Ferooz alitupiga!

Ferooz alitupiga!

Kalamu Nzito

JF-Expert Member
Joined
Aug 13, 2015
Posts
376
Reaction score
850
Wimbo wa Ferooz maarufu kama “Wema wangu umeniponza” ni wimbo unaosimulia namna dhamana ilimponza mtunzi. Ferooz anamuwekea dhamana rafiki yake ambaye alikamatwa kwa kosa la jinai. Baada ya kutolewa kwa dhamana, rafiki yake anatumia mwanya huo kutokomea kusikojulikana. Ferooz, akiwa kama mdhamini wa mtuhumiwa, anakamatwa na kuhukumiwa kifungo cha maisha.

Kiuhalisia, kumuwekea mtu dhamana haimaanishi kwamba unabeba tuhuma au mashitaka yake. Hivyo, mdhamini hawezi kuhukumiwa kwa makosa ya mtuhumiwa/mshitakiwa pale ambapo mtuhumiwa/mshitakiwa huyo atatoroka. Mdhamini atawajibika kwa kiasi cha fedha au mali aliyotumia kuweka dhamana hiyo tu.

Licha ya kasoro hiyo, wimbo ni mzuri sana na unaishi mpaka leo kwani, unaangazia ukweli mchungu wa namna gani tunaweza kuumizwa kwa kutenda wema.
 
Fasihi siyo lazima itoe ujumbe wa moja kwa moja au wa aina moja kwa watu wote. Sema huo ni mtazamo na uelewa wako.

Hatuwezi kupindisha facts kisa fasihi. Suala la dhamana ni suala la kisheria. Lazima tutazame kitaaluma pia na sio kifasihi tu ili uburudike. Natumaini umepata kitu.
 
Hatuwezi kupindisha facts kisa fasihi. Suala la dhamana ni suala la kisheria. Lazima tutazame kitaaluma pia na sio kifasihi tu ili uburudike. Natumaini umepata kitu.
Hujaelewa hoja mkuu!

Halafu hujui fasihi! Naona kwako fasihi ni kuburudisha TU!
 
Hujaelewa hoja mkuu!

Halafu hujui fasihi! Naona kwako fasihi ni kuburudisha TU!

Wewe ndo hujanielewa. Mimi nimeutazama wimbo katika jicho la kitaaluma (taaluma ya sheria). Fasihi ni jicho lingine kabisa.
 
Kitmbo hicho hii ngoma nlijua ni hali halisi. Ilinitoa machozi kabla ya kujua sanaa ni nini
 
Wimbo wa Ferooz maarufu kama “Wema wangu umeniponza” ni wimbo unaosimulia namna dhamana ilimponza mtunzi. Ferooz anamuwekea dhamana rafiki yake ambaye alikamatwa kwa kosa la jinai. Baada ya kutolewa kwa dhamana, rafiki yake anatumia mwanya huo kutokomea kusikojulikana. Ferooz, akiwa kama mdhamini wa mtuhumiwa, anakamatwa na kuhukumiwa kifungo cha maisha.

Kiuhalisia, kumuwekea mtu dhamana haimaanishi kwamba unabeba tuhuma au mashitaka yake. Hivyo, mdhamini hawezi kuhukumiwa kwa makosa ya mtuhumiwa/mshitakiwa pale ambapo mtuhumiwa/mshitakiwa huyo atatoroka. Mdhamini atawajibika kwa kiasi cha fedha au mali aliyotumia kuweka dhamana hiyo tu.

Licha ya kasoro hiyo, nyimbo ni nzuri sana na inaishi mpaka leo kwani, inaangazia ukweli mchungu wa namna gani tunaweza kuumizwa kwa kutenda wema.
Haya weka hayo maneno unayotaka katika wimbo tukuchangie ukarekodi na wewe sasa.

Sent from my Infinix X693 using JamiiForums mobile app
 
Hatuwezi kupindisha facts kisa fasihi. Suala la dhamana ni suala la kisheria. Lazima tutazame kitaaluma pia na sio kifasihi tu ili uburudike. Natumaini umepata kitu.
Walimu wako walikuwa na kazi sana!
 
Back
Top Bottom