
4. Rajab Zahir
5. Reliants Lusajo
6. Athuman Idd Chuji
7. Simon Msuva
8. Hassan Dilunga
9. Jerson Tegete
10. Said Bahanunzi
11. Hamis Kiiza

Hapo bado sijamuweka Nizar na Hamis Thabit
Umemsahau na Salum Telela mkuu.
 
Hiki ndicho kikosi cha kuwatoa waarabu koko wa misri.
1.Juma K Juma
2.Mbuyu Twite
3.Oscar Joshua
4.Nadri Cannavaro
5.Kelvin Yondani
6.Frank Domayo
7.Mrisho Ngassa
8.Haruna Niyonzima
9.Didier Kavumbagu
10.Emanuel Okwi
11.David Luhende

Benchi...........

Hii list c ndo ile iliopigwa goli 3 mpaka mkamkimbiza kocha au..?
 
attachment.php


Hivi hapa Okwi alikuwa anasema "kwa herini Simba" au alikuwa anamaanisha 5-0 ???
 
Wako wapi wale 'wachambuzi mahiri' wa soka walioshutumu, kudhihaki na kudhalilisha hatua za Yanga kumsajili Okwi? Ina maana zile hoja zao zote zilikuwa ni uchwara na batili? Walikiamini walichokuwa wakikiandika, waliandika ili kuvutia wasomaji, au waliandika kutokana na ushabiki wao tu dhidi ya Yanga? Mojawapo ya lolote kati ya hayo, maana yake ni kwamba tunalazimika kutokubaliana tena na uchambuzi wao ujao.

Wako wapi wale wanaosifiwa kwa kujua 'fitna za mpira' waliotoa viapo vinavyokaribiana na vya kufukua makaburi ya wapendwa wao iwapo Okwi angeichezea Yanga msimu huu? Ina maana vile viapo vyao vyote vilikuwa ni vya mdomoni tu, au waliamini walichokuwa wakikiapia? Maana yake ni kwamba hawataaminika tena mbele ya waliokariri viapo vyao, hasa wanachama, wapenzi na washabiki wa timu yao (ingawa hii si mara ya kwanza).

Wako wapi wale waliolumbana kwenye JF kwa kebehi na kejeli dhidi ya hoja zetu sahihi kwamba swala la Okwi kuichezea Yanga halihusiani hata kidogo na uhamisho wake wa Villa wala na madeni ya Simba kwa Etoile, kama vile kusivyokuwa na uhusano baina ya kisiki alichojikwaa mwendaji wa miguu na mahali alikoangukia? Maana yake ni kwamba kuna tofauti baina ya malumbano na mjadala. Mjadala hautumii fikira za utashi (wishful thinking) wa mtu, bali uhalisia wenye malengo (objective facts). Inshalla watajirudi kwenye mijadala ijayo ili isigeuke kuwa malumbano.

Wako wapi wale waliosema kwa vinywa vipana kwamba kulikuwa na mchezo mchafu kwenye swala zima la uhamisho wa Okwi kwenda Yanga, licha ya hoja bayana na mifano timamu kutoka kwa wahusika ambao bila ya shaka wana uelewa zaidi na kwa hivyo ndio wa kuaminiwa kuhusu swala hili kuliko wababaishaji wetu waliojivika majoho ya weledi wa mambo waliyoyadandia ukibwani ili kuganga njaa zao?

Yote kwa yote, tujifunze kupima ukweli wa mambo kwa uzito wa hoja zitolewazo na si kwa ukubwa wa vinywa (midomo) vya watoa hoja.
 
Hivi wakati Yanga inapigwa 3 na Mnyama mkali Okwi hakuwepo? Kuwafunga Wakojani sijui Wangazija wale ambao kazi yao ni uvuvi tu sio sawa na kuwafunga Wamisri au Simba SC.

Ukiwauliza Wamisri ni timu gani Tanzania bado wanaikumbuka kwa Umafia waliofanyiwa 2003 tena kwenye uwanja wao wa nyumbani watakujibu hawataki hata kusikia jina la Simba SC. Hahahaaaaaaaaaaaaaaa....pana chezea mzee wa kupiga njano 5 veve heeeee....hata Obama na ile rais staafu naitwa Bush najua.
 
Hivi wakati Yanga inapigwa 3 na Mnyama mkali Okwi hakuwepo? Kuwafunga Wakojani sijui Wangazija wale ambao kazi yao ni uvuvi tu sio sawa na kuwafunga Wamisri au Simba SC.

Ukiwauliza Wamisri ni timu gani Tanzania bado wanaikumbuka kwa Umafia waliofanyiwa 2003 tena kwenye uwanja wao wa nyumbani watakujibu hawataki hata kusikia jina la Simba SC. Hahahaaaaaaaaaaaaaaa....pana chezea mzee wa kupiga njano 5 veve heeeee....hata Obama na ile rais staafu naitwa Bush najua.

Alikuwa hajaidhinishwa na TFF & FIFA, sasa kazi tu.
 
Waache Wapige Kelele Hapo Sijaona Kikosi Cha Kuwafunga Waarabu. Inaonekana Okwi Sasa Amekuwa Mungu Wenu

Acha hasira mlisema OKwi hatocheza Yanga idhini imetoka mnasema tumemfanya MUNGU mtu aaaaaah mtani
 
Waache Wapige Kelele Hapo Sijaona Kikosi Cha Kuwafunga Waarabu. Inaonekana Okwi Sasa Amekuwa Mungu Wenu

Hata Simba walisema wataifunga Mgambo Shooting, kilichotokea tunajua wote. Mlisema kamwe Okwi hatacheza Yanga, sasa karuhusiwa. Hans papa alisema Okwi atacheza Mtani Jembe pekee, sasa atakipiga kwenye ligi hadi CAF. Kwa mara nyingine Rage et al. wameaibika tena; hiki ndicho kiini cha furaha yetu! Yanga oyee na Simba zii.
 
Waache Wapige Kelele Hapo Sijaona Kikosi Cha Kuwafunga Waarabu. Inaonekana Okwi Sasa Amekuwa Mungu Wenu

Wanajipa moyo hawa gongo wazi a.k.a kandambili a.k.a yebo yebo.. Watapigwa nje na ndani na El Ahly..
 
Back
Top Bottom