Felix Mkosamali (Case study)

Felix Mkosamali (Case study)

Huyo dogo noma,alimgaragaza milionea Jamar Tamimu tajiri la kibondo (ccm) kuanzia kwenye uchaguzi hadi mahakamani.Big up dogo!
 
Kijana FELIX anayyo sio wote walipata,yaani yeye ni mtu makini na tofauti,sio zile One za kuiba pepe za wengine siku hizi,Mimi namuunga Mkono kujisifia ndio kujiamini,katika hadhara lazima ujiamini,Hata mie niliipata sekondari na nipo mbaliii,kimaisha...Elimu ndio ufunguo..,na ni wa huko Kigoma pia,Mie nawaambia waha wote WASOME SAAANA,familia ni maskini,mkoa ni maskini..ILI HATIMAE TUINUE MKOA WETU...HONGERA SANA MKOSAMALI.
Tatizo la huyu ni kila anapotaka kujenga hoja kujitapa kuwa alipata Div. I ya digrii ya sheria! Namkumbusha kuwa Div.I aliyopata isiwe nguvu ya hoja ya kutaka mawazo yake yakubaliwe!

Kuna wengi ambao wahakufanikiwa kupata Div. I au kuwa na elimu ya chini kuliko yake lakini wanajenga hoja za nguvu katika kutetea wananchi wao na maslahi ya Taifa!
 
Huyu muheshimiwa namkubali sana ,,maana anahoja nzito sana na sijawahi kuona anaongea pumba na anaongea kwa vitendo huku mwili mzima ukionyesha msisitizo,,mfano alimshahuri mama yake ANNA TIBA IJUKA,,,,awalete wasomi waliomaliza degree za sheria jimboni kwakwe ili wasaidie kutatua migogoro ya ardhi ,,majengo atawapatia ,,,,mfano mzuri wakuigwa katika jamii
 
Tatizo la huyu ni kila anapotaka kujenga hoja kujitapa kuwa alipata Div. I ya digrii ya sheria! Namkumbusha kuwa Div.I aliyopata isiwe nguvu ya hoja ya kutaka mawazo yake yakubaliwe!

Kuna wengi ambao wahakufanikiwa kupata Div. I au kuwa na elimu ya chini kuliko yake lakini wanajenga hoja za nguvu katika kutetea wananchi wao na maslahi ya Taifa!
WANI zina utofauti wake mkuu kuna ile ya 7 na ya 17 ya vilaza. ha ha ha
 
2015 jimba la zito atachukua mwalimu wake wa siasa YARED FUBUSA subiri Tundu lisu no 2
 
Kijana FELIX anayyo sio wote walipata,yaani yeye ni mtu makini na tofauti,sio zile One za kuiba pepe za wengine siku hizi,Mimi namuunga Mkono kujisifia ndio kujiamini,katika hadhara lazima ujiamini,Hata mie niliipata sekondari na nipo mbaliii,kimaisha...Elimu ndio ufunguo..,na ni wa huko Kigoma pia,Mie nawaambia waha wote WASOME SAAANA,familia ni maskini,mkoa ni maskini..ILI HATIMAE TUINUE MKOA WETU...HONGERA SANA MKOSAMALI.
Nakuunga mkono kuwa tunahitaji vijana wetu kusoma sana ili taifa liondokane na ujinga!

Hoja yangu hapa ni uwezo wake wa kujenga hoja kwa hekima na busara! Ili mtu ajiamini mbele za watu si lazima ajisifie bali watu wanaomsikiliza na kumuona wamsifie! Kwa kujisifu mwenyewe kunaonyesha udhaifu wako na kutojiamini na ndiyo sababu unalazimika kutangaza bila kuulizwa uwezo wako wa elimu, fedha na rasilimali zingine!

Kifupi naweza ku-conclude kuwa Mkosamali ni dhaifu!
 
anafanya kazi nzuri sana ila namshauri apunguze jazba. akipunguza jazba atatisha sana. avae hisia kali kama kawaida yake lkn apunguze hasira na jazba. akimuiga lissu amekwisha. nataka awaige zitto na mnyika
 
the first product of saut graduate.amefungua njia subirin product zingine za DR KITIMA 2015..SAUT YA WENG NI SAUTI YA MUNGU.
 
1667.jpg

Felix Francis Mkosamali, Mbunge wa Jimbo la Muhambwe kwa tiketi ya Chama cha NCCR-Mageuzi, ni mbunge mdogo wa Jimbo katika Bunge la sasa, ambapo ana miaka 27.

Mwanasheria Msomi kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino kilichopo jijini Mwanza.

