fakalava
JF-Expert Member
- Jul 16, 2015
- 4,459
- 6,031
Huyu jamaa kabla ya kuokoka alikuwa ni jambazi wa kuogopwa hapa Tanzania na baadhi ya nchi jirani. Kwa hapa Tanzania alipatikana zaidi Keko (Dar es laam), Moshi (Kilimanjaro), Unga Limited (Arusha).
Alifanya matukio mengi ya ujambazi na kufanikiwa, lakini kuna matukio mengi alinusurika kifo ndiyo maana uso wake mpaka sasa umejaa makovu.
Mwishowe aliacha ujambazi na kuokoka akaamia Nairobi, akaanzisha kanisa na kuwa muimbaji. Kuna marafiki zake wakina Malebo, Mrefu pamaja na wanawake kadhaa ambao kati ya hao, Mrefu, pamoja na wanawake wawili alifanikiwa kuwashawishi wakaokoka lakini Malebo alikuwa kisiki cha Mpingo mpaka akaamua kumtungia wimbo.
Mpaka sasa kitu ambacho sikijui ni je, huyu Malebo alifanikiwa kuokoka na kuwa kondoo wa bwana au lah?