FCC yasema suala la Muungano wa Mwekezaji na Simba wameshalifunga

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464

Akifafanua hali ya sintofahamu inayoendelea kuhusu mchakato wa uwekezaji unaendelea kati ya Klabu ya Simba na mwekezaji Mohamed Dewji ‘Mo’, Mkurugenzi Mkuu Tume ya Ushindani (FCC), William Erio amesema kinachoangaliwa na watu wengi ni upande wa Mwekezaji na kusahau kuhusu kile kinachotakiwa kufanywa na Klabu ya Simba.

Amesema “Walipewa masharti ya Mwekezaji na yale ya Simba, walipokamilisha tukatoa cheti kuwa muungano umepitishwa na klichoombwa kimeridhiwa, kinachofuata ni utekelezaji.”

Ameongeza “Wiki mbili zilizopita upande wa Klabu (Baraza la Wadhamini wa Klabu) waliitwa RITA (Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini) wakitakiwa kuweka Hati za Jengo la Klabu zote ziwe mali mali ya Simba Sports Club Limited, sijajua nini kimeendelea huko.”
 
Ngoja tusubiri tuone kama Mzee Kilomoni atakubali kirahisi tu kutoa hizo hati za jengo kwa mwekezaji.
 
Ngoja tusubiri tuone kama Mzee Kilomoni atakubali kirahisi tu kutoa hizo hati za jengo kwa mwekezaji.
Hujaelewa hata hati zinatakiwa wapi. Hii elimu kuhusu hisa inabidi ienezwe kwanza maana wapo watu kama hawa hawaelewi lolote
 
Hujaelewa hata hati zinatakiwa wapi. Hii elimu kuhusu hisa inabidi ienezwe kwanza maana wapo watu kama hawa hawaelewi lolote
Nyinyi hangaikeni tu. Ila mwisho wa siku hati ya jengo haitolewi ng'o! Siyo kwa mwekezaji, au kampuni.
 
Back
Top Bottom