Kijana huyu mbunge aliweza kugombea na kupata jimbo la Muhambwe kwa kutumia fedha alizokopeshwa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu kumsaidia kuzunguka huku na kule ili kuwafikia wapiga kura. Pia

fedha nyingine zilizomsaidia wakati wa harakati za kampeni alizipata kwa kufundisha katika shule ya sekondari ya wasichana Boniconcili, ambapo alikuwa mwalimu wa muda (Part Time).
Pamoja na kuingia bungeni kwa taabu kijana huyu tunamwona kila siku anavyojitahidi kuisimamia serikali bila woga kwa kuchangia hoja zenye mashiko na kuonesha upeo wa kisomi katika uchangiaji hoja kwa nidhamu ya hali ya juu.
Somo (case study) kwa vijana kutoka kwa Mkosamali :

1. Siku zote penye nia pana njia. Pamoja na kidogo ukipatacho ukiwa na nidhamu na malengo dunduliza utimize
malengo yako. Kwani haba na haba hujaza kibaba.
2. Acha maisha tegemezi na uangalie fursa ulizo nazo uzitumie ili kutimiza malengo yako. i.e kama una kipaji
chochote jitahidi kukifanyia kazi na usibweteke
3. Woga ni dhambi kubwa sana, siku zote usitishwe na kitu chochote unapokuwa umesimamia ukweli, jidhihirishe wazi
nia yako na tetea haki yako bila kusaliti wenzio. Kumbuka kuwa mzalendo na kuitetea nchi yako kwani vijana ndio
watakaoleta mabadiliko katika nchi yetu. Naomba kuwakilisha.

Give credit where it's due. Nilimsikia akichangia kuhusu budget ya elimu in relation to matokeo ya Form Four niliukubali mchago wake maana aliongea bila kumungunya maneno. Na consistency yake haikuwa flawed na wabunge wa CCM waliojifanya kuomba mwongozo wa speaker. Yule mbunge wa Bukoba Vijijini kwa kweli ni msaliti wa wapiga kura wake maana yuko tayari kusema nyeusi ni nyeupe wakati kila mtu anaona ni nyeusi maana aliomba mwongozo ili kumvuruga kijana wetu. Nafikiri if NCCR work jointly with CDM we can lead the country to desired renaissance that is inclusive.
 
Nakuunga mkono kuwa tunahitaji vijana wetu kusoma sana ili taifa liondokane na ujinga!

Hoja yangu hapa ni uwezo wake wa kujenga hoja kwa hekima na busara! Ili mtu ajiamini mbele za watu si lazima ajisifie bali watu wanaomsikiliza na kumuona wamsifie! Kwa kujisifu mwenyewe kunaonyesha udhaifu wako na kutojiamini na ndiyo sababu unalazimika kutangaza bila kuulizwa uwezo wako wa elimu, fedha na rasilimali zingine!

Kifupi naweza ku-conclude kuwa Mkosamali ni dhaifu!
Kujisifia sio vizuri katika maisha lakini wakati mwingine inategemea mtu anajisifia katika mazingira gani and for which purpose. Wakati anasema yeye alipata point 7 kwanza kama sikosei alitumia plural pronoun ya "we". 'Mpaka wengine tukapata point 7" na hapo alikuwa anamsifia Mama Ndalichako kwa kuweka reliable control mechanism kwenye mitihani kiasi kwamba hakuna leakage. Kwa hiyo kujisifia kwake kulikuwa compliance na hoja aliyokuwa anaitetea na context haikuwa kuwatukana labda ambao hawakupata one au kutokusoma maana alikuwa anaikemea serikali pamoja na wabunge wanaoshabikia kuwa elimu imeboreka wakati matokeo ni fragile and have exposed the government and its compatriots who have been blowing trumpets in the so called improvement and growth in education while they and theirs are not studying in the respective school. With this end in view huwezi kumwita Mkosamali dhaifu
 
Tatizo la huyu ni kila anapotaka kujenga hoja kujitapa kuwa alipata Div. I ya digrii ya sheria! Namkumbusha kuwa Div.I aliyopata isiwe nguvu ya hoja ya kutaka mawazo yake yakubaliwe!

Kuna wengi ambao wahakufanikiwa kupata Div. I au kuwa na elimu ya chini kuliko yake lakini wanajenga hoja za nguvu katika kutetea wananchi wao na maslahi ya Taifa!

Mkuu hakuna Div. I katika vyuo vikuu na sina hakika kama ana first class maana hazipatikani pia kirahisi labda uende sijui ...tafuta mwenyewe mod asijenipiga ban kuwa sijafanya utafiti wa kutosha
 
Back
Top Bottom